< 2 Samweli 11 >

1 Katika mwanzo wa mwaka mpya, wakati wafalme watokapo kwenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu pamoja na watu wa mfalme na jeshi lote la Israeli. Wakawaangamiza Waamoni na kuuzunguka kwa jeshi mji wa Raba. Lakini Daudi akabaki Yerusalemu.
It happened, at the return of the year, at the time when kings go out, that David sent Joab, and his servants with him, and all Israel; and they destroyed the people of Ammon, and besieged Rabbah. But David stayed at Jerusalem.
2 Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura,
It happened at evening, that David arose from off his bed, and walked on the roof of the king's house; and he saw a woman bathing, and the woman was very beautiful in appearance.
3 naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?”
David sent and inquired after the woman. One said, "Isn't this Bathsheba, the daughter of Eliam, the wife of Uriah the Hethite?"
4 Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake.
David sent messengers, and took her; and she came in to him, and he lay with her (for she was purified from her uncleanness); and she returned to her house.
5 Huyo mwanamke akapata mimba akampelekea Daudi ujumbe, kusema, “Mimi ni mjamzito.”
The woman conceived; and she sent and told David, and said, "I am with child."
6 Ndipo Daudi akapeleka ujumbe kwa Yoabu, “Unipelekee Uria, Mhiti.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
Then David sent to Joab and said, "Send me Uriah the Hethite." So Joab sent Uriah to him.
7 Uria alipofika, Daudi akamuuliza habari za Yoabu, hali za askari na vita kwamba inaendeleaje.
And Uriah came to him, and David asked about the prosperity of Joab, and of the prosperity of the people, and of the prosperity of the war. And he said, "Its well."
8 Kisha Daudi akamwambia Uria, “Teremka nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Basi Uria akaondoka kutoka kwenye jumba la kifalme, tena zawadi zikamfuata kutoka kwa mfalme.
And David said to Uriah, "Go down to your house, and wash your feet." So Uriah went out from the presence of the king, and a gift from the king was sent after him.
9 Lakini Uria akalala kwenye ingilio la jumba la kifalme pamoja na watumishi wote wa bwana wake, na hakuteremka kwenda nyumbani kwake.
But Uriah slept at the door of the king's house with all the servants of his lord, and did not go down to his house.
10 Daudi alipoambiwa kwamba, “Uria hakwenda nyumbani,” Daudi akamuuliza, “Je, si ndiyo tu umefika kutoka safari ya mbali? Kwa nini hukwenda nyumbani?”
And it was reported to David, saying, "Uriah did not go down to his house." So David said to Uriah, "Haven't you come from a journey? Why did you not go down to your house?"
11 Uria akamwambia Daudi, “Sanduku la Mungu, na Israeli na Yuda wanakaa kwenye mahema, naye bwana wangu Yoabu na watu wa bwana wangu wamepiga kambi mahali pa wazi. Ningewezaje kwenda nyumbani kwangu ili nile, ninywe na kukutana na mke wangu? Hakika kama uishivyo sitafanya jambo la namna hiyo!”
Uriah said to David, "The ark, Israel, and Judah, are staying in tents; and my lord Joab, and the servants of my lord, are camped in the open field. Shall I then go into my house to eat and to drink, and to lie with my wife? As the LORD lives, and as you live, I will not do this thing."
12 Ndipo Daudi akamwambia, “Kaa hapa siku moja zaidi, nami kesho nitakutuma urudi.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku ile na siku iliyofuata.
David said to Uriah, "Stay here today also, and tomorrow I will let you depart." So Uriah stayed in Jerusalem that day.
13 Kwa ukaribisho wa Daudi, Uria akala na kunywa pamoja naye, Daudi akamlevya. Lakini jioni Uria alitoka kwenda kulala juu ya mkeka wake miongoni mwa watumishi wa bwana wake, hakwenda nyumbani.
And the next day David summoned him, and he ate and drank in his presence, and he made him drunk. But in the evening he went out and lay on a bed with the servants of his lord, and did not go down to his house.
14 Asubuhi yake Daudi akamwandikia Yoabu barua, akamtuma Uria kuipeleka.
It happened in the morning, that David wrote a letter to Joab, and sent it by the hand of Uriah.
