< Kutoka 26 >

1 “Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo.
Moreover, thou shalt make the tabernacle [with] ten curtains [of] fine twined linen, and blue, and purple, and scarlet: [with] cherubim of curious work shalt thou make them.
2 Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
The length of one curtain [shall be] eight and twenty cubits, and the breadth of one curtain four cubits: and every one of the curtains shall have one measure.
3 Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
The five curtains shall be coupled together one to another; and [other] five curtains [shall be] coupled one to another.
4 Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
And thou shalt make loops of blue upon the edge of the one curtain from the selvedge in the coupling; and likewise shalt thou make in the uttermost edge of [another] curtain, in the coupling of the second.
5 Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane.
Fifty loops shalt thou make in the one curtain, and fifty loops shalt thou make in the edge of the curtain that [is] in the coupling of the second; that the loops may take hold one of another.
6 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.
And thou shalt make fifty buttons of gold, and couple the curtains together with the buttons: and it shall be one tabernacle.
7 “Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
And thou shalt make curtains [of] goats' [hair] to be a covering upon the tabernacle: eleven curtains shalt thou make.
8 Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
The length of one curtain [shall be] thirty cubits, and the breadth of one curtain four cubits: and the eleven curtains [shall be all] of one measure.
9 Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani.
And thou shalt couple five curtains by themselves, and six curtains by themselves, and shalt double the sixth curtain in the front of the tabernacle.
10 Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
And thou shalt make fifty loops on the edge of the one curtain [that is] outmost in the coupling, and fifty loops in the edge of the curtain which coupleth the second.
11 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
And thou shalt make fifty buttons of brass, and put the buttons into the loops, and couple the tent together, that it may be one.
12 Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema.
And the remnant that remaineth of the curtains of the tent, the half curtain that remaineth, shall hang over the backside of the tabernacle.
13 Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.
And a cubit on the one side, and a cubit on the other side of that which remaineth in the length of the curtains of the tent, shall hang over the sides of the tabernacle on this side and on that side, to cover it.
14 Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
And thou shalt make a covering for the tent, [of] rams' skins dyed red, and a covering above [of] badgers' skins.
15 “Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
And thou shalt make boards for the tabernacle [of] shittim wood standing up.
16 Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
Ten cubits [shall be] the length of a board, and a cubit and a half [shall be] the breadth of one board.
17 zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
Two tenons [shall there be] in one board, set in order one against another: thus shalt thou make for all the boards of the tabernacle.
18 Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
And thou shalt make the boards for the tabernacle, twenty boards on the south side southward.
19 kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
And thou shalt make forty sockets of silver under the twenty boards; two sockets under one board for its two tenons, and two sockets under another board for its two tenons.
20 Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
And for the second side of the tabernacle on the north side [there shall be] twenty boards:
21 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
And their forty sockets [of] silver; two sockets under one board, and two sockets under another board.
22 Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
And for the sides of the tabernacle westward thou shalt make six boards.
23 na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
And two boards shalt thou make for the corners of the tabernacle in the two sides.
24 Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
And they shall be coupled together beneath, and they shall be coupled together above the head of it to one ring: thus shall it be for them both; they shall be for the two corners.
25 Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
And they shall be eight boards, and their sockets [of] silver, sixteen sockets; two sockets under one board, and two sockets under another board.
26 “Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
And thou shalt make bars [of] shittim wood; five for the boards of the one side of the tabernacle,
27 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
And five bars for the boards of the other side of the tabernacle, and five bars for the boards of the side of the tabernacle, for the two sides westward.
28 Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
And the middle bar in the midst of the boards shall reach from end to end.
29 Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
And thou shalt overlay the boards with gold, and make their rings [of] gold [for] places for the bars; and thou shalt overlay the bars with gold.
30 “Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
And thou shalt rear up the tabernacle according to the fashion thereof which was shown thee on the mount.
31 “Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
And thou shalt make a vail [of] blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen of curious work: with cherubim shall it be made.
32 Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.
And thou shalt hang it upon four pillars of shittim [wood] overlaid with gold: their hooks [shall be of] gold, upon the four sockets of silver.
33 Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.
And thou shalt hang the vail under the buttons, that thou mayst bring in thither within the vail the ark of the testimony: and the vail shall divide to you between the holy [place] and the most holy.
34 Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.
And thou shalt put the mercy-seat upon the ark of the testimony, in the most holy [place].
35 Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.
And thou shalt set the table without the vail, and the candlestick over against the table on the side of the tabernacle towards the south: and thou shalt put the table on the north side.
36 “Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
And thou shalt make a hanging for the door of the tent, [of] blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen, wrought with needle work.
37 Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.
And thou shalt make for the hanging five pillars [of] shittim [wood], and overlay them with gold, [and] their hooks [shall be of] gold: and thou shalt cast five sockets of brass for them.

< Kutoka 26 >