< Mhubiri 7 >

1 Afadhali sifa nzuri kuliko manukato safi, nayo siku ya kufa kuliko ya kuzaliwa.
Une bonne réputation vaut mieux que le bon parfum; et le jour de la mort, que le jour de la naissance.
2 Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu, kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu, imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao.
Mieux vaut aller dans une maison de deuil, que d'aller dans une maison de festin; car là est la fin de tout homme, et celui qui vit met cela dans son cœur.
3 Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo.
Mieux vaut la tristesse que le rire; car, par la tristesse du visage, le cœur devient joyeux.
4 Moyo wa wenye hekima uko katika nyumba ya msiba, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya anasa.
Le cœur des sages est dans la maison de deuil; mais le cœur des insensés est dans la maison de joie.
5 Afadhali kusikia karipio la mtu mwenye hekima, kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
Mieux vaux entendre la répréhension du sage, que d'entendre la chanson des insensés.
6 Kama ilivyo kuvunjika kwa miiba chini ya sufuria, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Hili nalo pia ni ubatili.
Car tel qu'est le bruit des épines sous la chaudière, tel est le rire de l'insensé. Cela aussi est une vanité.
7 Dhuluma humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, nayo rushwa huuharibu moyo.
Certainement l'oppression peut faire perdre le sens au sage; et le présent corrompt le cœur.
8 Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake, uvumilivu ni bora kuliko kiburi.
Mieux vaut la fin d'une chose que son commencement; mieux vaut un esprit patient qu'un esprit hautain.
9 Usiwe mwepesi kukasirika rohoni mwako, kwa kuwa hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
Ne te hâte point dans ton esprit de t'irriter; car l'irritation repose dans le sein des insensés.
10 Usiseme, “Kwa nini siku za kale zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa maana si hekima kuuliza maswali kama hayo.
Ne dis point: D'où vient que les jours passés étaient meilleurs que ceux-ci? Car ce n'est point par sagesse que tu t'enquiers de cela.
11 Hekima, kama ulivyo urithi, ni kitu chema na huwafaidia wale walionalo jua.
La sagesse est aussi bonne qu'un héritage; elle est un avantage pour ceux qui voient le soleil.
12 Hekima ni ulinzi kama fedha ilivyo ulinzi, lakini faida ya maarifa ni hii: kwamba hekima huhifadhi maisha ya aliye nayo.
Car on est à couvert à l'ombre de la sagesse et à l'ombre de l'argent; mais la science a cet avantage, que la sagesse fait vivre celui qui la possède.
13 Tafakari kile Mungu alichokitenda: Nani awezaye kunyoosha kile ambacho yeye amekipinda?
Regarde l'œuvre de Dieu; car qui peut redresser ce qu'il aura courbé?
14 Nyakati zikiwa nzuri, ufurahi, lakini nyakati zikiwa mbaya, tafakari: Mungu amefanya hiyo moja, naam, sanjari na hiyo nyingine. Kwa hiyo, mwanadamu hawezi kugundua kitu chochote kuhusu maisha yake ya baadaye.
Au jour de la prospérité, sois joyeux; et au jour de l'adversité, prends-y garde; aussi Dieu a fait l'un comme l'autre, afin que l'homme ne trouve rien de ce qui sera après lui.
15 Katika maisha haya yangu ya ubatili nimeshaona haya mawili: mtu mwadilifu akiangamia katika uadilifu wake, naye mtu mwovu akiishi maisha marefu katika uovu wake.
J'ai vu tout ceci pendant les jours de ma vanité. Il y a tel juste qui périt dans sa justice, et il y a tel méchant qui prolonge ses jours dans sa méchanceté.
16 Usiwe mwenye haki kupita kiasi, wala usiwe na hekima kupita kiasi: kwa nini kujiangamiza mwenyewe?
Ne sois pas juste à l'excès, et ne te fais pas trop sage; pourquoi te perdrais-tu?
17 Usiwe mwovu kupita kiasi, wala usiwe mpumbavu: kwa nini kufa kabla ya wakati wako?
Ne sois pas méchant à l'excès, et ne sois point insensé; pourquoi mourrais-tu avant ton temps?
18 Ni vyema kushika hilo moja na wala usiache hilo jingine likupite. Mtu amchaye Mungu ataepuka huko kupita kiasi.
Il est bon que tu retiennes ceci, et que tu ne négliges pas cela; car celui qui craint Dieu, sort de toutes ces choses.
19 Hekima humfanya yeye aliye nayo kuwa na uwezo zaidi kuliko watawala kumi katika mji.
La sagesse donne plus de force au sage que dix gouverneurs qui seraient dans une ville.
20 Hakuna mtu mwenye haki duniani ambaye hufanya mambo ya haki na kamwe asitende dhambi.
Certainement il n'y a point d'homme juste sur la terre, qui fasse le bien et qui ne pèche point.
21 Usitie maanani kila neno linalosemwa na watu, la sivyo, waweza kumsikia mtumishi wako akikulaani:
Aussi ne fais point attention à toutes les paroles qu'on dira, de peur que tu n'entendes ton serviteur parler mal de toi.
22 kwa kuwa unafahamu moyoni mwako kwamba wewe mwenyewe mara nyingi umewalaani wengine.
Car ton cœur a reconnu bien des fois que toi aussi tu as mal parlé des autres.
23 Yote haya niliyajaribu kwa hekima, nikasema, “Nimeamua kuwa na hekima”: lakini hii ilikuwa nje ya uwezo wangu.
J'ai éprouvé tout cela par la sagesse; et j'ai dit: J'acquerrai de la sagesse; mais elle s'est éloignée de moi.
24 Vyovyote hekima ilivyo, hekima iko mbali sana na imejificha, ni nani awezaye kuigundua?
Ce qui est loin, ce qui est profond, profond, qui peut l'atteindre?
25 Nikageuza fikira zangu ili kuelewa, kuchunguza na kuitafuta hekima na kusudi la mambo, na ili kuelewa ujinga wa uovu, na wazimu wa upumbavu.
J'ai appliqué mon cœur à connaître, à sonder et à chercher la sagesse et la raison de tout, et à connaître la méchanceté de la folie, et la sottise de la déraison.
26 Nimeona jambo lililo chungu kuliko mauti, mwanamke ambaye ni mtego, ambaye moyo wake ni wavu wa kutegea na mikono yake ni minyororo. Mtu ampendezaye Mungu atamkwepa, bali mwenye dhambi atanaswa naye.
Et j'ai trouvé plus amère que la mort, la femme dont le cœur est un piège et un filet, et dont les mains sont des liens; celui qui est agréable à Dieu lui échappera; mais le pécheur sera pris par elle.
27 Mhubiri anasema, “Tazama, hili ndilo nililogundua: “Nimegundua kitu kimoja baada ya kingine nilipokuwa katika kusudi la mambo:
Voici, dit l'Ecclésiaste, ce que j'ai trouvé, en examinant les choses une à une pour en trouver la raison.
28 ningali natafiti lakini sipati: nilimpata mwanaume mmoja mnyofu miongoni mwa elfu, lakini hakuna mwanamke mmoja mnyofu miongoni mwao.
Voici ce que mon âme cherche encore, mais que je n'ai point trouvé. J'ai trouvé un homme entre mille; mais je n'ai pas trouvé une femme entre elles toutes.
29 Hili ndilo peke yake nililolipata: Mungu amemuumba mwanadamu mnyofu, lakini mwanadamu amebuni mambo mengi.”
Seulement voici ce que j'ai trouvé: c'est que Dieu a fait l'homme droit; mais ils ont cherché beaucoup de discours.

< Mhubiri 7 >