< Torati 27 >

1 Mose na wazee wa Israeli wakawaagiza watu: “Yashikeni maagizo haya yote ninayowaagiza leo.
And Moses with the elders of Israel commanded the people, saying, Keep all the commandments which I command you this day.
2 Mtakapokuwa mmevuka Mto Yordani na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, msimamishe mawe makubwa na mkayatie lipu.
And it shall be on the day when ye shall pass over Jordan to the land which the LORD thy God giveth thee, that thou shalt set thee up great stones, and plaster them with plaster:
3 Andikeni juu yake maneno yote ya sheria hii wakati mtakapokuwa mmevuka na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, nchi itiririkayo maziwa na asali, kama vile Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi.
And thou shalt write upon them all the words of this law, when thou hast passed over, that thou mayest enter in to the land which the LORD thy God giveth thee, a land that floweth with milk and honey; as the LORD God of thy fathers hath promised thee.
4 Mtakapokuwa mmevuka Yordani, simamisheni mawe haya juu ya Mlima Ebali, kama ninavyowaagiza leo, mkayatie lipu.
Therefore it shall be when ye have gone over Jordan, that ye shall set up these stones, which I command you this day, in mount Ebal, and thou shalt plaster them with plaster.
5 Huko mjengeeni Bwana Mungu wenu madhabahu, madhabahu ya mawe. Msitumie kifaa chochote cha chuma juu yake.
And there shalt thou build an altar to the LORD thy God, an altar of stones: thou shalt not lift up any iron tool upon them.
6 Jengeni madhabahu ya Bwana Mungu wenu kwa mawe ya shambani, na mtoe sadaka za kuteketezwa juu yake kwa Bwana Mungu wenu.
Thou shalt build the altar of the LORD thy God of whole stones: and thou shalt offer on it burnt offerings to the LORD thy God:
7 Toeni sadaka za amani juu yake, mkizila na kufurahia mbele za Bwana Mungu wenu.
And thou shalt offer peace offerings, and shalt eat there, and rejoice before the LORD thy God.
8 Nanyi mtaandika maneno yote ya sheria hii kwa wazi sana juu ya mawe haya ambayo mmesimamisha.”
And thou shalt write upon the stones all the words of this law very plainly.
9 Kisha Mose na makuhani, ambao ni Walawi, wakawaambia Israeli wote, “Nyamaza ee Israeli, sikiliza! Sasa umekuwa taifa la Bwana Mungu wako.
And Moses and the priests the Levites spoke to all Israel, saying, Take heed, and hearken, O Israel; this day thou art become the people of the LORD thy God.
10 Mtii Bwana Mungu wako, na kufuata amri zake na maagizo ninayokupa leo.”
Thou shalt therefore obey the voice of the LORD thy God, and do his commandments and his statutes, which I command thee this day.
11 Siku ile ile Mose akawaagiza watu:
And Moses charged the people the same day, saying,
12 Mtakapovuka Mto Yordani, makabila haya yatasimama juu ya Mlima Gerizimu kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benyamini.
These shall stand upon mount Gerizim to bless the people, when ye have come over Jordan; Simeon, and Levi, and Judah, and Issachar, and Joseph, and Benjamin:
13 Makabila haya yatasimama juu ya Mlima Ebali kwa kutamka laana: Reubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani na Naftali.
And these shall stand upon mount Ebal to curse; Reuben, Gad, and Asher, and Zebulun, Dan, and Naphtali.
14 Nao Walawi watawasomea watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
And the Levites shall speak, and say to all the men of Israel with a loud voice,
15 “Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”
Cursed be the man that maketh any graven or molten image, an abomination to the LORD, the work of the hands of the craftsman, and putteth it in a secret place. And all the people shall answer and say, Amen.
16 “Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”
Cursed be he that dishonoureth his father or his mother. And all the people shall say, Amen.
17 “Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”
Cursed be he that removeth his neighbour’s landmark. And all the people shall say, Amen.
18 “Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”
Cursed be he that maketh the blind to wander out of the way. And all the people shall say, Amen.
19 “Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”
Cursed be he that perverteth the judgment of the stranger, fatherless, and widow. And all the people shall say, Amen.
20 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”
Cursed be he that lieth with his father’s wife; because he uncovereth his father’s skirt. And all the people shall say, Amen.
21 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”
Cursed be he that lieth with any manner of beast. And all the people shall say, Amen.
22 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”
Cursed be he that lieth with his sister, the daughter of his father, or the daughter of his mother. And all the people shall say, Amen.
23 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”
Cursed be he that lieth with his mother in law. And all the people shall say, Amen.
24 “Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”
Cursed be he that smiteth his neighbour secretly. And all the people shall say, Amen.
25 “Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”
Cursed be he that taketh reward to slay an innocent person. And all the people shall say, Amen.
26 “Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”
Cursed be he that confirmeth not all the words of this law to do them. And all the people shall say, Amen.

< Torati 27 >