< Torati 20 >

1 Mtakapokwenda vitani kupigana na adui zenu na mkaona farasi na magari ya vita na jeshi kubwa kuliko lenu, msiwaogope, kwa sababu Bwana Mungu wenu aliyewatoa kutoka Misri, atakuwa pamoja nanyi.
Quand tu iras à la guerre contre tes ennemis, et que tu verras des chevaux et des chars, un peuple plus nombreux que toi, ne les crains point; car l'Éternel ton Dieu qui t'a fait monter hors du pays d'Égypte est avec toi.
2 Wakati mtakapokaribia kwenda vitani, kuhani atakuja mbele na kuhutubia jeshi.
Et quand vous vous approcherez pour combattre, le sacrificateur s'avancera, et parlera au peuple.
3 Atasema: “Sikia, ee Israeli, leo unakwenda vitani kupigana na adui zako. Usife moyo wala usiogope, usitishwe wala usitiwe hofu mbele yao.
Et il leur dira: Écoute, Israël! Vous marchez aujourd'hui pour combattre vos ennemis; que votre cœur ne défaille point, ne craignez point, ne soyez point effrayés, et n'ayez point peur d'eux;
4 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ndiye huenda pamoja nanyi kuwapigania dhidi ya adui zenu na kuwapatia ushindi.”
Car l'Éternel votre Dieu est celui qui marche avec vous, afin de combattre pour vous contre vos ennemis, afin de vous délivrer.
5 Maafisa wataliambia jeshi: “Je, kuna yeyote aliyejenga nyumba mpya ambayo haijawekwa wakfu? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akaiweka wakfu.
Alors les officiers parleront au peuple, en disant: Qui est-ce qui a bâti une maison neuve, et ne l'a point inaugurée? qu'il s'en aille et retourne en sa maison, de peur qu'il ne meure dans la bataille, et qu'un autre ne l'inaugure.
6 Je, kuna yeyote aliyepanda shamba la mizabibu na hajaanza kulifurahia? Yeye na arudi nyumbani, au sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akalifurahia.
Et qui est-ce qui a planté une vigne, et n'en a point cueilli les premiers fruits? qu'il s'en aille et retourne en sa maison, de peur qu'il ne meure dans la bataille, et qu'un autre n'en cueille les premiers fruits.
7 Je, kuna yeyote aliyeposa mwanamke na hajamwoa? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akamwoa.”
Et qui est-ce qui a fiancé une femme, et ne l'a point épousée? qu'il s'en aille, et retourne en sa maison, de peur qu'il ne meure dans la bataille, et qu'un autre ne l'épouse.
8 Kisha maafisa wataongeza haya, “Je, kuna mtu anayeogopa ama kufa moyo? Yeye na arudi nyumbani ili ndugu zake nao wasije wakafa moyo pia.”
Et les officiers continueront à parler au peuple, et diront: Qui est-ce qui est craintif et lâche? qu'il s'en aille et retourne en sa maison, de peur que le cœur de ses frères ne se fonde comme le sien.
9 Wakati maafisa watakapomaliza kuzungumza na jeshi, watawateua wakuu wa vikosi.
Et dès que les officiers auront achevé de parler au peuple, ils établiront les chefs des troupes à la tête du peuple.
10 Wakati mtakapokwenda kushambulia mji, wapeni watu wake masharti ya amani.
Quand tu t'approcheras d'une ville pour l'attaquer, tu lui offriras la paix.
11 Wakikubali na kuwafungulia malango yao, watu wake wote watawatumikia kwa kufanya kazi ngumu na watawatumikia.
Et si elle te fait une réponse de paix et t'ouvre ses portes, tout le peuple qui s'y trouvera te sera tributaire et te servira.
12 Ikiwa watakataa kufanya mapatano ya amani na wakiwaingiza katika vita, basi mtauzunguka mji huo kwa vita.
Que si elle ne traite pas avec toi, mais qu'elle te fasse la guerre, alors tu l'assiégeras;
13 Wakati Bwana Mungu wenu atakapouweka mji huo mkononi mwenu, waueni kwa upanga wanaume wote waliomo ndani yake.
Et l'Éternel ton Dieu la livrera entre tes mains, et tu en feras passer tous les mâles au fil de l'épée.
14 Kwa upande wa wanawake, watoto, mifugo na kila kitu kingine chochote ndani ya huo mji, mnaweza kuvichukua kama nyara kwa ajili yenu. Nanyi mnaweza kuzitumia hizo nyara ambazo Bwana Mungu wenu amewapa kutoka kwa adui zenu.
Seulement, tu prendras pour toi les femmes, les petits enfants, le bétail et tout ce qui sera dans la ville, tout son butin. Et tu mangeras le butin de tes ennemis, que l'Éternel ton Dieu t'aura donné.
15 Hivi ndivyo mtakavyofanya kwa miji yote ambayo iko mbali nanyi, ambayo haimilikiwi na mataifa ya karibu.
Tu en feras ainsi à toutes les villes qui sont fort éloignées de toi, qui ne sont point des villes de ces nations-ci.
16 Hata hivyo, katika miji ya mataifa ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi, msiache kitu chochote hai kinachopumua.
Mais dans les villes de ces peuples que l'Éternel ton Dieu te donne en héritage, tu ne laisseras vivre rien de ce qui respire;
17 Waangamizeni kabisa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, kama Bwana Mungu wenu alivyowaamuru.
Car tu ne manqueras point de les vouer à l'interdit: les Héthiens, les Amoréens, les Cananéens, les Phéréziens, les Héviens, les Jébusiens, comme l'Éternel ton Dieu te l'a commandé,
18 La sivyo, watawafundisha kufuata mambo yote ya machukizo wanayofanya wakiabudu miungu yao, nanyi mtatenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu.
Afin qu'ils ne vous apprennent pas à imiter toutes les abominations qu'ils ont pratiquées envers leurs dieux, et que vous ne péchiez pas contre l'Éternel votre Dieu.
19 Wakati mtakapouzunguka mji kwa vita kwa muda mrefu, mkipigana dhidi yake ili kuuteka, msiharibu miti yake kwa kuikata kwa shoka, kwa sababu mtaweza kula matunda yake. Hivyo msiikate. Je, miti hiyo ya mashambani ni watu, hata muizingire?
Quand tu assiégeras une ville pendant longtemps, en l'attaquant pour la prendre, tu ne détruiras point ses arbres à coups de cognée, car tu pourras en manger le fruit; tu ne les couperas donc point; car l'arbre des champs est-il un homme, pour être assiégé par toi?
20 Hata hivyo, mnaweza kuikata miti ambayo sio miti ya matunda na kuitumia kujenga ngome, mpaka mji ulio katika vita na ninyi utakapoanguka.
Tu détruiras et tu couperas seulement les arbres que tu connaîtras n'être point des arbres fruitiers; et tu en bâtiras des forts contre la ville qui te fait la guerre, jusqu'à ce qu'elle succombe.

< Torati 20 >