< Kutoka 13 >

1 Bwana akamwambia Mose,
I PAN powiedział do Mojżesza:
2 “Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”
Poświęć mi wszystko, co pierworodne. Wszystko, co otwiera łono u synów Izraela, tak wśród ludzi, jak i wśród bydła. To należy do mnie.
3 Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu.
Mojżesz powiedział więc do ludu: Pamiętajcie ten dzień, w którym wyszliście z Egiptu, z domu niewoli. PAN bowiem potężną ręką wyprowadził was stamtąd. Nie będziecie jeść nic kwaszonego.
4 Leo, katika mwezi wa Abibu, mnatoka.
Dziś wychodzicie, w miesiącu Abib.
5 Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu:
A gdy PAN wprowadzi cię do ziemi Kananejczyków, Chetytów, Amorytów, Chiwwitów i Jebusytów, którą przysiągł dać waszym ojcom, ziemię opływającą mlekiem i miodem, wtedy będziesz obchodził ten obrzęd w tym samym miesiącu.
6 Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu.
Przez siedem dni będziesz jeść przaśny chleb, a siódmego dnia [będzie] święto dla PANA.
7 Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako.
Będziesz jadł przaśny chleb przez siedem dni i nie może znaleźć się u ciebie nic kwaszonego ani żaden zakwas nie może być widziany we wszystkich twoich granicach.
8 Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’
W tym dniu opowiesz swemu synowi: [Obchodzę to] ze względu na to, co PAN dla mnie uczynił, gdy wychodziłem z Egiptu.
9 Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.
To będzie jako znak na twojej ręce i jako pamiątka przed twoimi oczyma, aby prawo PANA było na twoich ustach. PAN bowiem potężną ręką wyprowadził cię z Egiptu.
10 Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.
Będziesz przestrzegał tej ustawy w wyznaczonym czasie, z roku na rok.
11 “Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako,
A gdy PAN wprowadzi cię do ziemi Kanaan, jak przysiągł tobie i twoim ojcom, i da ją tobie;
12 inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana.
Wtedy przeznaczysz dla PANA wszystko, co otwiera łono, i każdy płód otwierający łono z twojego bydła, [każdy] samiec [będzie] dla PANA.
13 Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.
Każde zaś pierworodne oślę wykupisz barankiem, a jeśli nie wykupisz, złamiesz mu kark. Wykupisz też każdego pierworodnego człowieka wśród twoich synów.
14 “Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
A gdy w przyszłości twój syn cię zapyta: Cóż to jest? Wtedy odpowiesz mu: PAN wyprowadził nas potężną ręką z Egiptu, z domu niewoli.
15 Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’
Gdy bowiem faraon stał się twardy i wzbraniał się nas wypuścić, wtedy PAN zabił wszystko, co pierworodne w ziemi Egiptu, od pierworodnego z ludzi aż do pierworodnego z bydła. Dlatego składam w ofierze PANU wszystkie samce otwierające łono, ale każdego pierworodnego z moich synów wykupuję.
16 Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”
[To] będzie jako znak na twojej ręce i jako przepaska ozdobna między twoimi oczyma, że PAN potężną ręką wyprowadził nas z Egiptu.
17 Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.”
A stało się tak, że gdy faraon wypuścił lud, Bóg nie prowadził go drogą przez ziemię Filistynów, chociaż była bliższa. Bóg bowiem powiedział: Żeby lud na widok wojny nie żałował i nie wrócił do Egiptu.
18 Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.
Ale Bóg prowadził lud okrężną drogą przez pustynię nad Morzem Czerwonym. I synowie Izraela wyszli z ziemi Egiptu w bojowym szyku.
19 Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”
Mojżesz wziął też ze sobą kości Józefa, gdyż ten zobowiązał synów Izraela przysięgą, mówiąc: Na pewno Bóg was nawiedzi. Zabierzcie więc stąd ze sobą moje kości.
20 Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa.
Wyruszyli z Sukkot i rozbili obóz w Etam, na skraju pustyni.
21 Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku.
A PAN szedł przed nimi za dnia w słupie obłoku, by prowadzić ich drogą, a nocą w słupie ognia, by im świecić, żeby mogli iść dniem i nocą.
22 Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.
Nie oddalał od ludu ani słupa obłoku za dnia, ani słupa ognia nocą.

< Kutoka 13 >