< Torati 32 >

1 Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitasema; sikia, ee nchi, maneno ya kinywa changu.
Slušaj, nebo, govoriæu; i zemlja neka èuje govor usta mojih.
2 Mafundisho yangu na yanyeshe kama mvua, na maneno yangu na yashuke kama umande, kama manyunyu juu ya majani mabichi, kama mvua tele juu ya mimea myororo.
Neka se spusti kao dažd nauka moja, i neka padne kao rosa govor moj, kao sitan dažd na mladu travu i kao krupan dažd na odraslu travu.
3 Nitalitangaza jina la Bwana. Naam, sifuni ukuu wa Mungu wetu!
Jer æu javljati ime Gospodnje; velièajte Boga našega.
4 Yeye ni Mwamba, kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni haki. Mungu mwaminifu ambaye hakosei, yeye ni mnyofu na mwenye haki.
Djelo je te stijene savršeno, jer su svi putovi njegovi pravda; Bog je vjeran, bez nepravde; pravedan je i istinit.
5 Wamefanya mambo ya upotovu mbele zake; kwa aibu yao, wao si watoto wake tena, lakini ni kizazi kilicho kiovu na kilichopotoka.
Oni se pokvariše prema njemu; njihovo nevaljalstvo nije nevaljalstvo sinova njegovijeh; to je rod zao i pokvaren.
6 Je, hii ndiyo njia ya kumlipa Bwana, enyi watu wajinga na wasio na busara? Je, yeye siye Baba yenu, Muumba wenu, aliyewafanya ninyi na kuwaumba?
Tako li vraæate Gospodu, narode ludi i bezumni? nije li on otac tvoj, koji te je zadobio? on te je naèinio i stvorio.
7 Kumbuka siku za kale; tafakari vizazi vya zamani vilivyopita. Uliza baba yako, naye atakuambia, wazee wako, nao watakueleza.
Opomeni se negdašnjih dana, pogledajte godine svakoga vijeka; pitaj oca svojega i on æe ti javiti, starije svoje i kazaæe ti.
8 Aliye Juu Sana alipowapa mataifa urithi wao, alipogawanya wanadamu wote, aliweka mipaka kwa ajili ya mataifa sawasawa na hesabu ya wana wa Israeli.
Kad višnji razdade našljedstvo narodima, kad razdijeli sinove Adamove, postavi meðe narodima po broju sinova Izrailjevih.
9 Kwa kuwa fungu la Bwana ni watu wake, Yakobo kura yake ya urithi.
Jer je dio Gospodnji narod njegov, Jakov je uže našljedstva njegova.
10 Katika nchi ya jangwa alimkuta, katika nyika tupu ivumayo upepo. Alimhifadhi na kumtunza; akamlinda kama mboni ya jicho lake,
Naðe ga u zemlji pustoj, na mjestu strašnu gdje buèi pustoš; vodi ga unaokolo, uèi ga i èuva kao zjenicu oka svojega.
11 kama tai avurugaye kiota chake, na kurukaruka juu ya makinda yake, ambaye hutanda mabawa yake kuwadaka, na huwachukua kwenye mabawa yake.
Kao što orao izmamljuje orliæe svoje, diže se nad ptiæima svojim, širi krila svoja, uzima ih i nosi na krilima svojim,
12 Bwana peke yake alimwongoza; hakuwepo mungu mgeni pamoja naye.
Tako ga Gospod voðaše, i s njim ne bješe tuðega boga;
13 Akamfanya apande sehemu zilizoinuka za nchi, akamlisha kwa mavuno ya mashamba. Akamlea kwa asali toka mwambani, na kwa mafuta kutoka mwamba mgumu,
Voðaše ga na visine zemaljske da jede rod poljski, i davaše mu da sisa med iz stijene i ulje iz tvrdoga kamena,
14 kwa jibini na maziwa kutoka makundi ya ngʼombe na kutoka makundi ya mbuzi, kwa mafuta ya wana-kondoo na mbuzi, kwa kondoo dume wazuri wa Bashani, na kwa ngano nzuri. Ukanywa damu ya zabibu inayotoa povu.
