< Mhubiri 10 >

1 Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
Dead flies cause the ointment of the apothecary to send forth a stinking smell: so does a little folly him that is in reputation for wisdom and honor.
2 Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
A wise man’s heart is at his right hand; but a fool’s heart at his left.
3 Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
Yes also, when he that is a fool walks by the way, his wisdom fails him, and he says to every one that he is a fool.
4 Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
If the spirit of the ruler rise up against you, leave not your place; for yielding pacifies great offenses.
5 Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
There is an evil which I have seen under the sun, as an error which proceeds from the ruler:
6 Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
Folly is set in great dignity, and the rich sit in low place.
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
I have seen servants on horses, and princes walking as servants on the earth.
8 Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
He that digs a pit shall fall into it; and whoever breaks an hedge, a serpent shall bite him.
9 Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
Whoever removes stones shall be hurt therewith; and he that splits wood shall be endangered thereby.
10 Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
If the iron be blunt, and he do not whet the edge, then must he put to more strength: but wisdom is profitable to direct.
11 Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
Surely the serpent will bite without enchantment; and a babbler is no better.
12 Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
The words of a wise man’s mouth are gracious; but the lips of a fool will swallow up himself.
13 Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
The beginning of the words of his mouth is foolishness: and the end of his talk is mischievous madness.
14 naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
A fool also is full of words: a man cannot tell what shall be; and what shall be after him, who can tell him?
15 Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
The labor of the foolish wearies every one of them, because he knows not how to go to the city.
16 Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
Woe to you, O land, when your king is a child, and your princes eat in the morning!
17 Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
Blessed are you, O land, when your king is the son of nobles, and your princes eat in due season, for strength, and not for drunkenness!
18 Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
By much slothfulness the building decays; and through idleness of the hands the house drops through.
19 Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
A feast is made for laughter, and wine makes merry: but money answers all things.
20 Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.
Curse not the king, no not in your thought; and curse not the rich in your bedchamber: for a bird of the air shall carry the voice, and that which has wings shall tell the matter.

< Mhubiri 10 >