< Torati 21 >

1 Kama mtu akikutwa ameuawa, naye amelala kwenye shamba katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki, wala haijulikani ni nani aliyemuua,
And if one be found slain with the sword in the land, which the Lord thy God gives thee to inherit, having fallen in the field, and they do not know who has smitten [him];
2 wazee wenu na waamuzi watatoka na kupima umbali kutoka maiti alipolala mpaka kwenye miji ya jirani.
thine elders and thy judges shall come forth, and shall measure the distances of the cities round about the slain man:
3 Kisha wazee wa ule mji ulio karibu zaidi na yule maiti watamchukua mtamba ambaye hajapata kufanyishwa kazi na ambaye hajafungwa nira,
and it shall be that the city which is nearest to the slain man the elders of that city shall take a heifer of the herd, which has not laboured, and which has not borne a yoke.
4 na kumpeleka kwenye bonde ambalo halijapata kulimwa au kupandwa mazao na ambapo kuna chemchemi itiririkayo. Huko kwenye hilo bonde, wazee watamvunja yule mtamba shingo.
And the elders of that city shall bring down the heifer into a rough valley, which has not been tilled and is not sown, and they shall slay the heifer in the valley.
5 Makuhani, hao wana wa Lawi, watasogea mbele, kwa kuwa Bwana Mungu wenu, amewachagua kuhudumu na kutoa baraka katika jina la Bwana, na kuamua mashauri yote ya mabishano na mashambulio.
And the priests the Levites shall come, because the Lord God has chosen them to stand by him, and to bless in his name, and by their word shall every controversy and every stroke be [decided].
6 Ndipo wazee wote wa mji ulio karibu zaidi na huyo maiti watanawa mikono yao juu ya huyo mtamba ambaye shingo yake imevunjwa huko kwenye bonde,
And all the elders of that city who draw nigh to the slain man shall wash their hands over the head of the heifer which was slain in the valley;
7 nao watatangaza: “Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona likifanyika.
and they shall answer and say, Our hands have not shed this blood, and our eyes have not seen [it].
8 Ee Bwana, ukubali upatanisho kwa watu wako Israeli, ambao umewakomboa, wala usiwahesabie watu wako hatia ya damu ya mtu asiyekuwa na hatia.” Nayo damu iliyomwagika itakuwa imefanyiwa upatanisho.
Be merciful to thy people Israel, whom thou hast redeemed, O Lord, that innocent blood may not be charged on thy people Israel: and the blood shall be atoned for to them.
9 Hivyo mtakuwa mmejitakasa wenyewe kutoka hatia ya kumwaga damu isiyokuwa na hatia, kwa kuwa mmefanya lile lililo sawa mbele za macho ya Bwana.
And thou shalt take away innocent blood from among you, if thou shouldest do that which is good and pleasing before the Lord thy God.
10 Mkienda vitani kupigana na adui zenu naye Bwana Mungu wenu akawatia adui mikononi mwenu, nanyi mkachukua mateka,
And if when thou goest out to war against thine enemies, the Lord thy God should deliver them into thine hands, and thou shouldest take their spoil,
11 kama ukiona miongoni mwa mateka mwanamke mzuri wa sura nawe wavutwa naye, waweza kumwoa akawa mke wako.
and shouldest see among the spoil a woman beautiful in countenance, and shouldest desire her, and take her to thyself for a wife,
12 Mlete nyumbani mwako, anyoe nywele na kukata kucha zake,
and shouldest bring her within thine house: then shalt thou shave her head, and pare her nails;
13 avue nguo alizokuwa amevaa alipotekwa. Baada ya kuishi nyumbani mwako na kumwombolezea baba yake na mama yake kwa mwezi mzima, ndipo utakapoweza kumwendea na kuwa mume wake naye atakuwa mke wako.
and shalt take away her garments of captivity from off her, and she shall abide in thine house, and shall bewail her father and mother the days of a month; and afterwards thou shalt go in to her and dwell with her, and she shall be thy wife.
14 Lakini kama hutaendelea kupendezwa naye, mwache aende popote anapotaka. Kamwe huwezi kumuuza au kumtendea kama mtumwa, kwa sababu utakuwa umemvunjia heshima.
And it shall be if thou do not delight in her, thou shalt send her out free; and she shall not by any means be sold for money, thou shalt not treat her contemptuously, because thou hast humbled her.
15 Kama mwanaume ana wake wawili, naye anampenda mmoja na mwingine hampendi na wote wawili wamemzalia wana wa kiume, lakini mwana mzaliwa wa kwanza ni wa yule mke asiyempenda,
And if a man have two wives, the one loved and the other hated, and both the loved and the hated should have born him [children], and the son of the hated should be first-born;
16 wakati anapotoa wosia wa mali yake kwa wanawe, kamwe asitoe haki za mzaliwa wa kwanza kwa mwana wa mke ampendaye kwa upendeleo, badala ya mzaliwa hasa wa kwanza, ambaye ni mwana wa mke ambaye hampendi.
then it shall be that whensoever he shall divide by inheritance his goods to his sons, he shall not be able to give the right of the first-born to the son of the loved one, having overlooked the son of the hated, which is the first-born.
17 Ni lazima amkubali mwana wa mke asiyempenda kama mzaliwa wa kwanza kwa kumpa sehemu ya vile vyote alivyo navyo maradufu. Mwana huyo ni ishara ya kwanza ya nguvu za baba yake. Haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.
But he shall acknowledge the first-born of the hated one to give to him double of all things which shall be found by him, because he is the first of his children, and to him belongs the birthright.
18 Kama mtu ana mwana mkaidi na mwasi ambaye hamtii baba yake na mama yake, na hasikii wazazi wanapomrudi,
And if any man has a disobedient and contentious son, who hearkens not to the voice of his father and the voice of his mother, and they should correct him, and he should not hearken to them;
19 baba yake na mama yake watamleta kwa wazee kwenye lango la mji wake.
then shall his father and his mother take hold of him, and bring him forth to the elders of his city, and to the gate of the place:
20 Watawaambia wazee, “Huyu mwanetu ni mkaidi na mwasi. Hatutii sisi, yeye ni mpotovu na mlevi.”
and they shall say to the men of their city, This our son is disobedient and contentious, he hearkens not to our voice, he is a reveler and a drunkard.
21 Kisha wanaume wote wa mjini mwake watampiga kwa mawe mpaka afe. Ndivyo imewapasa kuondoa maovu kati yenu. Israeli yote itasikia hili na kuogopa.
And the men of his city shall stone him with stones, and he shall die; and thou shalt remove the evil one from yourselves, and the rest shall hear and fear.
22 Kama mtu ana hatia ya kosa linalompasa kuuawa naye akauawa, mwili wake utaangikwa mtini,
And if there be sin in any one, [and] the judgment of death [be upon him], and he be put to death, and ye hang him on a tree:
23 kamwe msiuache mwili wake mtini usiku kucha. Hakikisheni mnauzika mwili wake siku ile ile, kwa sababu kila mtu anayeangikwa mtini yupo chini ya laana ya Mungu. Msiinajisi nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu.
his body shall not remain all night upon the tree, but ye shall by all means bury it in that day; for every one that is hanged on a tree is cursed of God; and ye shall by no means defile the land which the Lord thy God gives thee for an inheritance.

< Torati 21 >