< Torati 14 >

1 Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa,
Ye [are] the children of the LORD your God: ye shall not cut yourselves, nor make any baldness between your eyes for the dead.
2 kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.
For thou [art] a holy people to the LORD thy God, and the LORD hath chosen thee to be a peculiar people to himself, above all the nations that [are] upon the earth.
3 Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
Thou shalt not eat any abominable thing.
4 Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
These [are] the beasts which ye shall eat: the ox, the sheep, and the goat,
5 kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
The hart, and the roebuck, and the fallow-deer, and the wild-goat, and the pygarg, and the wild ox, and the chamois.
6 Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
And every beast that parteth the hoof, and cleaveth the cleft into two claws, [and] cheweth the cud among the beasts, that ye shall eat.
7 Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
Nevertheless, these ye shall not eat, of them that chew the cud, or of them that divide the cloven hoof; the camel, and the hare, and the coney: for they chew the cud, but divide not the hoof; [therefore] they [are] unclean to you.
8 Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
And the swine, because it divideth the hoof, yet cheweth not the cud, [is] unclean to you: ye shall not eat of their flesh, nor touch their dead carcass.
9 Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
These ye shall eat, of all that [are] in the waters: all that have fins and scales shall ye eat:
10 Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
And whatever hath not fins and scales ye may not eat; it [is] unclean to you.
11 Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
[Of] all clean birds ye shall eat.
12 Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
But these [are they] of which ye shall not eat: the eagle, and the ossifrage, and the ospray,
13 kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
And the glede, and the kite, and the vultur after his kind,
14 kunguru wa aina yoyote,
And every raven after his kind,
15 mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
And the owl, and the night-hawk, and the cuckow, and the hawk after his kind,
16 bundi, mumbi, bundi mkubwa,
The little owl, and the great owl, and the swan,
17 mwari, nderi, mnandi,
And the pelican, and the gier-eagle, and the cormorant,
18 korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
And the stork, and the heron after her kind, and the lapwing, and the bat.
19 Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
And every creeping animal that flieth [is] unclean to you: they shall not be eaten.
20 Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
[But of] all clean fowls ye may eat.
21 Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
Ye shall not eat [of] any thing that dieth of itself: thou shalt give it to the stranger that [is] in thy gates, that he may eat it; or thou mayest sell it to an alien: for thou [art] a holy people to the LORD thy God. Thou shalt not seethe a kid in his mother's milk.
22 Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.
Thou shalt truly tithe all the increase of thy seed, that the field bringeth forth year by year.
23 Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima.
And thou shalt eat before the LORD thy God, in the place which he shall choose to place his name there, the tithe of thy corn, of thy wine, and of thy oil, and the firstlings of thy herds and of thy flocks; that thou mayest learn to fear the LORD thy God always.
24 Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),
And if the way is too long for thee, so that thou art not able to carry it; [or] if the place is too far from thee, which the LORD thy God shall choose to set his name there, when the LORD thy God hath blessed thee:
25 basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua.
Then shalt thou turn [it] into money, and bind up the money in thy hand, and shalt go to the place which the LORD thy God shall choose:
26 Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi.
And thou shalt bestow that money for whatever thy soul desireth, for oxen, or for sheep, or for wine, or for strong drink, or for whatever thy soul desireth: and thou shalt eat there before the LORD thy God, and thou shalt rejoice, thou, and thy household.
27 Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.
And the Levite that [is] within thy gates, thou shalt not forsake him; for he hath no part nor inheritance with thee.
28 Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,
At the end of three years thou shalt bring forth all the tithe of thy increase the same year, and shalt lay [it] up within thy gates:
29 ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.
And the Levite, (because he hath no part nor inheritance with thee) and the stranger, and the fatherless, and the widow, who [are] within thy gates, shall come, and shall eat and be satisfied; that the LORD thy God may bless thee in all the work of thy hand which thou doest.

< Torati 14 >