< Torati 32 >

1 Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitasema; sikia, ee nchi, maneno ya kinywa changu.
Give ear, you heavens, and let me speak. Let the earth listen to the words of my mouth.
2 Mafundisho yangu na yanyeshe kama mvua, na maneno yangu na yashuke kama umande, kama manyunyu juu ya majani mabichi, kama mvua tele juu ya mimea myororo.
Let my teaching drop down like the rain, let my speech distill like the dew, like the gentle rain on the tender grass, and like the showers on the plants.
3 Nitalitangaza jina la Bwana. Naam, sifuni ukuu wa Mungu wetu!
For I will proclaim the name of Yahweh, and ascribe greatness to our God.
4 Yeye ni Mwamba, kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni haki. Mungu mwaminifu ambaye hakosei, yeye ni mnyofu na mwenye haki.
The Rock, his work is perfect; for all his paths are just. He is the faithful God, without iniquity. He is just and upright.
5 Wamefanya mambo ya upotovu mbele zake; kwa aibu yao, wao si watoto wake tena, lakini ni kizazi kilicho kiovu na kilichopotoka.
They have acted corruptly against him. They are not his children. It is their disgrace. They are a perverted and crooked generation.
6 Je, hii ndiyo njia ya kumlipa Bwana, enyi watu wajinga na wasio na busara? Je, yeye siye Baba yenu, Muumba wenu, aliyewafanya ninyi na kuwaumba?
Do you reward Yahweh in this way, you foolish and senseless people? Is he not your father, the one who has created you? He made you and established you.
7 Kumbuka siku za kale; tafakari vizazi vya zamani vilivyopita. Uliza baba yako, naye atakuambia, wazee wako, nao watakueleza.
Call to mind the days of ancient times, think about the years of many ages past. Ask your father and he will show you, your elders and they will tell you.
8 Aliye Juu Sana alipowapa mataifa urithi wao, alipogawanya wanadamu wote, aliweka mipaka kwa ajili ya mataifa sawasawa na hesabu ya wana wa Israeli.
When the Most High gave the nations their inheritance— when he divided all of mankind, and he set the boundaries of the peoples, as he also fixed the number of their gods.
9 Kwa kuwa fungu la Bwana ni watu wake, Yakobo kura yake ya urithi.
For Yahweh's portion is his people; Jacob is his apportioned inheritance.
10 Katika nchi ya jangwa alimkuta, katika nyika tupu ivumayo upepo. Alimhifadhi na kumtunza; akamlinda kama mboni ya jicho lake,
He found him in a desert land, and in the barren and howling wilderness; he shielded him and cared for him, he guarded him as the apple of his eye.
11 kama tai avurugaye kiota chake, na kurukaruka juu ya makinda yake, ambaye hutanda mabawa yake kuwadaka, na huwachukua kwenye mabawa yake.
As an eagle that guards her nest and flutters over her young, Yahweh spread out his wings and took them, and carried them on his pinions.
12 Bwana peke yake alimwongoza; hakuwepo mungu mgeni pamoja naye.
Yahweh alone led him; no foreign god was with him.
13 Akamfanya apande sehemu zilizoinuka za nchi, akamlisha kwa mavuno ya mashamba. Akamlea kwa asali toka mwambani, na kwa mafuta kutoka mwamba mgumu,
He made him ride on high places of the land, and he fed him the fruits of the field; he nourished him with honey from the rock, and oil from the flinty crag.
14 kwa jibini na maziwa kutoka makundi ya ngʼombe na kutoka makundi ya mbuzi, kwa mafuta ya wana-kondoo na mbuzi, kwa kondoo dume wazuri wa Bashani, na kwa ngano nzuri. Ukanywa damu ya zabibu inayotoa povu.
He ate butter from the herd and drank milk from the flock, with fat of lambs, rams of Bashan and goats, with the finest of the wheat— and you drank foaming wine made from the juice of grapes.
15 Yeshuruni alinenepa na kupiga teke; alikuwa na chakula tele, akawa mzito na akapendeza sana. Akamwacha Mungu aliyemuumba, na kumkataa Mwamba Mwokozi wake.
But Jeshurun grew fat and kicked— you grew fat, you were too fat, and you had eaten your fill— he abandoned the God who made him, and he rejected the Rock of his salvation.
16 Wakamfanya Mungu kuwa na wivu kwa miungu yao migeni, na kumkasirisha kwa sanamu zao za machukizo.
They made Yahweh jealous by their strange gods; with their abominations they angered him.
17 Wakatoa dhabihu kwa pepo, ambao si Mungu: miungu wasiyoijua, miungu iliyojitokeza siku za karibuni, miungu ambayo baba zenu hawakuiogopa.
They sacrificed to demons, which are not God— gods they had not known, gods that recently appeared, gods your fathers did not fear.
