< 2 Samweli 2 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
Après cela, David consulta l'Éternel, en disant: Monterai-je en quelqu'une des villes de Juda? Et l'Éternel lui répondit: Monte. Et David dit: Dans laquelle monterai-je? L'Éternel répondit: A Hébron.
2 Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
David monta donc là, avec ses deux femmes, Achinoam de Jizréel, et Abigaïl, de Carmel, qui avait été femme de Nabal.
3 Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
David fit monter aussi les hommes qui étaient avec lui, chacun avec sa famille, et ils demeurèrent dans les villes d'Hébron.
4 Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
Et ceux de Juda vinrent, et là ils oignirent David pour roi sur la maison de Juda. Et on rapporta à David que les gens de Jabès de Galaad avaient enseveli Saül.
5 akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
Alors David envoya des messagers vers les gens de Jabès de Galaad, et leur fit dire: Soyez bénis de l'Éternel, vous qui avez usé de cette humanité envers Saül, votre seigneur, et l'avez enseveli;
6 Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
Maintenant donc que l'Éternel veuille user envers vous de fidélité et de grâce! Et moi aussi je vous ferai du bien, parce que vous avez fait cela.
7 Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
Et maintenant, que vos mains se fortifient, et soyez des hommes de cœur; car Saül, votre seigneur, est mort, et la maison de Juda m'a oint pour être roi sur elle.
8 Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
Mais Abner, fils de Ner, chef de l'armée de Saül, prit Ishbosheth, fils de Saül, et le fit passer à Mahanaïm;
9 Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
Et il l'établit roi sur Galaad, sur les Ashuriens, sur Jizréel, sur Éphraïm, sur Benjamin, sur tout Israël.
10 Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
Ishbosheth, fils de Saül, était âgé de quarante ans quand il commença à régner sur Israël, et il régna deux ans. Il n'y eut que la maison de Juda qui suivit David.
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
Et le nombre des jours que David régna à Hébron sur la maison de Juda, fut de sept ans et six mois.
12 Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
Or Abner, fils de Ner, et les gens d'Ishbosheth, fils de Saül, sortirent de Mahanaïm pour marcher vers Gabaon.
13 Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
Joab aussi, fils de Tséruja, et les gens de David sortirent; et ils se rencontrèrent vers l'étang de Gabaon et se tinrent les uns de ce côté-ci de l'étang, les autres au delà de l'étang.
14 Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
Alors Abner dit à Joab: Que ces jeunes gens se lèvent maintenant, et qu'ils se battent devant nous. Et Joab dit: Qu'ils se lèvent!
15 Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
Ils se levèrent donc, et s'avancèrent en nombre égal, douze pour Benjamin et pour Ishbosheth, fils de Saül, et douze des gens de David.
16 Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
Alors chacun, saisissant son adversaire par la tête, lui passa son épée par le flanc, et ils tombèrent tous ensemble; et ce lieu-là fut appelé Helkath-Hatsurim (le champ des épées); il est près de Gabaon.
17 Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
Et il y eut, ce jour-là, un très rude combat, dans lequel Abner fut battu, avec ceux d'Israël, par les gens de David.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
Les trois fils de Tséruja, Joab, Abishaï et Asaël, étaient là. Or Asaël était léger de ses pieds comme un chevreuil dans la campagne.
19 Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
Et Asaël poursuivit Abner, sans se détourner de lui ni à droite ni à gauche.
20 Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
Abner regarda donc en arrière et dit: Est-ce toi, Asaël? Et il répondit: C'est moi.
21 Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
Et Abner lui dit: Détourne-toi à droite ou à gauche, et saisis-toi de l'un de ces jeunes gens, et prends sa dépouille pour toi. Mais Asaël ne voulut point se détourner de lui.
22 Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
Et Abner continuait à dire à Asaël: Détourne-toi de moi; pourquoi te jetterai-je mort par terre? et comment oserais-je paraître devant Joab, ton frère?
23 Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
Mais il ne voulut point se détourner; alors Abner le frappa au ventre avec le bout de derrière de sa lance, tellement que sa lance lui sortit par derrière; et il tomba là et mourut sur place; et tous ceux qui arrivaient au lieu où Asaël était tombé mort, s'arrêtaient.
24 Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
Joab et Abishaï poursuivirent donc Abner, et le soleil se couchait comme ils arrivaient au coteau d'Amma, qui est vis-à-vis de Guiach, au chemin du désert de Gabaon.
25 Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
Et les Benjamites se rallièrent auprès d'Abner, et se rangèrent en un bataillon, et se tinrent sur le sommet d'un coteau.
26 Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
Alors Abner cria à Joab, et dit: L'épée dévorera-t-elle sans cesse? Ne sais-tu pas bien qu'il y aura de l'amertume à la fin? et jusqu'à quand différeras-tu de dire au peuple qu'il cesse de poursuivre ses frères?
27 Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
Et Joab dit: Dieu est vivant! si tu n'eusses parlé, dès le matin déjà le peuple se serait retiré, chacun de la poursuite de son frère.
28 Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
Joab sonna donc de la trompette, et tout le peuple s'arrêta; et ils ne poursuivirent plus Israël et ne continuèrent plus à combattre.
29 Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
Ainsi Abner et ses gens marchèrent toute cette nuit-là par la campagne, et passèrent le Jourdain, et traversèrent tout le Bithron, et arrivèrent à Mahanaïm.
30 Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
Joab revint aussi de la poursuite d'Abner; et quand il eut assemblé tout le peuple, on trouva que des gens de David il manquait dix-neuf hommes, et Asaël.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
Mais les gens de David avaient frappé à mort trois cent soixante hommes de Benjamin et des gens d'Abner.
32 Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.
Et ils emportèrent Asaël, et l'ensevelirent dans le tombeau de son père, à Bethléhem. Et Joab et ses gens marchèrent toute la nuit, et au point du jour ils arrivèrent à Hébron.

< 2 Samweli 2 >