< Kutoka 24 >

1 Kisha Mungu akamwambia Mose, “Njooni huku juu kwa Bwana, wewe na Aroni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli. Mniabudu kwa mbali,
He said to Moses, "Come up to Jehovah, you, and Aaron, Nadab, and Abihu, and seventy of the elders of Israel; and worship from a distance.
2 lakini Mose peke yake ndiye atakayemkaribia Bwana; wengine wasije karibu. Nao watu wasije wakapanda pamoja naye.”
Moses alone shall come near to God, but they shall not come near, neither shall the people go up with him."
3 Mose alipokwenda na kuwaambia watu maneno yote na sheria zote za Bwana, wakaitikia kwa sauti moja, “Kila kitu alichosema Bwana tutakifanya.”
Moses came and told the people all the words of God, and all the ordinances; and all the people answered with one voice, and said, "All the words which Jehovah has spoken will we do."
4 Ndipo Mose akaandika kila kitu Bwana alichokuwa amesema. Akaamka kesho yake asubuhi na mapema na kujenga madhabahu chini ya mlima na kusimamisha nguzo kumi na mbili za mawe kuwakilisha makabila kumi na mawili ya Israeli.
Moses wrote all the words of Jehovah, and rose up early in the morning, and built an altar under the mountain, and twelve pillars for the twelve tribes of Israel.
5 Kisha akawatuma vijana wanaume wa Kiisraeli, nao wakatoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu za mafahali wachanga kuwa sadaka za amani kwa Bwana.
He sent young men of the children of Israel, who offered burnt offerings and sacrificed peace offerings of cattle to God.
6 Mose akachukua nusu ya damu ya wale wanyama na kuiweka kwenye mabakuli na nusu nyingine akainyunyiza juu ya madhabahu.
Moses took half of the blood and put it in basins, and half of the blood he sprinkled on the altar.
7 Kisha akachukua kile Kitabu cha Agano na kuwasomea watu. Nao wakajibu, “Tutafanya kila kitu alichosema Bwana, nasi tutatii.”
He took the book of the covenant and read it in the hearing of the people, and they said, "All that Jehovah has spoken will we do, and be obedient."
8 Ndipo Mose akachukua ile damu, akawanyunyizia wale watu, akasema, “Hii ni damu ya agano ambalo Bwana amelifanya nanyi kufuatana na maneno haya yote.”
Moses took the blood, and sprinkled it on the people, and said, "This is the blood of the covenant, which God has commanded you concerning all these words."
9 Mose na Aroni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli wakapanda mlimani,
Then Moses, Aaron, Nadab, Abihu, and seventy of the elders of Israel went up.
10 nao wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa na kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, iliyo safi kama anga angavu.
They saw the God of Israel. Under his feet was like a paved work of sapphire stone, like the skies for clearness.
11 Lakini Mungu hakuinua mkono wake dhidi ya hawa viongozi wa Waisraeli; walimwona Mungu, nao wakala na kunywa.
He did not lay his hand on the nobles of the children of Israel. They saw God, and ate and drank.
12 Bwana akamwambia Mose, “Panda uje kwangu huku mlimani na ukae hapa, nami nitakupa vibao vya mawe, vyenye sheria na amri ambazo nimeziandika ziwe mwongozo wao.”
Jehovah said to Moses, "Come up to me on the mountain, and stay here, and I will give you the tablets of stone with the law and the commands that I have written, that you may teach them."
13 Basi Mose akaondoka na Yoshua mtumishi wake, naye Mose akapanda juu kwenye mlima wa Mungu.
Moses rose up with Joshua, his servant, and Moses went up onto God's Mountain.
14 Mose akawaambia wazee wa Israeli, “Tungojeni hapa mpaka tutakapowarudia. Aroni na Huri wako pamoja nanyi, na kila aliye na neno aweza kuwaendea wao.”
He said to the elders, "Wait here for us, until we come again to you. Look, Aaron and Hur are with you. Whoever is involved in a dispute can go to them."
15 Mose alipopanda juu mlimani, wingu liliufunika huo mlima,
Moses went up on the mountain, and the cloud covered the mountain.
16 nao utukufu wa Bwana ukatua juu ya Mlima Sinai. Kwa muda wa siku sita wingu lilifunika mlima, na siku ya saba Bwana akamwita Mose kutoka katikati ya lile wingu.
The glory of God settled on Mount Sinai, and the cloud covered it six days. The seventh day he called to Moses out of the midst of the cloud.
17 Kwa Waisraeli utukufu wa Bwana ulionekana kama moto uteketezao juu ya mlima.
The appearance of the glory of Jehovah was like devouring fire on the top of the mountain in the eyes of the children of Israel.
18 Kisha Mose akaingia ndani ya lile wingu alivyokuwa akipanda mlimani. Naye akakaa huko mlimani kwa muda wa siku arobaini, usiku na mchana.
Moses entered into the midst of the cloud, and went up on the mountain; and Moses was on the mountain forty days and forty nights.

< Kutoka 24 >