< Kutoka 14 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
2 “Waambie Waisraeli wageuke nyuma na wapige kambi karibu na Pi-Hahirothi, kati ya Migdoli na bahari. Watapiga kambi kando ya bahari, mkabala na Baal-Sefoni.
Speak unto the children of Israel, that they turn and encamp before Pi-hahiroth, between Migdol and the sea: before Baal-Zephon, opposite to it, shall ye encamp by the sea.
3 Farao atafikiri kwamba, ‘Hao Waisraeli wanatangatanga katika nchi kwa kuchanganyikiwa, nalo jangwa limewafungia.’
And Pharaoh will say of the children of Israel, They are entangled in the land, the wilderness has hemmed them in.
4 Nami nitaufanya moyo wa Farao mgumu, naye atawafuatilia. Lakini nitajipatia utukufu kwa ajili yangu mwenyewe kupitia Farao na jeshi lake lote, nao Wamisri watajua kuwa mimi ndimi Bwana.” Kwa hiyo Waisraeli wakafanya hivyo.
And I will harden Pharaoh's heart, that he may pursue after them; and I will glorify myself in Pharaoh, and in all his host; and the Egyptians shall know that I am Jehovah. And they did so.
5 Mfalme wa Misri alipoambiwa kuwa Waisraeli wamekimbia, Farao na maafisa wake wakabadili nia zao kuhusu Waisraeli, wakasema, “Tumefanya nini? Tumewaachia Waisraeli waende zao na tumeukosa utumishi wao!”
And it was told the king of Egypt that the people had fled; and the heart of Pharaoh and of his bondmen was turned against the people, and they said, Why have we done this, that we have let Israel go from our service?
6 Kwa hiyo akaandaliwa gari lake la vita, naye akaenda pamoja na jeshi lake.
And he yoked his chariot, and took his people with him.
7 Akachukua magari bora mia sita, pamoja na magari mengine yote ya Misri, pamoja na maafisa wa magari hayo yote.
And he took six hundred chosen chariots, and all the chariots of Egypt, and captains over every one of them.
8 Bwana akaufanya mgumu moyo wa Farao, mfalme wa Misri, kwa hiyo akawafuatia Waisraeli, waliokuwa wakiondoka Misri kwa ujasiri.
And Jehovah hardened the heart of Pharaoh king of Egypt, and he pursued after the children of Israel; and the children of Israel had gone out with a high hand.
9 Nao Wamisri, yaani farasi wote wa Farao na magari ya vita, wapanda farasi na vikosi vya askari, wakawafuatia Waisraeli, wakawakuta karibu na Pi-Hahirothi, mkabala na Baal-Sefoni walipokuwa wamepiga kambi kando ya bahari.
And the Egyptians pursued after them, — all the horses and chariots of Pharaoh, and his horsemen, and his army, and overtook them where they had encamped by the sea, beside Pi-hahiroth, opposite to Baal-Zephon.
10 Farao alipokaribia, Waisraeli wakainua macho yao, wakawaona Wamisri wakija nyuma yao. Wakashikwa na hofu, wakamlilia Bwana.
And Pharaoh approached; and the children of Israel lifted up their eyes, and behold, the Egyptians marched after them; and the children of Israel were much afraid, and cried out to Jehovah.
11 Wakamwambia Mose, “Je, ni kwamba hayakuwako makaburi huko Misri hata umetuleta tufe huku jangwani? Umetufanyia nini kututoa Misri?
And they said to Moses, Is it because there were no graves in Egypt, thou hast taken us away to die in the wilderness? why hast thou done this to us, that thou hast led us out of Egypt?
12 Hatukukuambia tulipokuwa huko Misri, tuache tuwatumikie Wamisri? Ingekuwa vyema zaidi kwetu kuwatumikia Wamisri kuliko kufa jangwani!”
Is not this what we told thee in Egypt, when we said, Let us alone, and we will serve the Egyptians? For [it had been] better for us to serve the Egyptians than to die in the wilderness.
13 Mose akawajibu Waisraeli, “Msiogope. Simameni imara, nanyi mtauona wokovu Bwana atakaowapatia leo. Hao Wamisri mnaowaona leo kamwe hamtawaona tena.
And Moses said to the people, Fear not: stand still, and see the salvation of Jehovah, which he will work for you to-day; for the Egyptians whom ye have seen to-day, ye shall see them again no more for ever.
14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mnatakiwa kutulia tu.”
Jehovah will fight for you, and ye shall be still.
15 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Kwa nini wewe unanililia? Waambie Waisraeli waendelee mbele.
And Jehovah said to Moses, Why dost thou cry unto me? Speak unto the children of Israel, that they go forward.
16 Inua fimbo yako na unyooshe mkono wako juu ya bahari ili kuyagawa maji, hivyo kwamba Waisraeli wapate kupita mahali pakavu baharini.
