< Amosi 4 >

1 Sikilizeni neno hili, ninyi ngʼombe wa Bashani mlioko juu ya Mlima Samaria, ninyi wanawake mnaowaonea maskini, na kuwagandamiza wahitaji, na kuwaambia wanaume wenu, “Tuleteeni vinywaji!”
Écoutez cette parole, génisses de Bassan, qui êtes sur la montagne de Samarie, vous qui opprimez les petits, qui maltraitez les pauvres, qui dites à leurs maîtres: Apportez, et buvons!
2 Bwana Mwenyezi ameapa kwa utakatifu wake: “Hakika wakati utakuja mtakapochukuliwa na kulabu, na wanaosalia kwa ndoana za samaki.
Le Seigneur, l'Éternel, l'a juré par sa sainteté: Voici, les jours viennent sur vous, où l'on vous enlèvera avec des hameçons, et votre postérité avec des crochets de pêcheur.
3 Nanyi mtakwenda moja kwa moja kupitia mahali palipobomolewa kwenye ukuta, nanyi mtatupwa nje kuelekea Harmoni,” asema Bwana.
Vous sortirez par les brèches, chacune devant soi, et vous serez jetées vers la forteresse, dit l'Éternel.
4 “Nendeni Betheli mkatende dhambi; nendeni Gilgali mkazidi kutenda dhambi. Leteni dhabihu zenu kila asubuhi, zaka zenu kila mwaka wa tatu.
Allez à Béthel, et péchez; à Guilgal, et péchez davantage! Apportez vos sacrifices dès le matin, et vos dîmes tous les trois jours!
5 Mchome mkate uliotiwa chachu kama sadaka ya shukrani, jisifuni kuhusu sadaka zenu za hiari: jigambeni kwa ajili ya sadaka hizo, enyi Waisraeli, kwa kuwa hili ndilo mnalopenda kulitenda,” asema Bwana Mwenyezi.
Faites fumer vos offrandes d'action de grâces avec du levain; proclamez les offrandes volontaires et publiez-les; car c'est là ce que vous aimez, enfants d'Israël, dit le Seigneur, l'Éternel.
6 “Niliwapa njaa kwenye kila mji, na ukosefu wa chakula katika kila mji, hata hivyo bado hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
Et moi, je vous ai rendu les dents nettes dans toutes vos villes, et j'ai fait manquer le pain dans toutes vos demeures; et vous n'êtes pas revenus à moi, dit l'Éternel.
7 “Pia niliwazuilia ninyi mvua miezi mitatu kabla ya kufikia mavuno. Nilinyesha mvua kwenye mji mmoja, lakini niliizuia mvua isinyeshe mji mwingine. Shamba moja lilipata mvua, na lingine halikupata, nalo likakauka.
Je vous ai aussi refusé la pluie, quand il restait encore trois mois jusqu'à la moisson; j'ai fait pleuvoir sur une ville, et je n'ai pas fait pleuvoir sur une autre ville; un champ a reçu la pluie, et un autre champ, sur lequel il n'a point plu, a séché;
8 Watu walitangatanga mji hata mji kutafuta maji, lakini hawakupata ya kuwatosha kunywa, hata hivyo hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
Deux et trois villes sont allées vers une autre ville pour boire de l'eau, et n'ont pas été désaltérées; et vous n'êtes pas revenus à moi, dit l'Éternel.
9 “Mara nyingi nilizipiga bustani zenu na mashamba ya mizabibu, niliyapiga kwa kutu na ukungu. Nzige walitafuna tini zenu na miti ya mizeituni, hata hivyo hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
Je vous ai frappés par la rouille et par la pourriture des blés; vos jardins en grand nombre, vos vignes, vos figuiers et vos oliviers ont été dévorés par la sauterelle; et vous n'êtes pas revenus à moi, dit l'Éternel.
10 “Niliwapelekea tauni miongoni mwenu kama nilivyofanya kule Misri. Niliwaua vijana wenu wa kiume kwa upanga, niliwachukua farasi wenu. Nilijaza pua zenu kwa uvundo kutoka kwenye kambi zenu, hata hivyo hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
J'ai envoyé parmi vous la peste, telle que celle d'Égypte; et j'ai fait mourir par l'épée vos jeunes hommes, avec vos chevaux qui avaient été pris; et j'ai fait monter la puanteur de vos camps jusqu'à vos narines; et vous n'êtes pas revenus à moi, dit l'Éternel.
11 “Niliwaangamiza baadhi yenu kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora. Mlikuwa kama kijiti kiwakacho kilichonyakuliwa motoni, hata hivyo hamjanirudia,” asema Bwana.
Je vous ai détruits, comme Dieu détruisit Sodome et Gomorrhe; et vous avez été comme un tison arraché du feu; et vous n'êtes pas revenus à moi, dit l'Éternel.
12 “Kwa hiyo hili ndilo nitakalowafanyia, Israeli, na kwa sababu nitawafanyia hili, jiandaeni kukutana na Mungu wenu, ee Israeli.”
C'est pourquoi je te traiterai de la même manière, Israël; et puisque je te traiterai ainsi, prépare-toi à la rencontre de ton Dieu, ô Israël!
13 Yeye ambaye hufanya milima, anaumba upepo, na kufunua mawazo yake kwa mwanadamu, yeye ageuzaye asubuhi kuwa giza, na kukanyaga mahali pa juu pa nchi: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.
Car voici celui qui a formé les montagnes, et créé le vent, et qui révèle à l'homme quelle est sa pensée; qui fait l'aube et l'obscurité, et qui marche sur les hauteurs de la terre; son nom est l'Éternel, le Dieu des armées.

< Amosi 4 >