< Torati 10 >

1 Wakati ule Bwana aliniambia, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza uje kwangu juu mlimani. Pia utengeneze Sanduku la mbao.
En ce temps-là l'Eternel me dit: Taille-toi deux Tables de pierre comme les premières, et monte vers moi en la montagne, et puis tu te feras une Arche de bois.
2 Nitaandika juu ya vibao maneno yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza, ambavyo ulivivunja. Kisha utaviweka ndani ya Sanduku.”
Et j'écrirai sur ces Tables les paroles qui étaient sur les premières Tables que tu as rompues, et tu les mettras dans l'Arche.
3 Hivyo nikatengeneza Sanduku kwa mti wa mshita, nikachonga pia vibao vya mawe kama vile vya kwanza, kisha nikakwea mlimani nikiwa na vibao viwili mikononi mwangu.
Ainsi je fis une Arche de bois de Sittim, et je taillai deux Tables de pierre comme les premières; et je montai en la montagne, ayant les deux Tables en ma main.
4 Bwana akaandika juu ya hivi vibao kile alichokuwa amekiandika kabla, Amri Kumi alizokuwa amewatangazia juu mlimani, kutoka kwenye moto siku ile ya kusanyiko. Bwana akanikabidhi.
Et il écrivit dans ces Tables, comme il avait écrit la première fois, les dix paroles que l'Eternel vous avait prononcées sur la montagne, du milieu du feu, au jour de l'assemblée; puis l'Eternel me les donna.
5 Kisha nikashuka kutoka mlimani na kuweka vibao ndani ya Sanduku nililokuwa nimelitengeneza, kama Bwana alivyoniagiza, navyo viko huko sasa.
Je m'en retournai, je descendis de la montagne; je mis les Tables dans l'Arche que j'avais faite, et elles y sont demeurées, comme l'Eternel me l'avait commandé.
6 (Waisraeli walisafiri kutoka visima vya Yaakani hadi Mosera. Huko Aroni alifariki na kuzikwa, naye Eleazari mwanawe akachukua nafasi yake kama kuhani.
r les enfants d'Israël partirent de Beéroth Béné-Jahakan pour aller à Moséra. Aaron mourut là, et y fut enseveli, et Eléazar son fils fut Sacrificateur en sa place.
7 Kutoka pale, walisafiri hadi Gudgoda wakaendelea mpaka Yotbatha, nchi yenye vijito vya maji.
De là ils tirèrent vers Gudgod, et de Gudgod ils [allèrent] vers Jotbath, qui est un pays de torrents d'eaux.
8 Wakati huo Bwana aliteua kabila la Lawi kulibeba Sanduku la Agano la Bwana, kusimama mbele za Bwana ili kutoa huduma, na kutangaza baraka kwa Jina lake, kama wanavyofanya mpaka leo.
Or en ce temps-là l'Eternel avait séparé la Tribu de Lévi pour porter l'Arche de l'alliance de l'Eternel, pour se tenir devant la face de l'Eternel, pour le servir, et pour bénir en son Nom, jusqu'à ce jour.
9 Hiyo ndiyo sababu ya Walawi kutokuwa na sehemu wala urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama Bwana Mungu wao alivyowaambia.)
C'est pourquoi Lévi n'a point de portion ni d'héritage avec ses frères; [mais] l'Eternel est son héritage, ainsi que l'Eternel ton Dieu lui [en] a parlé.
10 Basi nilikaa mlimani kwa siku arobaini usiku na mchana, kama nilivyofanya mara ya kwanza, pia Bwana alinisikiliza hata wakati huu. Haikuwa nia yake kuwaangamiza.
Je me tins donc sur la montagne, comme la première fois; durant quarante jours et quarante nuits; et l'Eternel m'exauça encore cette fois-là; [ainsi] l'Eternel ne voulut point te détruire.
11 Bwana akaniambia, “Nenda, ukawaongoze watu katika njia yao ili kwamba waweze kuingia na kuimiliki nchi ile niliyowaapia baba zao kuwapa.”
Mais l'Eternel me dit: Lève-toi, va pour marcher devant ce peuple, afin qu'ils entrent au pays que j'ai juré à leurs pères de leur donner, et qu'ils le possèdent.
12 Na sasa, ee Israeli, Bwana Mungu wako anataka nini kwako ila kumcha Bwana Mungu wako, kwenda katika njia zake, kumpenda na kumtumikia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote,
Maintenant donc, ô Israël! qu'est-ce que demande de toi l'Eternel ton Dieu, sinon que tu craignes l'Eternel ton Dieu, que tu marches dans toutes ses voies, que tu l'aimes, et que tu serves l'Eternel ton Dieu de tout ton cœur, et de toute ton âme?
13 na kuyashika maagizo ya Bwana na amri zake ninazokupa leo kwa mafanikio yako mwenyewe?
En gardant les commandements de l'Eternel, et ses statuts, que je te commande aujourd'hui, afin que tu prospères.
14 Mbingu, hata mbingu za juu sana, dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, ni mali ya Bwana Mungu wako.
Voici, les cieux, et les cieux des cieux appartiennent à l'Eternel ton Dieu; la terre aussi, et tout ce qui [est] en elle.
15 Hata hivyo Bwana alikuwa na shauku na baba zako, akawapenda na akawachagua ninyi, wazao wao, kuliko mataifa yote, kama ilivyo leo.
[Mais] l'Eternel a pris son bon plaisir en tes pères seulement, pour les aimer, et il vous a choisis, vous qui êtes leur postérité après eux, entre tous les peuples; comme [il paraît] aujourd'hui.
16 Kwa hiyo tahirini mioyo yenu, na msiwe na shingo ngumu tena.
Circoncisez donc le prépuce de votre cœur, et ne roidissez plus votre cou.
17 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye uweza na wa kutisha, ambaye hana upendeleo na hapokei rushwa.
Car l'Eternel votre Dieu est le Dieu des dieux, et le Seigneur des seigneurs, le Fort, le grand, le puissant, et le terrible; qui n'a point d'égard à l'apparence des personnes, et qui ne prend point de présents;
18 Huwapigania yatima na wajane, humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi.
Qui fait droit à l'orphelin et à la veuve, qui aime l'étranger, pour lui donner de quoi se nourrir, et de quoi se vêtir.
19 Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri.
Vous aimerez donc l'étranger; car vous avez été étrangers au pays d'Egypte.
20 Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake.
Tu craindras l'Eternel ton Dieu, tu le serviras, tu t'attacheras à lui, et tu jureras par son Nom.
21 Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.
C'est lui qui est ta louange, et c'est lui qui est ton Dieu; qui a fait en ta faveur ces choses grandes et terribles que tes yeux ont vues.
22 Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.
Tes pères sont descendus en Egypte au nombre de soixante-dix âmes; et maintenant l'Eternel ton Dieu t'a fait devenir comme les étoiles des cieux, tant tu es en grand nombre.

< Torati 10 >