< Torati 18 >

1 Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya Bwana za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao.
The priests the Levites [Descendants of United with], all the tribe of Levi [United with], shall have no portion nor inheritance with Israel [God prevails]. They shall eat the offerings of Adonai made by fire and his portion.
2 Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
They shall have no inheritance among their brothers. Adonai is their inheritance, as he has spoken to them.
3 Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo.
This shall be the priests’ mishpat ·due· from the people, from those who offer a sacrifice, whether it be ox or sheep, that they shall give to the priest the shoulder, the two cheeks, and the inner parts.
4 Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu,
The first fruits of your grain, of your new wine, and of your oil, and the first of the first fleece of your sheep, you shall give him.
5 kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la Bwana siku zote.
For Adonai your God has chosen him out of all your tribes, to stand to minister in Adonai’s name, him and his sons forever.
6 Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo Bwana atapachagua,
If a Levite comes from any of your gates out of all Israel [God prevails], where he lives as a foreigner, and comes with all the desire of his soul to the place which Adonai shall choose;
7 anaweza akahudumu katika jina la Bwana Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za Bwana.
then he shall minister in the name of Adonai his God, as all his brothers the Levites [Descendants of United with] do, who stand there before Adonai.
8 Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake.
They shall have like portions to eat, in addition to that which comes from the sale of his family possessions.
9 Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko.
When you have come into the land which Adonai your God gives you, you shall not learn to imitate the abominations of those nations.
10 Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi,
There shall not be found with you anyone who makes his son or his daughter to pass through the fire, one who uses divination, one who practices sorcery, or an enchanter, or a sorcerer,
11 wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu.
or a charmer, or a consulter with a familiar spirit, or a sorcerer, or a necromancer.
12 Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu.
For whoever does these things is detestable to Adonai. Because of these abominations, Adonai your God drives them out from before you.
13 Kamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mungu wenu.
You shall be perfect with Adonai your God.
14 Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo.
For these nations that you shall dispossess sh'ma ·hear obey· those who practice sorcery and to diviners; but as for you, Adonai your God has not allowed you so to do.
15 Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye.
Adonai your God will raise up to you a prophet from among you, of your brothers, like me. You shall sh'ma ·hear obey· him.
16 Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”
This is according to all that you desired of Adonai your God in Horeb [Desert] in the day of the assembly, saying, “Let me not sh'ma ·hear obey· again Adonai my God’s voice, neither let me see this great fire any more, that I not die.”
17 Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema.
Adonai said to me, “They have well said that which they have spoken.
18 Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru.
I will raise them up a prophet from among their brothers, like you. I will put my words in his mouth, and he shall speak to them all that I shall enjoin him.
19 Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha.
It shall happen, that whoever will not sh'ma ·hear obey· my words which he shall speak in my name, I will require it of him.
20 Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.”
But the prophet who speaks a word presumptuously in my name, which I have not enjoined him to speak, or who speaks in the name of other deities, that same prophet shall die.”
21 Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na Bwana?”
You may say in your heart, “How shall we know the word which Adonai has not spoken?”
22 Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la Bwana hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao Bwana hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.
When a prophet speaks in Adonai’s name, if the thing does not follow, nor happen, that is the thing which Adonai has not spoken. The prophet has spoken it presumptuously. You shall not be afraid of him.

< Torati 18 >