Maslo od krava i mlijeko od ovaca s pretilinom od jaganjaca i ovnova Vasanskih i jaraca, sa srcem zrna pšeniènih; i pio si vino, krv od grožða.
15 Yeshuruni alinenepa na kupiga teke; alikuwa na chakula tele, akawa mzito na akapendeza sana. Akamwacha Mungu aliyemuumba, na kumkataa Mwamba Mwokozi wake.
Ali se Izrailj ugoji, pa se stade ritati; utio si, udebljao i zasalio; pa ostavi Boga koji ga je stvorio, i prezre stijenu spasenja svojega.
16 Wakamfanya Mungu kuwa na wivu kwa miungu yao migeni, na kumkasirisha kwa sanamu zao za machukizo.
Na revnost razdražiše ga tuðim bogovima, gadovima razgnjeviše ga.
17 Wakatoa dhabihu kwa pepo, ambao si Mungu: miungu wasiyoijua, miungu iliyojitokeza siku za karibuni, miungu ambayo baba zenu hawakuiogopa.
Prinosiše žrtve ðavolima, ne Bogu, bogovima, kojih nijesu znali, novim, koji iz bliza doðoše, kojih se nijesu strašili oci vaši.
18 Mkamwacha Mwamba, aliyewazaa ninyi; mkamsahau Mungu aliyewazaa.
Stijenu koja te je rodila zaboravio si; zaboravio si Boga stvoritelja svojega.
19 Bwana akaona hili, akawakataa, kwa sababu alikasirishwa na wanawe na binti zake.
Kad to vidje Gospod, razgnjevi se na sinove svoje i na kæeri svoje,
20 Akasema, “Nitawaficha uso wangu, nami nione mwisho wao utakuwa nini, kwa kuwa wao ni kizazi kilichopotoka, watoto ambao si waaminifu.
I reèe: sakriæu od njih lice svoje, vidjeæu kakav æe im biti pošljedak, jer su rod pokvaren, sinovi u kojima nema vjere.
21 Wamenifanya niwe na wivu kwa kile ambacho si mungu, na kunikasirisha kwa sanamu zao zisizokuwa na thamani. Nitawafanya wawaonee wivu wale ambao si taifa. Nitawafanya wakasirishwe na taifa lile lisilo na ufahamu.
Oni me razdražiše na revnost onijem što nije Bog, razgnjeviše svojim taštinama; i ja æu njih razdražiti na revnost onijem koji nije narod, narodom ludijem razljutiæu ih.
22 Kwa maana moto umewashwa kwa hasira yangu, ule uwakao hadi kwenye vina vya mauti. Utateketeza dunia pamoja na mazao yake, na kuwasha moto katika misingi ya milima. (Sheol h7585)
Jer se oganj razgorio u gnjevu mojem, i gorjeæe do najdubljega pakla; spaliæe zemlju i rod njezin, i popaliæe temelje brdima. (Sheol h7585)
23 “Nitalundika majanga juu yao na kutumia mishale yangu dhidi yao.
Zgrnuæu na njih zla, strijele svoje pobacaæu na njih.
24 Nitatuma njaa kali dhidi yao maradhi mabaya, yateketezayo na tauni ya kufisha; nitawapelekea meno makali ya wanyama mwitu, na sumu ya nyoka wale watambaao mavumbini.
Glad æe ih cijediti, vruæice i ljuti pomori proždiraæe ih; i zube zvjerske poslaæu na njih i jed zmija zemaljskih.
25 Barabarani upanga utawakosesha watoto; nyumbani mwao hofu itatawala. Vijana wao wa kiume na wa kike wataangamia, pia watoto wachanga na wazee wenye mvi.
Spolja æe ih ubijati maè, a po klijetima strah, i momka i djevojku, dijete na sisi i sijeda èovjeka.
