< Kutoka 21 >

1 “Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli:
A ovo su zakoni koje æeš im postaviti:
2 “Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
Ako kupiš roba Jevrejina, šest godina neka ti služi, a sedme nek otide slobodan bez otkupa.
3 Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye.
Ako bude došao inokosan, neka i otide inokosan; ako li bude imao ženu, neka ide i žena s njim.
4 Kama bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
Ako ga gospodar njegov oženi, i žena mu rodi sinove ili kæeri, žena s djecom svojom neka bude gospodaru njegovu, a on neka otide sam.
5 “Lakini kama mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
Ako li rob reèe tvrdo: ljubim gospodara svojega, ženu svoju i djecu svoju, neæu da idem da budem slobodan,
6 ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
Onda neka ga dovede gospodar njegov pred sudije i postavi na vratima ili kod dovratka, i ondje neka mu gospodar probuši uho šilom, pa neka mu robuje dovijeka.
7 “Kama mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume waachiwavyo.
Ako ko proda kæer svoju da bude robinja, da ne odlazi kao robovi što odlaze.
8 Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
Ako ne bude po volji gospodaru svojemu, i on je ne uzme za ženu, neka je pusti na otkupe; ali da nema vlasti prodati je u tuð narod uèinivši joj nevjeru.
9 Kama akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
Ako li je zaruèi sinu svojemu, da joj uèini po pravu koje imaju kæeri.
10 Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
Ako li uzme drugu, da joj ne umali hrane ni odijela ni zajednice.
11 Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
Ako joj ovo troje ne uèini, onda nek otide bez otkupa.
12 “Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
Ko udari èovjeka, te umre, da se pogubi.
13 Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
Ako li ne bude htio, nego mu ga Bog dade u ruke, odrediæu ti mjesto kuda može uteæi.
14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
Ako bi ko nahvalice ustao na bližnjega svojega da ga ubije iz prijevare, odvuci ga i od oltara mojega da se pogubi.
15 “Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Ko udari oca svojega ili mater svoju, da se pogubi.
16 “Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
Ko ukrade èovjeka i proda ili se naðe u njegovijem rukama, da se pogubi.
17 “Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Ko opsuje oca svojega ili mater svoju, da se pogubi.
18 “Kama watu wakigombana na mmoja akimpiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa bali akaugua na kulala kitandani,
Kad se svade ljudi, pa jedan udari drugoga kamenom ili pesnicom, ali onaj ne umre nego padne u postelju,
19 yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia kama mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda wake aliopoteza na awajibike mpaka apone kabisa.
Ako se pridigne i izaðe o štapu, da ne bude kriv onaj koji je udario, samo dangubu da mu naknadi i svu vidarinu da plati.
20 “Kama mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
Ko udari roba svojega ili robinju štapom tako da mu umre pod rukom, da je kriv;
21 lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
Ali ako preživi dan ili dva, da nije kriv, jer je njegov novac.
22 “Ikiwa watu wawili wanapigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
Kad se svade ljudi, pa koji od njih udari trudnu ženu tako da izaðe iz nje dijete, ali se ne dogodi smrt, da plati globu koliko muž ženin reèe, a da plati preko sudija;
23 Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
Ako li se dogodi smrt, tada æeš uzeti život za život,
24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
Oko za oko, zub za zub, ruku za ruku, nogu za nogu,
25 kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
Užeg za užeg, ranu za ranu, modricu za modricu.
26 “Ikiwa mtu atampiga mtumwa mwanaume au mwanamke kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
Ako ko udari po oku roba svojega ili robinju svoju, te mu pokvari oko, da ga otpusti slobodna za oko njegovo.
27 Kama akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
I ako izbije zub robu svojemu ili robinji svojoj, da ga pusti slobodna za zub njegov.
28 “Kama fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
Ako vo ubode èovjeka ili ženu, te umre, da se vo zaspe kamenjem i da se ne jede meso od njega, a gospodar od vola da nije kriv.
29 Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
Ali ako je vo prije bio bodaè i gospodar njegov znao za to pa ga nije èuvao, te ubije èovjeka ili ženu, vo da se zaspe kamenjem, i gospodar njegov da se pogubi.
30 Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
Ako mu se odredi da se otkupi, neka da otkup za život svoj, koliko mu se odredi.
31 Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
Ako ubode sina ili kæer, da mu bude po istom zakonu.
32 Ikiwa fahali atampiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
Ako li roba ubode vo ili robinju, da da gospodaru njihovu trideset sikala srebra i vo da se zaspe kamenjem.
33 “Kama mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ngʼombe au punda akatumbukia ndani yake,
Ako ko otkrije jamu ili iskopa jamu a ne pokrije, pa upadne vo ili magarac,
34 mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
Da naknadi gospodar od jame i plati novcem gospodaru njihovu, a što je uginulo da je njegovo.
35 “Kama fahali wa mtu fulani atamuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
Ako vo jednoga ubode vola drugome, te pogine, onda da prodadu vola živoga i novce da podijele, tako i ubijenoga vola da podijele.
36 Hata hivyo, kama ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
Ako li se znalo da je vo prije bio bodaè pa ga nije èuvao gospodar njegov, da da vola za vola, a ubijeni neka bude njemu.

< Kutoka 21 >