18 Mkamwacha Mwamba, aliyewazaa ninyi; mkamsahau Mungu aliyewazaa.
You have deserted the Rock, who became your father, and you forgot the God who gave you birth.
19 Bwana akaona hili, akawakataa, kwa sababu alikasirishwa na wanawe na binti zake.
Yahweh saw this and he rejected them, because his sons and his daughters provoked him so.
20 Akasema, “Nitawaficha uso wangu, nami nione mwisho wao utakuwa nini, kwa kuwa wao ni kizazi kilichopotoka, watoto ambao si waaminifu.
“I will hide my face from them,” he said, “and I will see what their end will be; for they are a perverse generation, children who are unfaithful.
21 Wamenifanya niwe na wivu kwa kile ambacho si mungu, na kunikasirisha kwa sanamu zao zisizokuwa na thamani. Nitawafanya wawaonee wivu wale ambao si taifa. Nitawafanya wakasirishwe na taifa lile lisilo na ufahamu.
They have made me jealous by what is not god and angered me by their worthless things. I will make them envious by those who are not a people; by a foolish nation I will make them angry.
22 Kwa maana moto umewashwa kwa hasira yangu, ule uwakao hadi kwenye vina vya mauti. Utateketeza dunia pamoja na mazao yake, na kuwasha moto katika misingi ya milima. (Sheol h7585)
For a fire is kindled by my anger and is burning to the lowest Sheol; it is devouring the earth and its harvest; it is setting on fire the foundations of the mountains. (Sheol h7585)
23 “Nitalundika majanga juu yao na kutumia mishale yangu dhidi yao.
I will heap disasters on them; I will shoot all my arrows at them;
24 Nitatuma njaa kali dhidi yao maradhi mabaya, yateketezayo na tauni ya kufisha; nitawapelekea meno makali ya wanyama mwitu, na sumu ya nyoka wale watambaao mavumbini.
They will be wasted by hunger and devoured by burning heat and bitter destruction; I will send on them the teeth of wild animals, with the poison of things that crawl in the dust.
25 Barabarani upanga utawakosesha watoto; nyumbani mwao hofu itatawala. Vijana wao wa kiume na wa kike wataangamia, pia watoto wachanga na wazee wenye mvi.
Outside the sword will bereave, and in the bedrooms terror will do so. It will destroy both young man and virgin, the nursing baby, and the man of gray hairs.
26 Nilisema ningewatawanya na kufuta kumbukumbu lao katika mwanadamu.
I said that I would scatter them far away, that I would make the memory of them to cease from among mankind.
27 Lakini nilihofia dhihaka za adui, adui asije akashindwa kuelewa, na kusema, ‘Mikono yetu imeshinda; Bwana hakufanya yote haya.’”
Were it not that I feared the provocation of the enemy, and that their enemies would judge mistakenly, and that they would say, 'Our hand is exalted,' I would have done all this.
28 Wao ni taifa lisilo na akili, hakuna busara ndani yao.
For Israel is a nation devoid of wisdom, and there is no understanding in them.
29 Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili, na kutambua mwisho wao utakuwa aje!
Oh, that they were wise, that they understood this, that they would consider their coming fate!
30 Mtu mmoja angewezaje kufukuza elfu moja, au wawili kufukuza elfu kumi, kama si kwamba Mwamba wao amewauza, kama si kwamba Bwana amewaacha?
How could one chase a thousand, and two put ten thousand to flight, unless their Rock had sold them, and Yahweh had given them up?
31 Kwa kuwa mwamba wao si kama Mwamba wetu, sawasawa na vile adui zetu wanavyokiri.
For our enemies' rock is not like our Rock, just as even our enemies admit.
32 Mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma, na kutoka kwenye mashamba ya Gomora. Zabibu zake zimejaa sumu, na vishada vyake vimejaa uchungu.
For their vine comes from the vine of Sodom, and from the fields of Gomorrah; their grapes are grapes of poison; their clusters are bitter.
33 Mvinyo wao ni sumu ya nyoka, sumu yenye kufisha ya swila.
Their wine is the poison of serpents and the cruel venom of asps.
34 “Je, hili sikuliweka akiba na kulifungia kwenye vyumba vyangu vya hazina?
Is not this plan secretly kept by me, sealed up among my treasures?
35 Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza. Wakati utakapowadia, mguu wao utateleza; siku yao ya maafa ni karibu, na maangamizo yao yanawajia haraka.”
Vengeance is mine to give, and recompense, at the time when their foot slips; for the day of disaster for them is near, and the things that are to come on them will hurry to happen.”
36 Bwana atawahukumu watu wake, na kuwahurumia watumishi wake atakapoona nguvu zao zimekwisha wala hakuna yeyote aliyebaki, mtumwa au aliye huru.
