< Mhubiri 11 >

1 Tupa mkate wako juu ya maji, kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.
Send out your bread on the waters, for you will find it again after many days.
2 Wape sehemu watu saba, naam hata wanane, kwa maana hujui ni baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
Share it with seven, even eight people, for you do not know what disasters are coming on the earth.
3 Kama mawingu yamejaa maji, hunyesha mvua juu ya nchi. Kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, mahali ulipoangukia, hapo ndipo utakapolala.
If the clouds are full of rain, they empty themselves on the earth, and if a tree falls toward the south or toward the north, wherever the tree falls, there it will remain.
4 Yeyote atazamaye upepo hatapanda, yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.
Anyone who watches the wind might not plant, and anyone who watches the clouds might not harvest.
5 Kama vile usivyofahamu njia ya upepo, au jinsi mwili uumbwavyo ndani ya tumbo la mama, vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu, Muumba wa vitu vyote.
As you do not know the path of the wind, nor how a baby's bones grow in the pregnant womb, so also you cannot comprehend the work of God, who created everything.
6 Panda mbegu yako asubuhi, nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee, kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa, kwamba ni hii au ni ile, au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.
In the morning plant your seed; until the evening, work with your hands as needed, for you know not which will prosper, whether morning or evening, or this or that, or whether they will both alike be good.
7 Nuru ni tamu, tena inafurahisha macho kuona jua.
Truly the light is sweet, and it is a pleasant thing for the eyes to see the sun.
8 Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani, na aifurahie yote. Lakini na akumbuke siku za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.
If someone lives many years, let him be happy in all of them, but let him think about the coming days of darkness, for they will be many. Everything to come is vanishing vapor.
9 Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana, moyo wako na ukupe furaha katika siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na chochote macho yako yaonayo, lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote Mungu atakuleta hukumuni.
Take joy, young man, in your youth, and let your heart be joyful in the days of your youth. Pursue the good desires of your heart, and whatever is within the sight of your eyes. However, know that God will bring you into judgment for all these things.
10 Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako, kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.
Drive anger away from your heart, and ignore any pain in your body, because youth and its strength are vapor.

< Mhubiri 11 >