< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
Et David adressa à l'Éternel les paroles de ce cantique, au jour où l'Éternel l'eut délivré de la main de tous ses ennemis, et de la main de Saül.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
Il dit: Éternel, mon rocher, ma forteresse et mon libérateur!
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
O Dieu, mon rocher, vers qui je me retire; mon bouclier et la force qui me délivre, ma haute retraite et mon asile! mon Sauveur! tu me garantis de la violence.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Je m'écrie: Loué soit l'Éternel! Et je suis délivré de mes ennemis.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Car les flots de la mort m'avaient environné, les torrents des méchants m'avaient effrayé;
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Les liens du Sépulcre m'avaient environné; les filets de la mort m'avaient surpris. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
Dans ma détresse, j'invoquai l'Éternel, je criai à mon Dieu; de son palais il entendit ma voix, et mon cri parvint à ses oreilles.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Alors la terre fut ébranlée et trembla, les fondements des cieux s'agitèrent et s'ébranlèrent, parce qu'il était courroucé.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Une fumée montait de ses narines, et de sa bouche un feu dévorant; il en jaillissait des charbons embrasés.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Il abaissa les cieux, et descendit, ayant l'obscurité sous ses pieds.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Il était monté sur un chérubin et volait; il parut sur les ailes du vent.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
Il mit autour de lui les ténèbres comme une tente, des amas d'eaux, des nuées épaisses.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
De la splendeur qui était devant lui, s'embrasèrent des charbons de feu.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
L'Éternel tonna des cieux; le Très-Haut fit retentir sa voix.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
Il lança des flèches, et dispersa mes ennemis; il lança des éclairs, et les mit en déroute.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Alors le fond de la mer apparut, et les fondements du monde se découvrirent, par la menace de l'Éternel, par le souffle du vent de sa colère.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Il étendit sa main d'en haut, et me prit; il me tira des grosses eaux.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Il me délivra de mon ennemi puissant, et de mes adversaires qui étaient plus forts que moi.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Ils m'avaient surpris au jour de ma calamité, mais l'Éternel fut mon appui.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Il m'a mis au large; il m'a délivré, parce qu'il a pris son plaisir en moi.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
L'Éternel m'a traité selon ma justice; il m'a rendu selon la pureté de mes mains;
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Car j'ai gardé les voies de l'Éternel, et je n'ai point été infidèle à mon Dieu.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Car toutes ses ordonnances sont devant moi, et je ne m'écarte point de ses statuts.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
J'ai été intègre devant lui, et je me suis gardé de mon iniquité.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Aussi l'Éternel m'a rendu selon ma justice, selon ma pureté à ses yeux.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Avec celui qui est bon, tu es bon; avec l'homme intègre tu es intègre.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
Avec celui qui est pur, tu te montres pur; mais avec le pervers, tu agis selon sa perversité.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Tu sauves le peuple affligé; mais de ton regard tu abaisses les orgueilleux.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Car tu es ma lampe, ô Éternel! Et l'Éternel fait resplendir mes ténèbres.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Avec toi je fonds sur une troupe; avec mon Dieu je franchis la muraille.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
La voie de Dieu est parfaite, la parole de l'Éternel est éprouvée; il est le bouclier de tous ceux qui se retirent vers lui.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Car qui est Dieu, sinon l'Éternel? Et qui est un rocher, sinon notre Dieu?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Le Dieu qui est ma forteresse assurée, et qui enseigne à l'homme intègre sa voie;
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Qui rend mes pieds semblables à ceux des biches, et m'affermit sur mes hauteurs;
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Qui forme mes mains au combat, et mes bras bandent un arc d'airain.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Tu m'as donné le bouclier de ton salut, et ta bonté m'a fait devenir grand.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Tu élargis le chemin sous mes pas, et mes pieds ne chancellent point.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Je poursuis mes ennemis; je les détruis; et je ne reviens qu'après les avoir exterminés.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Je les consume, je les écrase, et ils ne se relèvent plus; ils tombent sous mes pieds.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Car tu m'as ceint de force pour le combat; tu fais plier sous moi mes adversaires.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Tu fais tourner le dos à mes ennemis devant moi; ceux qui me haïssent, je les détruis.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Ils regardent, et point de libérateur! Ils crient à l'Éternel, mais il ne leur répond point.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Et je les broie comme la poussière de la terre; je les écrase, je les foule comme la boue des rues.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Tu me sauves des dissensions de mon peuple; tu me gardes pour être chef des nations. Le peuple que je ne connaissais pas, m'est assujetti.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Les fils de l'étranger viennent me flatter; dès que leur oreille a entendu, ils se sont soumis.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Les fils de l'étranger défaillent, et sortent tremblants de leurs retraites.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
L'Éternel est vivant! Et béni soit mon rocher! Que Dieu, le rocher de mon salut, soit exalté!
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
Le Dieu qui me donne vengeance, et qui m'assujettit les peuples; qui me fait échapper à mes ennemis.
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Tu m'élèves au-dessus de mes adversaires, tu me délivres de l'homme violent.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
C'est pourquoi, ô Éternel, je te louerai parmi les nations, et je chanterai ton nom!
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
C'est lui qui délivre magnifiquement son roi, et qui fait miséricorde à son oint, à David et à sa postérité, à jamais!

< 2 Samweli 22 >