< Mhubiri 10 >

1 Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
Mrtve muhe lekarnarjevemu mazilu povzročijo, da od sebe širi smrdljiv vonj; tako je majhna neumnost tistemu, ki ima sloves zaradi modrosti in časti.
2 Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
Srce modrega človeka je pri njegovi desnici, toda bedakovo srce pri njegovi levici.
3 Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
Da, tudi kadar kdor je bedak, hodi po poti, ga njegova modrost izneverja in vsakemu govori, da je bedak.
4 Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
Če vladarjev duh vstane zoper tebe, ne zapusti svojega mesta, kajti ustrežljivost pomirja velike prestopke.
5 Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
Je zlo, ki sem ga videl pod soncem, kakor pomota, ki izvira od vladarja:
6 Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
neumnost je postavljena na visoko dostojanstvo, bogati pa sedijo na nizkem kraju.
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
Videl sem služabnike na konjih, prince pa hoditi kakor služabniki po tleh.
8 Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
Kdor koplje jamo, bo padel vanjo, kdorkoli pa lomi ograjo, ga bo pičila kača.
9 Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
Kdorkoli odstranja kamne, bo z njimi poškodovan in kdor cepi drva, bo s tem izpostavljen nevarnosti.
10 Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
Če je železo topo in ne nabrusi ostrine, potem mora vložiti več moči; toda modrost je koristna, da usmerja.
11 Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
Zagotovo bo kača pičila brez izrekanja uroka in blebetavec ni boljši.
12 Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
Besede iz ust modrega moža so milostljive, toda ustnice bedaka bodo samega sebe pogoltnile.
13 Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
Začetek besed iz njegovih ust je nespametnost, konec njegovega govora pa je pogubna norost.
14 naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
Tudi bedak je poln besed. Človek ne more povedati kaj bo, in kaj bo za njim, kdo mu lahko pove?
15 Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
Trud nespametnih izčrpava vsakogar izmed njih, ker ne ve kako iti do mesta.
16 Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
Gorje tebi, oh dežela, kadar je tvoj kralj otrok in tvoji princi jedo zjutraj!
17 Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
Blagoslovljena si ti, oh dežela, kadar je tvoj kralj sin plemičev in tvoji princi jedo v pravšnjem obdobju, za moč in ne za pijanost!
18 Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
Z veliko lenobe zgradba propada in zaradi brezdelja rok kaplja skozi hišo.
19 Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
Praznovanje je narejeno za smeh in vino dela vesele, toda denar odgovarja vsem stvarem.
20 Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.
Ne preklinjaj kralja niti v svojih mislih in ne preklinjaj bogatega v svoji spalnici, kajti zračna ptica bo odnesla glas in kar ima peruti, bo povedalo zadevo.

< Mhubiri 10 >