< 2 Samweli 8 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
Après cela il arriva que David battit les Philistins, et les abaissa, et David prit Methegamma de la main des Philistins.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
Il battit aussi les Moabites, et les mesura au cordeau, les faisant coucher par terre; et il en mesura deux cordeaux pour les faire mourir, et un plein cordeau pour leur sauver la vie; et [le pays] des Moabites fut à David sous cette condition, qu'ils lui seraient sujets et tributaires.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
David battit aussi Hadadhézer fils de Réhob, Roi de Tsoba, comme il allait pour recouvrer ses limites sur le fleuve d'Euphrate.
4 Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
Et David lui prit mille et sept cents hommes de cheval, et vingt mille hommes de pied, et coupa les jarrets [des chevaux] de tous les chariots, mais il en réserva cent chariots.
5 Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
Car les Syriens de Damas étaient venus pour donner du secours à Hadadhézer Roi de Tsoba; et David battit vingt-deux mille Syriens.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Puis David mit garnison en Syrie de Damas, et [le pays] de ces Syriens fut à David sous cette condition, qu'ils lui seraient sujets et tributaires; et l'Eternel gardait David partout où il allait.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
Et David prit les boucliers d'or qui étaient aux serviteurs de Hadadhézer, et les apporta à Jérusalem.
8 Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
Le Roi David emporta aussi une grande quantité d'airain de Bétah, et de Bérothaï, villes de Hadadhézer.
9 Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
Or Tohi, Roi de Hamath, apprit que David avait défait toutes les forces de Hadadhézer.
10 akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
Et il envoya Joram son fils vers le Roi David, pour le saluer, et le féliciter de ce qu'il avait fait la guerre contre Hadadhézer, et de ce qu'il l'avait défait; car Hadadhézer était en guerre continuellement avec Tohi, et [Joram] apporta des vaisseaux d'argent, et des vaisseaux d'or, et des vaisseaux d'airain;
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
Lesquels David consacra à l'Eternel avec l'argent et l'or qu'il avait [déjà] consacrés [du butin] de toutes les nations qu'il s'était assujetties;
12 yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
De Syrie, de Moab, des enfants de Hammon, des Philistins, de Hamalec, et du butin de Hadadhézer, fils de Réhob, Roi de Tsoba.
13 Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
David s'acquit aussi [une grande] réputation de ce qu'en retournant de la défaite des Syriens, [il tailla en pièces] dans la vallée du sel dix-huit mille Iduméens.
14 Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
Et il mit garnison dans l'Idumée, il mit, dis-je, garnison dans toute l'Idumée; et tous les Iduméens furent assujettis à David; et l'Eternel gardait David partout où il allait.
15 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
Ainsi David régna sur tout Israël, faisant droit et justice à tout son peuple.
16 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Et Joab fils de Tséruja avait la charge de l'armée; et Jéhosaphat fils d'Ahilud, était commis sur les registres.
17 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
Et Tsadok fils d'Ahitub, et Ahimélec fils d'Abiathar étaient les Sacrificateurs, et Séraja était le Secrétaire.
18 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.
Et Bénaja fils de Jéhojadah était sur les Kéréthiens et les Péléthiens; et les fils de David étaient les principaux Officiers.

< 2 Samweli 8 >