26 Nilisema ningewatawanya na kufuta kumbukumbu lao katika mwanadamu.
Rekao bih: rasijaæu ih po svijem uglovima zemaljskim, uèiniæu da nestane spomena njihova izmeðu ljudi,
27 Lakini nilihofia dhihaka za adui, adui asije akashindwa kuelewa, na kusema, ‘Mikono yetu imeshinda; Bwana hakufanya yote haya.’”
Da mi nije do mržnje neprijateljeve, da se ne bi neprijatelji njihovi ponijeli i rekli: ruka se naša uzvisila, a nije Gospod uèinio sve ovo.
28 Wao ni taifa lisilo na akili, hakuna busara ndani yao.
Jer su narod koji propada sa svojih namjera, i nema u njih razuma.
29 Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili, na kutambua mwisho wao utakuwa aje!
Kamo da su pametni, da razumiju ovo, i gledaju na pošljedak svoj!
30 Mtu mmoja angewezaje kufukuza elfu moja, au wawili kufukuza elfu kumi, kama si kwamba Mwamba wao amewauza, kama si kwamba Bwana amewaacha?
Kako bi jedan gonio tisuæu a dvojica tjerala deset tisuæa, da ih nije stijena njihova prodala i Gospod ih predao?
31 Kwa kuwa mwamba wao si kama Mwamba wetu, sawasawa na vile adui zetu wanavyokiri.
Jer stijena njihova nije kao naša stijena; neprijatelji naši neka budu sudije.
32 Mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma, na kutoka kwenye mashamba ya Gomora. Zabibu zake zimejaa sumu, na vishada vyake vimejaa uchungu.
Jer je èokot njihov od èokota Sodomskoga i iz polja Gomorskoga; grožðe je njihovo grožðe otrovno, puca su mu gorka.
33 Mvinyo wao ni sumu ya nyoka, sumu yenye kufisha ya swila.
Vino je njihovo otrov zmajevski, i ljuti jed aspidin.
34 “Je, hili sikuliweka akiba na kulifungia kwenye vyumba vyangu vya hazina?
Nije li to sakriveno kod mene, zapeèaæeno u riznicama mojim?
35 Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza. Wakati utakapowadia, mguu wao utateleza; siku yao ya maafa ni karibu, na maangamizo yao yanawajia haraka.”
Moja je osveta i plata, u svoje vrijeme popuznuæe noga njihova, jer je blizu dan propasti njihove, i ide brzo što æe ih zadesiti.
36 Bwana atawahukumu watu wake, na kuwahurumia watumishi wake atakapoona nguvu zao zimekwisha wala hakuna yeyote aliyebaki, mtumwa au aliye huru.
Sudiæe Gospod narodu svojemu, i žao æe mu biti sluga njegovijeh, kad vidi da je prošla snaga i da nema ništa ni od uhvaæenoga ni od ostavljenoga.
37 Atasema: “Sasa iko wapi miungu yao, mwamba walioukimbilia,
I reæi æe: gdje su bogovi njihovi? stijena u koju se uzdaše?
38 miungu wale waliokula mafuta ya dhabihu zao na kunywa mvinyo wa sadaka zao za vinywaji? Wainuke basi, wawasaidie! Wawapeni basi ulinzi!
Koji salo od žrtava njegovijeh jedoše i piše vino od naljeva njihovijeh. Neka ustanu i pomogu vam, i neka vam budu zaklon.
39 “Tazama basi, Mimi mwenyewe, Mimi Ndiye! Hakuna mungu mwingine ila Mimi. Mimi ninaua na Mimi ninafufua, Mimi nimejeruhi na Mimi nitaponya, wala hakuna awezaye kuokoa kutoka mkononi mwangu.
Vidite sada da sam ja, ja sam, i da nema Boga osim mene. Ja ubijam i oživljujem, ranim i iscjeljujem, i nema nikoga ko bi izbavio iz moje ruke.
40 Ninainua mkono wangu kuelekea mbinguni na kusema: Hakika kama niishivyo milele,
Jer podižem k nebu ruku svoju i kažem: ja sam živ dovijeka.
