< Esta 7 >

1 Basi mfalme na Hamani wakaenda kula chakula pamoja na Malkia Esta.
So the king and Haman came to banquet with Esther the queen.
2 Walipokuwa wakinywa mvinyo katika siku ya pili, mfalme akauliza tena, “Malkia Esta, ni nini haja yako? Utapewa. Ombi lako ni nini? Hata nusu ya ufalme, utapewa.”
The king said again to Esther on the second day at the banquet of wine, "What is your petition, queen Esther? It shall be granted you. What is your request? Even to the half of the kingdom it shall be performed."
3 Kisha Malkia Esta akajibu, “Kama nimepata kibali kwako, ee mfalme, tena kama inapendeza utukufu wako, nijalie maisha yangu, hii ndiyo haja yangu. Pia uokoe watu wangu, hili ndilo ombi langu.
Then Esther the queen answered, "If I have found favor in your sight, O king, and if it please the king, let my life be given me at my petition, and my people at my request.
4 Kwa kuwa mimi na watu wangu tumeuzwa kwa kuangamizwa, kuchinjwa na kuharibiwa. Kama tungalikuwa tumeuzwa tu kuwa watumwa wa kiume na wa kike, ningalinyamaza kimya, kwa sababu shida kama hii isingalitosha kumsumbua mfalme.”
For we are sold, I and my people, to be destroyed, to be slain, and to perish. But if we had been sold for bondservants and bondmaids, I would have held my peace, although the adversary could not have compensated for the king's loss."
5 Mfalme Ahasuero akamuuliza Malkia Esta, “Ni nani huyu? Yuko wapi mtu huyu aliyethubutu kufanya jambo kama hili?”
Then King Achashyerosh said to Esther the queen, "Who is he, and where is he who dared presume in his heart to do so?"
6 Esta akasema, “Mtesi na adui ni huyu mwovu Hamani.” Hamani alifadhaika mbele ya mfalme na malkia.
Esther said, "An adversary and an enemy, even this wicked Haman." Then Haman was afraid before the king and the queen.
7 Mfalme akainuka kwa ghadhabu, akaacha mvinyo wake, akaenda kwenye bustani ya jumba la kifalme. Lakini Hamani, akitambua kwamba mfalme ameshaamua hatima yake, alibaki nyuma kumsihi Malkia Esta aokoe maisha yake.
The king arose in his wrath from the banquet of wine and went into the palace garden. Haman stood up to make request for his life to Esther the queen; for he saw that there was evil determined against him by the king.
8 Mara mfalme aliporudi kutoka bustani ya jumba la kifalme na kuja kwenye ukumbi wa karamu, Hamani alikuwa akijitupa juu ya kiti mahali ambapo Esta alikuwa akiegemea. Mfalme akasema kwa nguvu, “Je, atamdhalilisha malkia hata huku nyumbani akiwa pamoja nami!” Mara neno lilipotoka kinywani mwa mfalme, walifunika uso wa Hamani.
Then the king returned out of the palace garden into the place of the banquet of wine; and Haman had fallen on the couch where Esther was. Then the king said, "Will he even assault the queen in front of me in the house?" As the word went out of the king's mouth, they covered Haman's face.
9 Kisha Harbona, mmoja wa matowashi wanaomtumikia mfalme, akasema, “Mahali pa kuangika watu penye urefu wa mita ishirini na mbili pako nyumbani mwa Hamani. Alikuwa amepatengeneza kwa ajili ya Mordekai, ambaye alizungumza ili kumsaidia mfalme.” Mfalme akasema, “Mwangikeni juu yake!”
Then Harbonah, one of the eunuchs who were with the king said, "Look, the gallows seventy-three feet eight inches high, which Haman has made for Mordecai, who spoke good for the king, is standing at Haman's house." The king said, "Hang him on it."
10 Kwa hiyo wakamtundika Hamani mahali alipokuwa ameandaa kwa ajili ya Mordekai. Ndipo ghadhabu ya mfalme ikatulia.
So they hanged Haman on the gallows that he had prepared for Mordecai. Then was the king's wrath pacified.

< Esta 7 >