< Torati 30 >

1 Wakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popote Bwana Mungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa,
Or, quand toutes ces choses, que je t'ai représentées, seront venues sur toi, soit la bénédiction, soit la malédiction, et que tu les rappelleras à ton cœur, parmi toutes les nations où l'Éternel ton Dieu t'aura chassé;
2 hapo wewe na watoto wako mtakapomrudia Bwana Mungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo,
Et que tu te convertiras à l'Éternel ton Dieu, et que tu obéiras à sa voix, de tout ton cœur et de toute ton âme, toi et tes enfants, selon tout ce que je te commande aujourd'hui;
3 ndipo Bwana Mungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya.
Alors l'Éternel ton Dieu ramènera tes captifs et aura compassion de toi, et il te rassemblera de nouveau d'entre tous les peuples parmi lesquels l'Éternel ton Dieu t'aura dispersé.
4 Hata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka huko Bwana Mungu wako atakukusanya na kukurudisha.
Quand tes dispersés seraient au bout des cieux, de là l'Éternel ton Dieu te rassemblera, et de là il te retirera.
5 Yeye Bwana atakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako.
Et l'Éternel ton Dieu te ramènera au pays que possédèrent tes pères, et tu le posséderas; il te fera du bien, et te multipliera plus que tes pères.
6 Bwana Mungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi.
Et l'Éternel ton Dieu circoncira ton cœur, et le cœur de ta postérité, pour que tu aimes l'Éternel ton Dieu de tout ton cœur et de toute ton âme, afin que tu vives.
7 Bwana Mungu wako ataweka laana hizi zote juu ya adui zako ambao wanakuchukia na kukutesa.
Et l'Éternel ton Dieu mettra toutes ces imprécations sur tes ennemis, et sur ceux qui te haïssent et qui t'auront persécuté.
8 Utamtii tena Bwana na kuzishika amri zake zote ninazokupa leo.
Mais toi, tu te convertiras, et tu obéiras à la voix de l'Éternel, et tu pratiqueras tous ses commandements que je te prescris aujourd'hui.
9 Ndipo Bwana Mungu wako atakapokufanikisha sana katika kazi zote za mikono yako na katika uzao wa tumbo lako, wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako. Bwana atakufurahia tena na kukufanikisha, kama alivyowafurahia baba zako,
Et l'Éternel ton Dieu te fera abonder en biens dans toutes les œuvres de ta main, dans le fruit de tes entrailles, dans le fruit de ton bétail et dans le fruit de ton sol; car l'Éternel prendra de nouveau plaisir à te faire du bien, comme il y a pris plaisir pour tes pères,
10 kama ukimtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake ambayo yameandikwa katika Kitabu hiki cha Sheria, na kumgeukia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
Quand tu obéiras à la voix de l'Éternel ton Dieu, pour garder ses commandements et ses statuts écrits dans ce livre de la loi; quand tu te convertiras à l'Éternel ton Dieu de tout ton cœur et de toute ton âme.
11 Ninachokuagiza leo sio kigumu sana kwako au usichokiweza.
Car ce commandement que je te prescris aujourd'hui n'est point trop élevé au-dessus de toi, et n'est pas éloigné.
12 Hakiko juu mbinguni, ili uulize, “Ni nani atakayepanda mbinguni kukileta na kututangazia ili tuweze kutii?”
Il n'est pas dans les cieux, pour qu'on dise: Qui montera pour nous aux cieux, et nous l'apportera, et nous le fera entendre, pour que nous le pratiquions?
13 Wala hakiko ngʼambo ya bahari, ili uulize, “Ni nani atakayevuka bahari kwenda kukichukua na kututangazia ili tupate kutii?”
Il n'est point non plus au delà de la mer, pour qu'on dise: Qui passera pour nous au delà de la mer, et nous l'apportera, et nous le fera entendre, pour que nous le pratiquions?
14 La hasha! Lile neno liko karibu sana nawe; liko kinywani mwako na ndani ya moyo wako ili uweze kulitii.
Car cette parole est fort près de toi, dans ta bouche et dans ton cœur, afin que tu l'accomplisses.
15 Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo.
Regarde, j'ai mis aujourd'hui devant toi la vie et le bien, la mort et le mal.
16 Ninakuamuru leo kwamba umpende Bwana Mungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, naye Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.
Car je te commande aujourd'hui d'aimer l'Éternel ton Dieu, de marcher dans ses voies, et d'observer ses commandements, ses statuts et ses ordonnances, afin que tu vives, et que tu multiplies, et que l'Éternel ton Dieu te bénisse, au pays où tu vas pour le posséder.
17 Lakini kama moyo wako ukigeukia mbali ukawa huna utii, kama umevutwa kuisujudia miungu mingine na kuiabudu,
Mais si ton cœur se détourne, et que tu n'obéisses pas, et que tu te laisses aller à te prosterner devant d'autres dieux et à les servir,
18 nakutangazia leo hii kwamba hakika utaangamizwa. Hutaishi maisha marefu katika nchi unayovuka Yordani kuiingia na kuimiliki.
Je vous déclare aujourd'hui que vous périrez certainement; vous ne prolongerez point vos jours sur la terre où tu vas entrer en passant le Jourdain, pour la posséder.
19 Leo ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yako kwamba nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana. Basi sasa chagueni uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi,
Je prends aujourd'hui les cieux et la terre à témoin contre vous, que j'ai mis devant toi la vie et la mort, la bénédiction et la malédiction. Choisis donc la vie, afin que tu vives, toi et ta postérité,
20 na ili upate kumpenda Bwana Mungu wako, uisikilize sauti yake na kuambatana naye. Kwa kuwa Bwana ndiye uzima wako, na atakupa wingi wa siku ili upate kuishi katika nchi aliyoapa kuwapa baba zako Abrahamu, Isaki na Yakobo.
En aimant l'Éternel ton Dieu, en obéissant à sa voix, et en demeurant attaché à lui; car c'est lui qui est ta vie et la longueur de tes jours; en sorte que tu habites sur le sol que l'Éternel a juré de donner à tes pères, Abraham, Isaac et Jacob.

< Torati 30 >