< Esta 6 >

1 Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe.
On that night, the king couldn't sleep. He commanded the book of records of the chronicles to be brought, and they were read to the king.
2 Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumuua Mfalme Ahasuero.
It was found written that Mordecai had told of Bigthana and Teresh, two of the king's eunuchs, who were doorkeepers, who had tried to lay hands on the King Achashyerosh.
3 Mfalme akauliza, “Je, ni heshima na shukrani gani Mordekai alipokea kwa ajili ya jambo hili?” Watumishi wake wakajibu, “Hakuna lolote alilofanyiwa.”
The king said, "What honor and dignity has been bestowed on Mordecai for this?" Then the king's servants who attended him said, "Nothing has been done for him."
4 Mfalme akasema, “Ni nani yuko uani?” Wakati huo huo Hamani alikuwa ameingia ua wa nje wa jumba la mfalme kusema na mfalme kuhusu kumwangika Mordekai katika mahali pa kuangikia watu alipokuwa amepajenga kwa ajili yake.
The king said, "Who is in the court?" Now Haman had come into the outer court of the king's house, to speak to the king about hanging Mordecai on the gallows that he had prepared for him.
5 Watumishi wake wakamjibu, “Hamani amesimama uani.” Mfalme akaamuru, “Mleteni ndani.”
The king's servants said to him, "Look, Haman stands in the court." The king said, "Let him come in."
6 Hamani alipoingia, mfalme alimuuliza, “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu?” Basi Hamani akawaza moyoni mwake, “Ni nani mwingine ambaye mfalme angemheshimu kuliko mimi?”
So Haman came in. The king said to him, "What shall be done to the man whom the king delights to honor?" Now Haman said in his heart, "Who would the king delight to honor more than myself?"
7 Kwa hiyo akamjibu mfalme, “Kwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu,
Haman said to the king, "For the man whom the king delights to honor,
8 aletewe joho la kifalme ambalo mfalme ameshalivaa na farasi ambaye mfalme alishampanda, ambaye amevikwa taji ya kifalme kichwani mwake.
let royal clothing be brought which the king uses to wear, and the horse that the king rides on, and on the head of which a crown royal is set.
9 Kisha joho na farasi vikabidhiwe kwa mmojawapo wa wakuu wa mfalme anayeheshimika sana. Nao wamvike mtu yule ambaye mfalme anapenda kumheshimu, na aongozwe akiwa juu ya farasi kupitia barabara za mji, wakitangaza mbele yake, ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu!’”
And let the clothing and the horse be delivered to the hand of one of the king's most noble officials, and let him clothe the man whom the king delights to honor with them, and have him ride on horseback through the city square, and proclaim before him, 'Thus shall it be done to the man whom the king delights to honor.'"
10 Mfalme akamwamuru Hamani, “Nenda mara moja, chukua joho na farasi na ufanye kama vile ulivyopendekeza kwa Mordekai Myahudi, akaaye langoni mwa mfalme. Usipuuze kufanya kitu chochote ulichoshauri.”
Then the king said to Haman, "Hurry and take the clothing and the horse, as you have said, and do this for Mordecai the Jew, who sits at the King's Gate. Let nothing fail of all that you have spoken."
11 Hivyo Hamani akachukua joho na farasi. Akamvika Mordekai, na kumpandisha juu ya farasi akamtembeza katika barabara za mji akitangaza mbele yake, “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme anapenda kumheshimu!”
Then Haman took the clothing and the horse, and arrayed Mordecai, and had him ride through the city square, and proclaimed before him, "Thus shall it be done to the man whom the king delights to honor."
12 Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme. Lakini Hamani akakimbia nyumbani, akiwa amejaa huzuni,
Mordecai came back to the King's Gate, but Haman hurried to his house, mourning and having his head covered.
13 naye akamweleza Zereshi mkewe pamoja na rafiki zake wote kila kitu ambacho kimempata. Washauri wake pamoja na Zereshi mkewe wakamwambia, “Kwa kuwa Mordekai, ambaye mbele yake umeanza kuanguka ni wa asili ya Kiyahudi, huwezi kushindana naye; kwa hakika utaanguka!”
Haman recounted to Zeresh his wife and all his friends everything that had happened to him. Then his wise men and Zeresh his wife said to him, "If Mordecai, before whom you have begun to fall, is of Jewish descent, you will not prevail against him, but you will surely fall before him."
14 Walipokuwa bado wakizungumza naye, matowashi wa mfalme wakaja na kumharakisha Hamani aende katika karamu aliyoiandaa Esta.
While they were yet talking with him, the king's eunuchs came, and hurried to bring Haman to the banquet that Esther had prepared.

< Esta 6 >