< Kutoka 10 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake kuwa mgumu na mioyo ya maafisa wake ili kwamba nipate kutenda ishara hizi zangu za ajabu miongoni mwao
And the LORD said to Moses, Go in to Pharaoh: for I have hardened his heart, and the heart of his servants; that I might show these my signs before him:
2 ili upate kuwaeleza watoto wako na wajukuu wako jinsi nilivyowatendea Wamisri kwa ukali na jinsi nilivyofanya ishara zangu miongoni mwao, nanyi mpate kujua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
And that thou mayest tell in the ears of thy son, and of thy son's son, what things I have wrought in Egypt, and my signs which I have done among them; that ye may know how that I [am] the LORD.
3 Kwa hiyo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania, asemalo: ‘Utaendelea hata lini kukataa kunyenyekea mbele yangu? Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
And Moses and Aaron came in to Pharaoh, and said to him, Thus saith the LORD God of the Hebrews, How long wilt thou refuse to humble thyself before me? Let my people go, that they may serve me.
4 Kama ukikataa kuwaachia waende, kesho nitaleta nzige katika nchi yako.
Else, if thou shalt refuse to let my people go, behold, to-morrow will I bring the locusts into thy border:
5 Nao watafunika uso wa ardhi hata usionekane. Watatafuna mabaki machache yaliyobakizwa baada ya ile mvua ya mawe, yaani pamoja na kila mti unaoota katika mashamba yenu.
And they shall cover the face of the earth, that one cannot be able to see the earth: and they shall eat the residue of that which hath escaped, which remaineth to you from the hail, and shall eat every tree which groweth for you out of the field:
6 Nzige hao watajaza nyumba zako, za maafisa wako wote na za Wamisri wote. Jambo ambalo baba zenu wala babu zenu hawajapata kuona tangu siku ile walipoanza kuishi katika nchi hii mpaka leo hii.’” Ndipo Mose akageuka na kumwacha Farao.
And they shall fill thy houses, and the houses of all thy servants, and the houses of all the Egyptians; which neither thy fathers, nor thy fathers' fathers have seen, since the day that they were upon the earth to this day. And he turned himself, and went out from Pharaoh.
7 Maafisa wa Farao wakamwambia, “Mpaka lini huyu mtu atakuwa tanzi kwetu? Waachie hao watu waende zao, ili wapate kumwabudu Bwana Mungu wao. Je, bado hutambui kuwa Misri imeangamia?”
And Pharaoh's servants said to him, How long shall this man be a snare to us? Let the men go, that they may serve the LORD their God: knowest thou not yet that Egypt is destroyed?
8 Ndipo Mose na Aroni wakaletwa kwa Farao. Farao akawaambia, “Nendeni, mkamwabudu Bwana Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaokwenda?”
And Moses and Aaron were brought again to Pharaoh: and he said to them, Go, serve the LORD your God: [but] who [are] they that shall go?
9 Mose akajibu, “Tutakwenda na vijana wetu na wazee, pamoja na wana wetu na binti zetu, pia pamoja na kondoo zetu, ngʼombe, mbuzi, farasi na punda kwa sababu tutaadhimisha sikukuu kwa Bwana.”
And Moses said, We will go with our young and with our old, with our sons and with our daughters, with our flocks and with our herds will we go; for we [must hold] a feast to the LORD.
10 Farao akasema, “Bwana awe pamoja nanyi, kama nikiwaruhusu mwondoke pamoja na wanawake wenu na watoto wenu! Ni wazi kwamba mna makusudi mabaya.
And he said to them, Let the LORD be so with you, as I will let you go, and your little ones: look [to it]; for evil [is] before you.
11 La hasha! Wanaume peke yao na waende, wakamwabudu Bwana, kwa kuwa hilo ndilo mmekuwa mkiomba.” Kwa hiyo Mose na Aroni wakaondolewa mbele ya Farao.
Not so: go now ye [that are] men, and serve the LORD; for that you desired. And they were driven out from Pharaoh's presence.
12 Basi Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya Misri ili kundi la nzige liweze kuingia juu ya nchi na kutafuna kila kitu kiotacho katika mashamba na kila kitu kilichosazwa na ile mvua ya mawe.”
And the LORD said to Moses, Stretch out thy hand over the land of Egypt for the locusts, that they may come upon the land of Egypt, and eat every herb of the land, [even] all that the hail hath left.
13 Kwa hiyo Mose akanyoosha fimbo yake juu ya Misri, Bwana akauleta upepo wa mashariki ukavuma katika nchi yote mchana wote na usiku kucha, kufikia asubuhi upepo ukawa umeleta nzige.
