< Torati 25 >

1 Watu wanapokuwa na ugomvi, wapeleke mahakamani na waamuzi wataamua shauri hilo; watawaachia wasio na kosa na kuwahukumu wenye hatia.
If cause is bitwixe ony men, and thei axen iugis, thei schulen yyue the victorie of riytfulnesse to him, whom thei perseyuen to be iust, thei schulen condempne hym of wickidnesse, whom thei perseyuen to be wickid.
2 Kama mtu mwenye hatia anastahili kuchapwa, mwamuzi atamwamuru alale chini ili achapwe mbele yake idadi ya viboko kulingana na kosa lake,
Sotheli if thei seen hym that synnede, worthi of betyngis, thei schulen caste him doun, and make to be betun bifor hem; also the maner of betyngis schal be for the mesure of synne,
3 lakini kamwe asichapwe zaidi ya viboko arobaini. Ikiwa atachapwa zaidi ya viboko arobaini, nduguyo atadhalilika machoni pako.
so oneli that tho passe not the noumbre of fourti, lest thi brother be to-rent viliche bifore thin iyen, and go awei.
4 Usimfunge maksai kinywa anapopura nafaka.
Thou schalt not bynde the `mouth of the oxe tredynge thi fruytis in the corn floor.
5 Ikiwa ndugu wanaishi pamoja na mmoja wao akafa bila kuacha mwana, kamwe mjane wake asiolewe nje ya jamaa hiyo. Ndugu wa mumewe atamchukua, amwoe na kutimiza wajibu wa shemeji kwake.
Whanne britheren dwellen to gidere, and oon of hem is deed with out fre children, the wijf of the deed brother schal not be weddid to anothir man, but his brothir schal take hir, and schal reise seed of his brother.
6 Mwana wa kwanza atakayemzaa atapewa jina la ndugu aliyekufa ili jina lake lisifutike katika Israeli.
And he schal clepe the firste gendrid sone `of hir bi the name `of hym, `that is, of the deed brothir, that his name be not don awei fro Israel.
7 Hata hivyo, ikiwa ndugu huyo wa mume hataki kuoa huyo mke wa nduguye, mjane atawaendea wazee kwenye lango la mji na kusema, “Ndugu wa mume wangu anakataa kuendeleza jina la nduguye katika Israeli. Hataki kutimiza wajibu wa shemeji kwangu.”
Forsothe if he nyle take the wijf of his brother, which is due to hym bi lawe, the womman schal go to the yate of the citee; and sche schal axe the grettere men in birthe, and sche schal seie, `The brother of myn hosebonde nyle reise seed of his brother in Israel, nethir wole take me in to mariage.
8 Ndipo wazee wa mji wake watamwita na kuzungumza naye. Kama atashikilia kukataa akisema, “Sitaki kumwoa,”
And anoon thei schulen make hym to be clepid, and thei schulen axe. If he answerith, Y nyle take hir to wijf;
9 mjane wa nduguye atamwendea mbele ya wazee, atamvua kiatu kimoja na kumtemea mate usoni, na kusema, “Hivi ndivyo ambavyo hufanywa kwa mtu ambaye atakataa kuendeleza jamaa ya ndugu yake.”
the womman schal go to hym bifor the eldre men of Israel, and sche schal take awei the schoo, and sche schal spete in to his face, and schal seie, So it schal be doon to the man, that bildith not `the hows of his brother;
10 Jamaa ya mtu huyo itafahamika katika Israeli kama Jamaa ya Aliyevuliwa Kiatu.
and `the name of hym schal be clepid in Israel, The hows of the man vnschood.
11 Ikiwa watu wawili wanapigana na mke wa mmoja wao akaja kumwokoa mumewe na yule anayemshambulia, naye mke huyo akifika na kumkamata sehemu za siri,
If twei men han strijf bitwixe hem silf, and oon bigynneth to stryue ayens another, and the wijf of `the tother man wole delyuere hir hosebonde fro the hond of the strongere man, and puttith hond, and `takith the schamefast membris `of hym,
12 huyo mwanamke utamkata mkono wake. Usimhurumie.
thou schalt kitte awei `the hond of hir, nether thou schalt be bowid on hir bi ony mercy.
13 Usiwe na mawe ya kupimia ya aina mbili katika mkoba wako, moja zito na jingine jepesi.
Thou schalt not haue in the bagge dyuerse weiytis,
14 Usiwe na vipimo viwili tofauti katika nyumba yako, kimoja kikubwa, kingine kidogo.
a grettere and a lesse, nether a buyschel more and lesse schal be in thin hows.
15 Ni lazima uwe na uzito na vipimo sahihi na vya haki, ili upate kuishi maisha marefu katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.
Thou schalt haue a iust weiyte and trewe, and an euene buyschel `and trewe schal be to thee, that thou lyue in myche tyme on the lond which thi Lord God schal yyue to thee.
16 Kwa maana Bwana Mungu wako humchukia yeyote ambaye hufanya mambo kama haya, yeyote anayetenda kwa udanganyifu.
For the Lord schal haue hym abhomynable that doith these thingis, and he wlatith, `ethir cursith, al vnriytfulnesse.
17 Kumbuka kile Waamaleki walichowatendea mlipokuwa njiani mkitoka Misri.
Haue thou mynde what thingis Amalech dide to thee in the weie, whanne thou yedist out of Egipt;
18 Wakati mlipokuwa mmechoka na kuishiwa nguvu kwa safari yenu, wakawapiga wale wote waliokuja nyuma. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.
hou he cam to thee, and killide the laste men of thin oost, that saten wery, whanne thou were disesid with hungur and trauel, and he dredde not God.
19 Bwana Mungu wako atakapokupa pumziko mbali na adui zako wote wanaokuzunguka katika nchi akupayo kuimiliki kuwa urithi, utafutilia mbali kumbukumbu lote la Waamaleki chini ya mbingu. Usisahau!
Therfor whanne thi Lord God hath youe reste to thee, and hath maad suget alle naciouns `bi cumpas, in the lond which he bihiyte to thee, thou schalt do awei `the name of hym vndur heuene; be thou war lest thou foryete.

< Torati 25 >