15 Ndani ya barua aliandika, “Mweke Uria mstari wa mbele mahali ambapo mapigano ni makali sana. Kisha wewe uondoke ili Uria aangushwe chini na kuuawa.”
He wrote in the letter, saying, "Send Uriah to the forefront of the hottest battle, and retreat from him, that he may be struck, and die."
16 Hivyo Yoabu alipokuwa ameuzingira mji kwa jeshi, akamweka Uria mahali ambapo alijua kuwa ulinzi wa adui ulikuwa imara sana.
It happened, when Joab kept watch on the city, that he assigned Uriah to the place where he knew that valiant men were.
17 Wakati watu wa mjini walipotoka kwenda kupigana dhidi ya Yoabu, baadhi ya watu katika jeshi la Daudi wakauawa, zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, akafa.
The men of the city went out, and fought with Joab. Some of the people fell, even of the servants of David; and Uriah the Hethite died also.
18 Yoabu akampelekea Daudi maelezo yote ya vita.
Then Joab sent and told David all the things concerning the war;
19 Akamwagiza mjumbe hivi, “Utakapokuwa umemaliza kumpa mfalme maelezo ya vita,
and he commanded the messenger, saying, "When you have finished telling all the things concerning the war to the king,
20 hasira ya mfalme yaweza kuwaka, naye aweza kukuuliza, ‘Kwa nini mlisogea karibu hivyo na mji kupigana? Hamkujua kuwa wangeweza kuwapiga mishale kutoka ukutani?
it shall be that, if his anger rises and he asks you, 'Why did you go so near to the city to fight? Did you not know that they would shoot from the wall.
21 Ni nani aliyemuua Abimeleki mwana wa Yerub-Besheth? Je, mwanamke hakutupa juu yake jiwe la juu la kusagia kutoka ukutani, kwa hiyo akafa huko Thebesi? Kwa nini mlisogea hivyo karibu ya ukuta?’ Ikiwa atakuuliza hivi, ndipo umwambie, ‘Pia mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa.’”
Who struck Abimelech the son of Jerubbaal? Did a woman not cast an upper millstone on him from the wall, so that he died at Thebez? Why did you go so near the wall?' Then you shall say, 'Your servant Uriah the Hethite is dead also.'"
22 Mjumbe akaondoka. Alipowasili akamwambia Daudi kila kitu alichokuwa ametumwa na Yoabu kusema.
And the messenger of Joab went to the king in Jerusalem and came and reported to David all that Joab had told him.
23 Mjumbe akamwambia Daudi, “Watu walituzidi nguvu wakatoka nje ya mji dhidi yetu kwenye eneo la wazi, lakini tuliwarudisha nyuma mpaka kwenye ingilio la mji.
The messenger said to David, "The men prevailed against us, and came out to us into the field, and we were on them even to the entrance of the gate.
24 Ndipo wapiga upinde walitupa mishale kwa watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watu wa mfalme wakafa. Zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, mtumishi wako amekufa.”
And the archers shot at your servants from off the wall, and some eighteen men of the king's servants are dead. And your servant Uriah the Hethite is dead also."
25 Daudi akamwambia mjumbe, “Ukamwambie Yoabu hivi, ‘Jambo hili lisikutie wasiwasi, upanga hula huyu sawa na ulavyo mwingine. Zidisha mashambulizi dhidi ya mji na uangamize.’ Mwambie Yoabu hivi ili kumtia moyo.”
Then David said to the messenger, "Thus you shall tell Joab, 'Do not let this thing displease you, for the sword devours one as well as another. Make your battle stronger against the city, and overthrow it.' Encourage him."
26 Mke wa Uria aliposikia kwamba mumewe amekufa, akamwombolezea.
When the wife of Uriah heard that Uriah her husband was dead, she made lamentation for her husband.
27 Baada ya muda wa maombolezo kwisha, Daudi akamtaka aletwe nyumbani kwake, naye akawa mkewe, na akamzalia mwana. Lakini jambo alilokuwa amefanya Daudi lilimchukiza Bwana.
When the mourning was past, David sent and took her home to his house, and she became his wife, and bore him a son. But the thing that David had done displeased the LORD.

< 2 Samweli 11 >