And Moses stretched forth his rod over the land of Egypt, and the LORD brought an east wind upon the land all that day, and all [that] night: [and] when it was morning, the east wind brought the locusts.
14 Wakaivamia Misri yote na kukaa kila eneo la nchi kwa wingi. Kamwe hapajapata kuwepo pigo la nzige kama hilo, wala halitakuwepo tena.
And the locusts went up over all the land of Egypt, and rested in all the borders of Egypt: very grievous [were they]; before them there were no such locusts as they, neither after them will be such.
15 Wakafunika ardhi yote mpaka ardhi ikawa nyeusi. Wakatafuna kile chote kilichokuwa kimebakizwa na ile mvua ya mawe, kila kitu kiotacho mashambani pamoja na matunda kwenye miti. Hakuna kitu chochote cha kijani kilichosalia katika miti au mmea katika nchi yote ya Misri.
For they covered the face of the whole earth, so that the land was darkened; and they ate every herb of the land, and all the fruit of the trees which the hail had left: and there remained not any green thing on the trees, or in the herbs of the field, through all the land of Egypt.
16 Farao akawaita Mose na Aroni kwa haraka na kuwaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu na dhidi yenu pia.
Then Pharaoh called for Moses and Aaron in haste; and he said, I have sinned against the LORD your God, and against you.
17 Sasa unisamehe dhambi yangu mara moja tena na umwombe Bwana Mungu wako aondoe pigo hili baya kwangu.”
Now therefore forgive, I pray thee, my sin only this once, and entreat the LORD your God that he may take away from me this death only.
18 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akamwomba Bwana.
And he went out from Pharaoh, and entreated the LORD.
19 Naye Bwana akaugeuza upepo ukavuma kutoka magharibi, wenye nguvu nyingi, ambao uliwaondoa wale nzige na kuwapeleka kwenye Bahari ya Shamu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki popote katika nchi ya Misri.
And the LORD turned a mighty strong west wind which took away the locusts, and cast them into the Red sea: there remained not one locust in all the borders of Egypt.
20 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke.
But the LORD hardened Pharaoh's heart, so that he would not let the children of Israel go.
21 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.”
And the LORD said to Moses, Stretch out thy hand towards heaven, that there may be darkness over the land of Egypt, even darkness [which] may be felt.
22 Kwa hiyo Mose akaunyoosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu.
And Moses stretched forth his hand towards heaven: and there was a thick darkness in all the land of Egypt three days:
23 Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi.
They saw not one another, neither rose any from his place for three days: but all the children of Israel had light in their dwellings.
24 Ndipo Farao akamwita Mose na kusema, “Nendeni, mkamwabudu Bwana. Hata wanawake na watoto wenu mwaweza kwenda nao pia, lakini kondoo, mbuzi na ngʼombe wenu waacheni.”
And Pharaoh called to Moses, and said, Go ye, serve the LORD; only let your flocks and your herds be stayed: let your little ones also go with you.
25 Lakini Mose akasema, “Huna budi kuturuhusu tuwe na dhabihu na sadaka za kuteketezwa za kutoa mbele za Bwana Mungu wetu.
And Moses said, Thou must give us also sacrifices, and burnt-offerings, that we may sacrifice to the LORD our God.
26 Sisi ni lazima tuondoke na mifugo yetu pia, wala hakuna ukwato utakaoachwa nyuma. Inatupasa kutumia baadhi ya hiyo mifugo katika kumwabudu Bwana Mungu wetu, kwa kuwa mpaka tutakapofika huko hatutakuwa tumefahamu ni nini tutakachotumia katika kumwabudu Bwana.”
Our cattle also shall go with us; there shall not a hoof be left behind; for of them must we take to serve the LORD our God; and we know not with what we must serve the LORD, until we come thither.
27 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, hakuwa radhi kuwaachia waondoke.
But the LORD hardened Pharaoh's heart, and he would not let them go.
28 Farao akamwambia Mose, “Ondoka mbele yangu! Hakikisha kuwa hutakuja mbele yangu tena! Siku ile utakapouona uso wangu utakufa.”
And Pharaoh said to him, Depart from me, take heed to thyself, see my face no more: for in [that] day thou seest my face, thou shalt die.
29 Mose akamjibu, “Iwe kama ulivyosema! Kamwe sitauona uso wako tena.”
And Moses said, Thou hast spoken well, I will see thy face again no more.

< Kutoka 10 >