< 2 Wafalme 23 >

1 Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
And thei telden to the kyng that, that sche seide; `which kyng sente, and alle the elde men of Juda, and of Jerusalem, weren gaderid to hym.
2 Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
And the kyng stiede in to the temple of the Lord, and alle the men of Juda, and alle men that dwelliden in Jerusalem with hym, the preestis, and the prophetis, and al the puple, fro litil `til to greet; and he redde, while alle men herden, alle the wordis of the book of boond of pees of the Lord, which book was foundun in the hows of the Lord.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
And the kyng stood on the grees; and he smoot boond of pees bifor the Lord, that thei schulden go aftir the Lord, and kepe hise comaundementis and witnessyngis and cerymonyes in al the herte and in al the soule, that thei schulden reise the wordis of this boond of pees, that weren writun in that book; and the puple assentide to the couenaunt.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
And the kyng comaundide to Helchie, the bischop, and to the preestis of the secounde ordre, and to the porteris, that thei schulden caste out of the temple alle the vesselis, that weren maad to Baal, and in the wode, and to al the knyythod of heuene; and he brente tho vessels with out Jerusalem, in the euene valey of Cedron, and he bar the poudir of tho `vessels in to Bethel.
5 Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
And he dide awei false dyuynours `that dyuynyden in the entrailis of beestis sacrified to idols, whiche the kingis of Juda hadden sett to make sacrifice in hiy thingis bi the citees of Juda, and in the cumpas of Jerusalem; and he dide awey hem that brenten encense to Baal, and to the sunne, and to the moone, and to twelue signes, and to al the knyythod of heuene.
6 Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
And he made the wode to be borun out of the hows of the Lord without Jerusalem in the euene valey of Cedron, and he brente it there; and he droof it in to poudir, and castide it forth on the sepulcris of the comyn puple.
7 Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
Also he distriede the litle housis of `men turnyd into wommens condiciouns, whiche housis weren in the hows of the Lord; for whiche the wymmen `maden as litil howsis of the wode.
8 Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
And he gaderide alle the preestis fro the citees of Juda, and he defoulide the hiye thingis, where the preestis maden sacrifice, fro Gabaa `til to Bersabee; and he distriede the auters of yatis in the entryng of the dore of Josie, prince of a citee, which dore was at the lift half of the yate of the cytee.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Netheles the preestis of hiye thingis stieden not to the auter of the Lord in Jerusalem, but oneli thei eten therf looues in the myddis of her britheren.
10 Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
Also he defoulide Tophet, which is in the euene valey of the sone of Ennon, that no man schulde halewe his sone ether his douytir bi fier to Moloch.
11 Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
Also he dide awei horsis, whiche the kyngis of Juda hadden youe to the sunne, in the entryng of the temple of the Lord, bisidis the chaumbir of Nathanmalech, geldyng, that was in Pharurym; forsothe he brente bi fier the charis of the sunne.
12 Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
Also the kyng distriede the auteris, that weren on the roouys of the soler of Achaz, whiche auteris the kyngis of Juda hadden maad; and the kyng distriede the auteris, whiche Manasses hadde maad in the twei grete placis of the temple of the Lord; and he ran fro thennus, and scateride the askis of tho in to the strond of Cedron.
13 Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
Also the kyng defoulide the hiye thingis, that weren in Jerusalem at the riyt part of the hil of offencioun, whiche Salomon, kyng of Israel, hadde bildid to Astroth, the ydol of Sidoneis, and to Chamos, the offencioun of Moab, and to Melchon, abhominacioun of the sones of Amon;
14 Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
and he al to-brak ymagis, and kittide doun wodis, and fillide the places of tho with the boonys of deed men.
15 Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
Ferthermore also he distriede the auter that was in Bethel, and `he distriede the hiye thing, which Jeroboam, sone of Nabath, hadde maad, that made Israel to do synne; and he distriede that hiy autir, and brente it, and al to brak it in to poudir, and kittide doun also the wode.
16 Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
And Josias turnyde, and siy there sepulcris that weren in the hil; and he sente, and took the boonys fro the sepulcris, and brente tho on the auter, and defoulide it bi the word of the Lord, which word the man of God spak, that biforseide these wordis.
