< Torati 24 >

1 Ikiwa mtu atamwoa mke na akamchukia kwa sababu ya kukosa adabu, naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake,
Quand un homme aura pris une femme et l'aura épousée, si elle ne trouve pas grâce à ses yeux, parce qu'il aura trouvé en elle quelque chose de honteux, il lui écrira une lettre de divorce, la lui mettra dans la main, et la renverra de sa maison.
2 ikiwa baada ya kuondoka nyumbani kwake atakuwa mke wa mtu mwingine,
Et si, étant sortie de sa maison, elle s'en va et devient la femme d'un autre homme,
3 ikiwa mume wake wa pili atachukizwa naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake, au kama akifa,
Si ce dernier mari la hait, lui écrit une lettre de divorce, la lui met dans la main, et la renvoie de sa maison; ou si ce dernier mari, qui l'avait prise pour femme, meurt,
4 basi yule mume wake wa kwanza, ambaye alimpa talaka, haruhusiwi kumwoa tena baada ya mwanamke huyo kuwa najisi. Hayo yatakuwa machukizo machoni pa Bwana. Usilete dhambi juu ya nchi ambayo Bwana Mungu wako anakupa kama urithi.
Son premier mari, qui l'avait renvoyée, ne pourra pas la reprendre pour femme après qu'elle a été souillée; car ce serait une abomination devant l'Éternel, et tu ne chargeras point de péché le pays que l'Éternel ton Dieu te donne en héritage.
5 Kama mtu ameoa karibuni, kamwe asipelekwe vitani au kupewa wajibu mwingine wowote. Kwa mwaka mmoja atakuwa huru kubaki nyumbani ili amfurahishe mke aliyemwoa.
Quand un homme aura nouvellement pris femme, il n'ira point à la guerre, et on ne lui imposera aucune charge; pendant un an il en sera exempt pour sa famille, et il réjouira la femme qu'il aura prise.
6 Usitoe jozi ya mawe ya kusagia, hata ikiwa lile la juu, kuweka rehani kwa ajili ya deni, kwa sababu itakuwa ni kuweka uhai wa mtu kama dhamana.
On ne prendra point pour gage les deux meules, ni la meule de dessus; car ce serait prendre pour gage la vie de son prochain.
7 Kama mtu akikamatwa akiiba yeyote miongoni mwa ndugu zake wa Waisraeli na kumtenda kama mtumwa au akimuuza, mwizi huyo ni lazima auawe. Nawe utaondoa uovu kutoka miongoni mwenu.
Quand on trouvera un homme qui aura dérobé quelqu'un de ses frères, des enfants d'Israël, et l'aura fait esclave ou vendu, ce larron mourra; et tu ôteras le méchant du milieu de toi.
8 Pakitokea magonjwa ya ngozi ya kuambukiza, mwe waangalifu sana kufanya sawasawa na maagizo ya makuhani, ambao ni Walawi. Ni lazima mfuate kwa uangalifu yale niliyowaamuru.
Prends garde à la plaie de la lèpre, pour bien observer et pour faire tout ce que les sacrificateurs, de la race de Lévi, vous enseigneront; vous prendrez garde à faire comme je leur ai commandé.
9 Kumbukeni kile Bwana Mungu wenu alichomfanyia Miriamu njiani baada ya ninyi kutoka Misri.
Souviens-toi de ce que l'Éternel ton Dieu fit à Marie dans le chemin, quand vous sortiez d'Égypte.
10 Unapomkopesha jirani yako chochote, usiingie nyumbani kwake kutwaa kile anachokitoa kama rehani.
Quand tu prêteras quelque chose à ton prochain, tu n'entreras point dans sa maison pour prendre son gage;
11 Ukae nje na umwache huyo mtu uliyemkopesha akuletee hiyo rehani.
Tu te tiendras dehors, et l'homme à qui tu prêtes t'apportera le gage dehors.
12 Ikiwa mtu huyo ni maskini, usiende kulala ukiwa na hiyo rehani yake katika milki yako.
Et si c'est un homme pauvre, tu ne te coucheras point ayant encore son gage.
13 Rudisha vazi lake kabla ya machweo ya jua ili apate kulilalia. Kisha atakushukuru na kitaonekana kama kitendo cha haki mbele za Bwana Mungu wako.
Tu ne manqueras pas de lui rendre le gage, au coucher du soleil, afin qu'il couche dans son vêtement, et qu'il te bénisse; et cela te sera imputé à justice devant l'Éternel ton Dieu.
14 Usimwonee mtu maskini na mhitaji ambaye umemwajiri, akiwa ni nduguyo Mwisraeli au mgeni anayeishi katika mojawapo ya miji yenu.
Tu ne feras point tort au mercenaire pauvre et indigent, d'entre tes frères ou d'entre les étrangers qui demeurent dans ton pays, dans tes portes.
15 Mlipe ujira wake kila siku kabla ya jua kutua, kwa sababu yeye ni maskini na anautegemea ujira huo. La sivyo, anaweza kumlilia Bwana dhidi yako, nawe ukapata hatia ya dhambi.
Tu lui donneras son salaire, le jour même, avant que le soleil se couche; car il est pauvre, et son âme s'y attend; de peur qu'il ne crie contre toi à l'Éternel, et qu'il n'y ait du péché en toi.
16 Baba wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya baba zao; kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe.
On ne fera point mourir les pères pour les enfants; on ne fera point non plus mourir les enfants pour les pères; on fera mourir chacun pour son péché.
17 Usipotoshe hukumu ya mgeni au yatima, au kuchukua vazi la mjane kama rehani.
Tu ne pervertiras point le droit d'un étranger, ni d'un orphelin, et tu ne prendras point pour gage le vêtement d'une veuve.
18 Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa huko Misri, naye Bwana Mungu wenu akawakomboa kutoka huko. Hii ndiyo sababu ninawaamuru kutenda hili.
Et tu te souviendras que tu as été esclave en Égypte, et que l'Éternel ton Dieu t'a racheté de là. C'est pourquoi, je te commande de faire ces choses.
19 Unapovuna shamba lako na ukasahau mganda, usirudi kuuchukua. Acha kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane, ili Bwana Mungu wako aweze kukubariki wewe katika kazi zote za mikono yako.
Quand tu feras ta moisson dans ton champ, et que tu y auras oublié une poignée d'épis, tu ne retourneras point pour la prendre; elle sera pour l'étranger, pour l'orphelin et pour la veuve, afin que l'Éternel ton Dieu te bénisse dans toutes les œuvres de tes mains.
20 Unapovuna zeituni kutoka miti yako, usirudie matawi mara ya pili. Acha kilichobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.
Quand tu secoueras tes oliviers, tu n'y retourneras point pour examiner branche après branche; ce qui restera sera pour l'étranger, pour l'orphelin et pour la veuve.
21 Unapochuma zabibu katika shamba lako la mizabibu usirudie tena. Acha zinazobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.
Quand tu vendangeras ta vigne, tu n'y feras pas grappiller après toi; ce qui restera sera pour l'étranger, pour l'orphelin et pour la veuve.
22 Kumbuka kwamba mlikuwa watumwa katika nchi ya Misri. Ndiyo sababu ninawaamuru kufanya hili.
Et tu te souviendras que tu as été esclave au pays d'Égypte; c'est pourquoi, je te commande de faire cela.

< Torati 24 >