And thou, lift thy staff, and stretch out thy hand over the sea, and divide it; and the children of Israel shall go on dry [ground] through the midst of the sea.
17 Nitaifanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu kusudi waingie baharini wakiwafuatia. Nami nitajipatia utukufu kupitia Farao pamoja na jeshi lake lote, kupitia magari yake ya vita na wapanda farasi wake.
And I, behold, I will harden the hearts of the Egyptians, and they shall pursue after them; and I will glorify myself in Pharaoh and in all his host, in his chariots and in his horsemen.
18 Nao Wamisri watajua kwamba Mimi ndimi Bwana nitakapojipatia utukufu kupitia Farao, magari yake ya vita na wapanda farasi wake.”
And the Egyptians shall know that I am Jehovah, when I have glorified myself in Pharaoh, in his chariots and in his horsemen.
19 Ndipo malaika wa Mungu, aliyekuwa akisafiri mbele ya jeshi la Israeli, akaondoka akakaa nyuma yao. Pia ile nguzo ya wingu ikaondoka hapo mbele yao na kusimama nyuma,
And the Angel of God, who went before the camp of Israel, removed and went behind them; and the pillar of the cloud went from before them, and stood behind them.
20 ikakaa kati ya majeshi ya Misri na Israeli. Usiku kucha wingu likaleta giza upande mmoja na nuru kwa upande mwingine, kwa hiyo hakuna aliyemkaribia mwenzake usiku kucha.
And it came between the camp of the Egyptians and the camp of Israel; and was a cloud and darkness, and lit up the night; and the one did not come near the other all the night.
21 Ndipo Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, naye Bwana akayasukuma maji ya bahari nyuma kwa upepo mkali wa mashariki usiku ule wote na kupafanya nchi kavu. Maji yakagawanyika,
And Moses stretched out his hand over the sea; and Jehovah made the sea go [back] by a strong east wind all the night, and made the sea dry [land], and the waters were divided.
22 nao Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, maji yakiwa ukuta upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto.
And the children of Israel went through the midst of the sea on the dry [ground]; and the waters were a wall to them on their right hand and on their left.
23 Wamisri wakawafuatia ndani ya bahari, pamoja na farasi wote wa Farao, magari ya vita na wapanda farasi.
And the Egyptians pursued and came after them — all Pharaoh's horses, his chariots and his horsemen, into the midst of the sea.
24 Karibia mapambazuko, Bwana akaliangalia jeshi la Wamisri kutoka ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha.
And it came to pass in the morning watch, that Jehovah looked upon the camp of the Egyptians, in the pillar of fire and of the cloud, and embarrassed the camp of the Egyptians.
25 Mungu akayaondoa magurudumu ya magari yao, kwa hivyo wakayaendesha kwa shida. Nao Wamisri wakasema, “Tuachane na Waisraeli! Bwana anawapigania dhidi ya Misri.”
And he took off their chariot wheels, and caused them to drive with difficulty; and the Egyptians said, Let us flee before Israel, for Jehovah is fighting for them against the Egyptians!
26 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya bahari ili maji yarudiane yawafunike Wamisri, magari yao ya vita na wapanda farasi wao.”
And Jehovah said to Moses, Stretch out thy hand over the sea, that the waters may return upon the Egyptians, upon their chariots and upon their horsemen.
27 Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, wakati wa mapambazuko bahari ikarudiana na kuwa kama kawaida. Wamisri wakajaribu kuyakimbia maji, lakini Bwana akawasukumia ndani ya bahari.
And Moses stretched out his hand over the sea, and the sea returned to its strength toward the morning; and the Egyptians fled against it; and Jehovah overturned the Egyptians into the midst of the sea.
28 Maji yakarudiana na kuyafunika magari ya vita na wapanda farasi pamoja na jeshi lote la Farao lililokuwa limewafuata Waisraeli ndani ya bahari. Hakuna hata mmoja wao aliyenusurika.
And the waters returned, and covered the chariots and the horsemen of all the host of Pharaoh that had come into the sea after them; there remained not even one of them.
29 Lakini Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, ukiwepo ukuta wa maji upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto.
And the children of Israel walked on dry [ground] through the midst of the sea; and the waters were a wall to them on their right hand and on their left.
30 Siku ile Bwana akawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wamisri, nao Waisraeli wakawaona Wamisri wamelala ufuoni mwa bahari wakiwa wamekufa.
Thus Jehovah saved Israel that day out of the hand of the Egyptians; and Israel saw the Egyptians dead on the sea-shore.
31 Basi Waisraeli walipoona uwezo mkubwa Bwana aliodhihirisha dhidi ya Wamisri, watu wakamwogopa Bwana na wakaweka tumaini lao kwake na kwa Mose mtumishi wake.
And Israel saw the great power [with] which Jehovah had wrought against the Egyptians; and the people feared Jehovah, and believed in Jehovah, and in Moses his bondman.

< Kutoka 14 >