For Yahweh will give justice to his people, and he will pity his servants. He will see that their power is gone, and no one remains, either slaves or free people.
37 Atasema: “Sasa iko wapi miungu yao, mwamba walioukimbilia,
Then he will say, “Where are their gods, the rock in whom they took refuge?—
38 miungu wale waliokula mafuta ya dhabihu zao na kunywa mvinyo wa sadaka zao za vinywaji? Wainuke basi, wawasaidie! Wawapeni basi ulinzi!
The gods who ate the fat of their sacrifices and drank the wine of their drink offerings? Let them rise up and help you; let them be your protection.
39 “Tazama basi, Mimi mwenyewe, Mimi Ndiye! Hakuna mungu mwingine ila Mimi. Mimi ninaua na Mimi ninafufua, Mimi nimejeruhi na Mimi nitaponya, wala hakuna awezaye kuokoa kutoka mkononi mwangu.
See now that I, even I, am God, and that there is no god besides me; I kill, and I make alive; I wound, and I heal, and there is no one who can save you from my might.
40 Ninainua mkono wangu kuelekea mbinguni na kusema: Hakika kama niishivyo milele,
For I lift up my hand to heaven and say, 'As I live forever, I will act.
41 wakati ninapounoa upanga wangu unaometameta na mkono wangu unapoushika ili kutoa hukumu, nitalipiza kisasi juu ya adui zangu na kuwalipiza wale wanaonichukia.
When I sharpen my glittering sword, and when my hand begins to bring justice, I will render vengeance on my enemies, and I will pay back those who hate me.
42 Nitailevya mishale yangu kwa damu, wakati upanga wangu ukitafuna nyama: damu ya waliochinjwa pamoja na mateka, vichwa vya viongozi wa adui.”
I will make my arrows drunk with blood, and my sword will devour flesh with the blood of the killed and the captives, and from the heads of the leaders of the enemy.'”
43 Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake, kwa kuwa atailipiza damu ya watumishi wake, atalipiza kisasi juu ya adui zake na kufanya upatanisho kwa ajili ya nchi na watu wake.
Rejoice, you nations, with God's people, for he will avenge the blood of his servants; he will render vengeance on his enemies, and he will make atonement for his land, for his people.
44 Mose na Yoshua mwana wa Nuni wakaja, wakanena maneno yote ya wimbo watu wakiwa wanasikia.
Moses came and recited all the words of this song in the ears of the people, he, and Joshua son of Nun.
45 Mose alipomaliza kuyasoma maneno haya yote kwa Israeli wote,
Then Moses finished reciting all these words to all Israel.
46 akawaambia, “Yawekeni moyoni maneno yote ambayo nimewatangazia kwa makini siku hii ya leo, ili kwamba mpate kuwaagiza watoto wenu wayatii kwa bidii maneno yote ya sheria hii.
He said to them, “Fix your mind on all the words that I have witnessed to you today, so that you may command your children to keep them, all the words of this law.
47 Siyo maneno matupu tu kwenu, bali ni uzima wenu. Kwa hayo mtaishi maisha marefu katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”
For this is no trivial matter for you, because it is your life, and through this thing you will prolong your days in the land that you are going over the Jordan to possess.”
48 Siku hiyo hiyo Bwana akamwambia Mose,
Yahweh spoke to Moses on that same day and said,
49 “Kwea katika mapangano ya Mlima Abarimu hadi kilima cha Nebo kilichoko Moabu, ngʼambo ya Yeriko, na uitazame Kanaani, nchi ninayowapa Waisraeli kama milki yao wenyewe.
“Go up into this range of the mountains of Abarim, up Mount Nebo, which is in the land of Moab, opposite Jericho. You will look at the land of Canaan, which I am giving to the people of Israel as their possession.
50 Utafia kwenye mlima huo unaokwea na kukusanyika pamoja na watu wako, kama ndugu yako Aroni alivyofia juu ya Mlima Hori naye akakusanyika kwa watu wake.
You will die on the mountain that you go up, and you will be gathered to your people, as Aaron your fellow Israelite died on Mount Hor and was gathered to his people.
51 Hii ni kwa sababu ninyi wawili mlivunja uaminifu nami mbele ya Waisraeli kwenye maji ya Meriba-Kadeshi katika Jangwa la Sini, na kwa sababu hamkuuinua utakatifu wangu miongoni mwa Waisraeli.
This will happen because you were unfaithful to me among the people of Israel at the waters of Meribah in Kadesh, in the wilderness of Zin; because you did not treat me with honor and respect among the people of Israel.
52 Kwa hiyo, utaiona tu nchi kwa mbali; wewe hutaingia nchi ninayowapa watu wa Israeli.”
For you will see the land before you, but you will not go there, into the land that I am giving to the people of Israel.”

< Torati 32 >