41 wakati ninapounoa upanga wangu unaometameta na mkono wangu unapoushika ili kutoa hukumu, nitalipiza kisasi juu ya adui zangu na kuwalipiza wale wanaonichukia.
Ako naoštrim sjajni maè svoj i uzmem u ruku sud, uèiniæu osvetu na neprijateljima svojim i vratiæu onima koji mrze na me.
42 Nitailevya mishale yangu kwa damu, wakati upanga wangu ukitafuna nyama: damu ya waliochinjwa pamoja na mateka, vichwa vya viongozi wa adui.”
Opojiæu strijele svoje krvlju, i maè æe se moj najesti mesa, krvlju isjeèenijeh i zarobljenijeh, kad poènem osvetu na neprijateljima.
43 Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake, kwa kuwa atailipiza damu ya watumishi wake, atalipiza kisasi juu ya adui zake na kufanya upatanisho kwa ajili ya nchi na watu wake.
Veselite se narodi s narodom njegovijem, jer æe pokajati krv sluga svojih, i osvetiæe se neprijateljima svojim, i oèistiæe zemlju svoju i narod svoj.
44 Mose na Yoshua mwana wa Nuni wakaja, wakanena maneno yote ya wimbo watu wakiwa wanasikia.
I doðe Mojsije i izgovori sve rijeèi pjesme ove narodu, on i Isus sin Navin.
45 Mose alipomaliza kuyasoma maneno haya yote kwa Israeli wote,
A kad izgovori Mojsije sve rijeèi ove svemu Izrailju,
46 akawaambia, “Yawekeni moyoni maneno yote ambayo nimewatangazia kwa makini siku hii ya leo, ili kwamba mpate kuwaagiza watoto wenu wayatii kwa bidii maneno yote ya sheria hii.
Reèe im: privijte srce svoje k svijem rijeèima koje vam ja danas zasvjedoèavam, i kazujte ih sinovima svojim da bi držali sve rijeèi ovoga zakona i tvorili ih.
47 Siyo maneno matupu tu kwenu, bali ni uzima wenu. Kwa hayo mtaishi maisha marefu katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”
Jer nije prazna rijeè da za nju ne marite, nego je život vaš; i tom æete rijeèju produljiti dane svoje na zemlji, u koju idete preko Jordana da je naslijedite.
48 Siku hiyo hiyo Bwana akamwambia Mose,
U isti dan reèe Gospod Mojsiju govoreæi:
49 “Kwea katika mapangano ya Mlima Abarimu hadi kilima cha Nebo kilichoko Moabu, ngʼambo ya Yeriko, na uitazame Kanaani, nchi ninayowapa Waisraeli kama milki yao wenyewe.
Izidi na ovu goru Avarimsku, na goru Navav, koja je u zemlji Moavskoj prema Jerihonu, i vidi zemlju Hanansku koju dajem sinovima Izrailjevijem u državu.
50 Utafia kwenye mlima huo unaokwea na kukusanyika pamoja na watu wako, kama ndugu yako Aroni alivyofia juu ya Mlima Hori naye akakusanyika kwa watu wake.
I umri na gori na koju izideš, i priberi s k rodu svojemu, kao što je umro Aron brat tvoj na gori Oru i pribrao se k rodu svojemu.
51 Hii ni kwa sababu ninyi wawili mlivunja uaminifu nami mbele ya Waisraeli kwenye maji ya Meriba-Kadeshi katika Jangwa la Sini, na kwa sababu hamkuuinua utakatifu wangu miongoni mwa Waisraeli.
Jer mi zgriješiste meðu sinovima Izrailjevijem na vodi od svaðe u Kadisu, u pustinji Sinu, što me ne proslaviste meðu sinovima Izrailjevijem.
52 Kwa hiyo, utaiona tu nchi kwa mbali; wewe hutaingia nchi ninayowapa watu wa Israeli.”
Pred sobom æeš vidjeti zemlju, ali neæeš u nju uæi, u zemlju koju dajem sinovima Izrailjevijem.

< Torati 32 >