< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
David spoke to Jehovah the words of this song in the day that Jehovah delivered him out of the hand of all his enemies, and out of the hand of Saul:
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
and he said, "Jehovah is my Rock, and my fortress, and my deliverer.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
My God, my Rock, in him I will take refuge, my shield, and the horn of my salvation, my high tower, and my refuge, my savior; from violent people he saves me.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
I call on Jehovah, who is worthy to be praised, and I am saved from my enemies.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
For the waves of death surrounded me, and the currents of ungodliness overwhelmed me.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
The cords of Sheol were around me. The snares of death caught me. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
In my distress I called upon Jehovah, and I cried out to my God. He heard my voice out of his temple, and my cry came into his ears.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Then the earth shook and trembled. The foundations of the mountains quaked and were shaken, because he was angry.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Smoke went up out of his nostrils. Fire out of his mouth devoured. Coals were kindled by it.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
He bowed the heavens also, and came down. Thick darkness was under his feet.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
He rode on a cherub, and flew; and he soared on the wings of the wind.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
He made darkness his hiding place, his canopy around him thick clouds dark with water.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
From the brightness before him his thick clouds passed on, with hailstones and coals of fire.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Jehovah thundered from heaven. The Most High uttered his voice.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
And he sent out arrows and scattered them, and he shot lightning bolts and routed them.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Then the channels of the sea appeared. The foundations of the world were laid bare by the rebuke of Jehovah, at the blast of the breath of his nostrils.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
He sent from on high and he took me. He drew me out of many waters.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
He delivered me from my strong enemy, from those who hated me, for they were too mighty for me.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
They came on me in the day of my calamity, but Jehovah was my support.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
He also brought me out into a large place. He delivered me, because he delighted in me.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Jehovah rewarded me according to my righteousness. He rewarded me according to the cleanness of my hands.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
For I have kept the ways of Jehovah, and have not wickedly departed from my God.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
For all his ordinances were before me, and his statutes I did not put away from me.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
I was also perfect toward him. I kept myself from my iniquity.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Therefore Jehovah has rewarded me according to my righteousness, according to the cleanness of my hands in his sight.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
With the faithful you show yourself faithful. With the innocent you show yourself innocent.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
With the pure you show yourself pure. And with the crooked you show yourself tortuous.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
You save a humble people, but the eyes of the proud you will bring low.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
For you light my lamp. Jehovah my God lights up my darkness.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
For by you, I run against a troop. By my God, I leap over a wall.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
As for God, his way is perfect. The word of Jehovah is pure. He is a shield to all those who take refuge in him.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
For who is God, besides Jehovah? Who is a rock, besides our God,
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
the God who girds me with strength, and makes my way blameless?
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
He makes my feet like those of a deer, and sets me on my high places.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
He teaches my hands to war, so that my arms bend a bow of bronze.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
You have also given me the shield of your salvation, and your right hand holds me up, and your help has made me great.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
You have enlarged my steps under me. My feet have not slipped.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
I pursued my enemies and overtook them, and I did not turn back until they were destroyed.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
And I consumed them, and struck them through, so that they did not rise. And they fell beneath my feet.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
For you have equipped me with strength for the battle. You have subdued under me those who rose up against me.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
You have also made my enemies turn their backs to me, that I might cut off those who hate me.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
They cry out, but there was none to save; even to Jehovah, but he did not answer them.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Then I ground them as fine as the dust on the surface of a path. Like the mud in the streets, I trampled them.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
You also have delivered me from the strivings of my people. You have kept me to be the head of the nations. A people whom I have not known will serve me.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
As soon as they hear of me they obey me. Foreigners come cringing to me;
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
they are not bound in chains.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Jehovah lives. Blessed be my rock. Exalted be God, the rock of my salvation,
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
even the God who executes vengeance for me, and subdues peoples under me,
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
who brings me away from my enemies. Yes, you lift me up above those who rise up against me. You protect me from the violent man.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Therefore I will praise you, Jehovah, among the nations, and will sing praises to your name.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
He gives great deliverance to his king, and shows loving kindness to his anointed, to David and to his descendants, until forever."

< 2 Samweli 22 >