< Amosi 3 >

1 Sikilizeni neno hili alilosema Bwana dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:
Hear this word that the LORD hath spoken against you, O children of Israel, against the whole family which I brought up out of the land of Egypt, saying:
2 “Ni ninyi tu niliowachagua kati ya jamaa zote za dunia; kwa hiyo nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi zenu zote.”
You only have I known of all the families of the earth; therefore I will visit upon you all your iniquities.
3 Je, watu wawili hutembea pamoja wasipokubaliana kufanya hivyo?
Will two walk together, except they have agreed?
4 Je, simba hunguruma katika kichaka wakati hana mawindo? Aweza kuvuma katika pango wakati ambao hajakamata chochote?
Will a lion roar in the forest, when he hath no prey? Will a young lion give forth his voice out of his den, if he have taken nothing?
5 Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?
Will a bird fall in a snare upon the earth, where there is no lure for it? Will a snare spring up from the ground, and have taken nothing at all?
6 Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari, watu hawatetemeki? Mji upatwapo na maafa, je, si Bwana amesababisha?
Shall the horn be blown in a city, and the people not tremble? Shall evil befall a city, and the LORD hath not done it?
7 Hakika Bwana Mwenyezi hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
For the Lord GOD will do nothing, but He revealeth His counsel unto His servants the prophets.
8 Simba amenguruma: je, ni nani ambaye hataogopa? Bwana Mwenyezi ametamka: je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?
The lion hath roared, who will not fear? The Lord GOD hath spoken, who can but prophesy?
9 Tangazeni katika ngome za Ashdodi na katika ngome za Misri: “Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria; angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake, na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”
Proclaim it upon the palaces at Ashdod, and upon the palaces in the land of Egypt, and say: 'Assemble yourselves upon the mountains of Samaria, and behold the great confusions therein, and the oppressions in the midst thereof.'
10 Bwana asema: “Hawajui kutenda lililo jema, wale ambao hujilundikia nyara na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”
For they know not to do right, saith the LORD, who store up violence and robbery in their palaces.
11 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Adui ataizingira nchi; ataangusha chini ngome zenu na kuteka nyara maboma yenu.”
Therefore thus saith the Lord GOD: An adversary, even round about the land! And he shall bring down thy strength from thee, and thy palaces shall be spoiled.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba vipande viwili tu vya mfupa wa mguu au kipande cha sikio, hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa, wale wakaao Samaria kwenye kingo za vitanda vyao, na katika Dameski kwenye viti vyao vya fahari.”
Thus saith the LORD: As the shepherd rescueth out of the mouth of the lion two legs, or a piece of an ear, so shall the children of Israel that dwell in Samaria escape with the corner of a couch, and the leg of a bed.
13 “Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Hear ye, and testify against the house of Jacob, saith the Lord GOD, the God of hosts.
14 “Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake, nitaharibu madhabahu za Betheli; pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.
For in the day that I shall visit the transgressions of Israel upon him, I will also punish the altars of Beth-el, and the horns of the altar shall be cut off, and fall to the ground.
15 Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika, pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi; nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,” asema Bwana.
And I will smite the winter-house with the summer-house; and the houses of ivory shall perish, and the great houses shall have an end, saith the LORD.

< Amosi 3 >