< 2 Samweli 23 >

1 Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
Now these are the last words of David. David the son of Jesse says, the man whom God raised up, the anointed of the God of Jacob, the sweet psalmist of Israel:
2 “Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
"The Spirit of Jehovah spoke by me. His word was on my tongue.
3 Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
The God of Jacob said, the Rock of Israel spoke to me, 'One who rules over men righteously, who rules in the fear of God,
4 yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
shall be as the light of the morning, when the sun rises, a morning without clouds, when the tender grass springs out of the earth, through clear shining after rain.'
5 “Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
Most certainly my house is not so with God, yet he has made with me an everlasting covenant, ordered in all things, and sure, for it is all my salvation, and all my desire, although he doesn't make it grow.
6 Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
But all of the ungodly shall be as thorns to be thrust away, because they can't be taken with the hand,
7 Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
But the man who touches them must be armed with iron and the staff of a spear. They shall be utterly burned with fire in their place."
8 Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
These are the names of the warriors whom David had: Jeshbaal the son of Hachmoni, leader of the Three. He wielded his spear against eight hundred whom he killed at one time.
9 Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
After him was Eleazar the son of Dodo, the Ahohite, one of the Three warriors. He was with David in Pas Dammim when they defied the Philistines who were gathered there for battle, and the men of Israel had retreated.
10 lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
He arose, and struck the Philistines until his hand was weary, and his hand froze to the sword; and Jehovah worked a great victory that day; and the people returned after him only to take spoil.
11 Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
After him was Shamma the son of Agee the Hararite. The Philistines were gathered together at Lehi, where there was a plot of ground full of lentils; and the people fled from the Philistines.
12 Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
But he stood in the midst of the plot, and defended it, and killed the Philistines; and Jehovah worked a great victory.
13 Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
And three of the Thirty chief men went down, and came to David in the harvest time to the cave of Adullam; and the troop of the Philistines was camped in the Valley of Rephaim.
14 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
David was then in the stronghold; and the garrison of the Philistines was then in Bethlehem.
15 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
And David had a craving and said, "Oh that one would give me water to drink of the well of Bethlehem, which is by the gate."
16 Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
The Three warriors broke through the army of the Philistines, and drew water out of the well of Bethlehem, that was by the gate, and took it, and brought it to David: but he would not drink of it, but poured it out to Jehovah.
17 Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
He said, "Far be it from me, Jehovah, that I should do this. Shall I drink the blood of the men who went in jeopardy of their lives?" Therefore he would not drink it. The Three warriors did these things.
18 Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
And Abishai, the brother of Joab, the son of Zeruiah, was leader of the Thirty. And he wielded his spear against three hundred and killed them, and had a name beside the Three.
19 Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
He was the most illustrious of the Thirty, and he became their leader. However he did not attain to the Three.
20 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Benaiah the son of Jehoiada was a valiant man of Kabzeel, who performed great deeds. He killed the two sons of Ariel of Moab. He also went down and killed a lion in the midst of a pit in time of snow.
21 Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
He killed an Egyptian, a man of great stature. And the Egyptian had a spear in his hand; but he went down to him with a staff, and grabbed the spear out of the Egyptian's hand, and killed him with his own spear.
22 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
Benaiah the son of Jehoiada did these things, and had a name among the Three warriors.
23 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
He was more honored than the Thirty, but he did not attain to the Three. David set him over his guard.
24 Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
Asahel the brother of Joab was one of the Thirty; Elhanan the son of Dodo from Bethlehem,
25 Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
Shammah the Harodite, Elika the Harodite,
26 Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
Helez the Paltite, Ira the son of Ikkesh the Tekoite,
27 Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
Abiezer the Anathothite, Sibbekai the Hushathite,
28 Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
Zalmon the Ahohite, Maharai the Netophathite,
29 Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
Heled the son of Baanah the Netophathite, Ittai the son of Ribai of Gibeah of the people of Benjamin,
30 Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
Benaiah a Pirathonite, Hiddai of Nahale Gaash.
31 Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
Abiel son of the Arbathite, Azmaveth the Bahurimite,
32 Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
Eliahba the Shaalbinite, Jashen the Gizonite,
33 mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
Jonathan son of Shamma the Hararite, Ahiam the son of Sakar the Hararite,
34 Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
Eliphelet the son of Ahasbai the Maacathite, Eliam the son of Ahithophel the Gilonite,
35 Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
Hezrai the Carmelite, Paarai the Archite,
36 Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
Igal the son of Nathan, from the army of the Hagrites,
37 Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
Zelek the Ammonite, Naharai the Beerothite, armor bearer to Joab the son of Zeruiah,
38 Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
Ira the Jattirite, Gareb the Jattirite,
39 na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.
Uriah the Hethite: thirty-seven in all.

< 2 Samweli 23 >