< Torati 23 >

1 Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.
No man injured by crushing or cutting off may enter the assembly of Yahweh.
2 Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
No illegitimate child may belong to the assembly of Yahweh; as far as to the tenth generation of his descendants, none of them may belong to the assembly of Yahweh.
3 Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
An Ammonite or a Moabite may not belong to the assembly of Yahweh; as far as to the tenth generation of his descendants, none of them may belong to the assembly of Yahweh.
4 Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi.
This is because they did not meet you with bread and with water on the road when you had come out of Egypt, and because they hired against you Balaam son of Beor from Pethor in Aram Naharaim, to curse you.
5 Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda.
But Yahweh your God would not listen to Balaam; instead, Yahweh your God turned the curse into a blessing for you, because Yahweh your God loved you.
6 Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.
You must never seek their peace or prosperity, during all your days.
7 Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.
You must not detest an Edomite, for he is your brother; you must not abhor an Egyptian, because you were a foreigner in his land.
8 Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.
The descendants of the third generation that are born to them may belong to the assembly of Yahweh.
9 Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.
When you march out as an army against your enemies, then you must keep yourselves from every evil thing.
10 Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.
If there is among you any man who is unclean because of what happened to him at night, then he must go out of the army's camp; he must not come back into the camp.
11 Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.
When evening comes, he must bathe himself in water; when the sun goes down, he will come back inside the camp.
12 Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.
You must have a place also outside the camp to which you will go;
13 Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.
and you will have something among your tools to dig with; when you squat down to relieve yourself, you must dig with it and then put back the earth and cover up what has come out from you.
14 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.
For Yahweh your God walks in the midst of your camp to give you victory and to give your enemies into your hand. Therefore your camp must be holy, so that he may not see any unclean thing among you and turn away from you.
15 Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.
You must not give back to his master a slave who has escaped from his master.
16 Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.
Let him live with you, in whatever town he chooses. Do not oppress him.
17 Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
There must be no cultic prostitute among any of the daughters of Israel, neither must there be a cultic prostitute among the sons of Israel.
18 Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.
You must not bring the wages of a prostitute or the wages of a dog into the house of Yahweh your God for any vow; for both these are abominations to Yahweh your God.
19 Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.
You must not lend on interest to your fellow Israelite—interest of money, interest of food, or the interest of anything that is lent on interest.
20 Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.
To a foreigner you may lend on interest; but to your fellow Israelite you must not lend on interest, so that Yahweh your God may bless you in all that you put your hand to, in the land which you are going in to possess.
21 Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.
When you make a vow to Yahweh your God, you must not be slow in fulfilling it, for Yahweh your God will surely require it of you; it would be sin for you not to fulfill it.
22 Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.
But if you will refrain from making a vow, it will be no sin for you.
23 Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.
That which has gone out from your lips you must observe and do; according as you have vowed to Yahweh your God, anything that you have freely promised with your mouth.
24 Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.
When you go into your neighbor's vineyard, you may eat as many grapes as you desire, but do not put any in your basket.
25 Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.
When you go into your neighbor's ripe grain, you may pluck the heads of grain with your hand, but do not put a sickle to your neighbor's ripe grain.

< Torati 23 >