17 Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
And the kyng seide, What is this biriel, which Y se? And the citeseyns of that citee answeriden to hym, It is the sepulcre of the man of God, that cam fro Juda, and biforseide these wordis, whiche thou hast doon on the auter of Bethel.
18 Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
And the kyng seide, Suffre ye hym; no man moue hise boonys. And hise boonys dwelliden vntouchid with the boones of the prophete, that cam fro Samarie.
19 Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
Ferthermore also Josias dide awei alle the templis of hiye thingis, that weren in the citees of Samarie, whiche the kyngis of Israel hadden maad to terre the Lord to ire; and he dide to tho templis bi alle thingis whiche he hadde do in Bethel.
20 Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
And he killide alle the preestis of hiye thingis, that weren there on the auteris, and he brente mennus boonus on tho auteris; and he turnede ayen to Jerusalem;
21 Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
and comaundide to al the puple, and seide, Make ye pask to `youre Lord God, vp that, that is writun in the book of this boond of pees.
22 Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
Forsothe sich pask was not maad, fro the daies of iugis that demyden Israel, and of alle daies of the kyngis of Israel and of Juda,
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
as this pask was maad to the Lord in Jerusalem in the eiytenthe yeer of kyng Josias.
24 Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
But also Josias dide awei men hauynge fendis spekinge in her wombis, and false diuinouris in auteris, and `he dide awei the figuris of idols, and alle vnclennessis, and abhomynaciouns, that weren in the lond of Juda and in Jerusalem, that he schulde do the wordis of the lawe, that weren writun in the book, `which book Elchie, the preest, foond in the temple of the Lord.
25 Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
No kyng bifor him was lijk hym, `that turnede ayen to the Lord in al his herte, and in al his soule, and in al his vertu, bi al the lawe of Moises; nether aftir hym roos ony lijk hym.
26 Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
Netheles the Lord was not turned awei fro the ire of his greet veniaunce, bi which his strong veniaunce was wrooth ayens Juda, for the terryngis to ire by whiche Manasses hadde terrid hym to ire.
27 Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
Therfor the Lord seide, Y schal do awei also Juda fro my face, as Y dide awei Israel; and Y schal caste awei this citee, which Y chees, Jerusalem, and the hows `of which Y seide, My name schal be there.
28 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Forsothe the residue of wordis of Josias, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Juda?
29 Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
In the daies of hym Farao Nechao, kyng of Egipt, stiede ayens the kyng of Assiriens, to the flood Eufrates; and Josias, kyng of Juda, yede in to metyng of hym, and Josias was slayn in Magedo, whanne he hadde seyn hym.
30 Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
And `hise seruauntis baren hym deed fro Magedo, and brouyte him in to Jerusalem, and birieden hym in his sepulcre; and the puple of the lond took Joachaz, sone of Josias, and anoyntiden hym, and maden hym kyng for his fadir.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
Joachaz was of thre and twenti yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede thre monethis in Jerusalem; the name of his modir was Amychal, douyter of Jeremye of Lobna.
32 Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
And he dide yuel bifor the Lord, bi alle thingis which hise fadris hadden do.
33 Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
And Farao Nechao boond hym in Reblatha, which is in the lond of Emath, that he schulde not regne in Jerusalem; and he settide `peyne, ether raunsum, to the lond, in an hundrid talentis of siluer, and in a talent of gold.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
And Farao Nechao made kyng Eliachim, sone of Josias, for Josias, his fadir; and he turnede the name of hym Joachym; forsothe Farao took Joachaz, and ledde hym in to Egipt.
35 Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
Sotheli Joachym yaf siluer and gold to Farao, whanne he hadde comaundid to the lond bi alle yeeris, that it schulde be brouyt, bi the comaundement of Farao; and he reiside of ech man bi hise myytis bothe siluer and gold, of the puple of the lond, that he schulde yyue to Pharao Nechao.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
Joachym was of fyue and twenti yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede eleuene yeer in Jerusalem; the name of his modir was Zebida, douyter of Phadaia of Ruma.
37 Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.
And he dide yuel bifor the Lord, bi alle thingis which hise fadris hadden do.

< 2 Wafalme 23 >