< 2 Wafalme 18 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Roku trzeciego Ozeasza, syna Eli, króla Izraelskiego, królował Ezechyjasz, syn Achaza, króla Judzkiego.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
Dwadzieścia i pięć lat mu było, gdy począł królować, a dwadzieścia i dziewięć lat królował w Jeruzalemie. Imię matki jego było Abi, córka Zacharyjaszowa.
3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Daudi baba yake alivyofanya.
I czynił co było dobrego przed oczyma Pańskiemi, według wszystkiego, jako czynił Dawid, ojciec jego.
4 Akapaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, akazivunja sanamu, akakatakata nguzo za Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba Mose aliyotengeneza, kwa kuwa hadi siku hizo wana wa Israeli walikuwa wanaifukizia uvumba (ilikuwa ikiitwa Nehushtani).
On zniósł wyżyny, i skruszył bałwany, i powycinał gaje, a pokruszył węża miedzianego, którego był uczynił Mojżesz; bo aż do onych dni Izraelczycy kadzili mu, i nazwał go Nehustan.
5 Hezekia aliweka tumaini lake kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Hapakuwepo na mfalme mwingine wa kufanana naye miongoni mwa wafalme wa Yuda, kabla yake au baada yake.
W Panu Bogu Izraelskim ufał; a po nim nie był żaden podobny jemu między wszystkimi królami Judzkimi, i którzy byli przed nim.
6 Alishikamana na Bwana kwa bidii wala hakuacha kumfuata; alishika amri ambazo Bwana alikuwa amempa Mose.
Bo się trzymał Pana, nie odstępując od niego, a strzegąc przykazania jego, które był przykazał Pan Mojżeszowi.
7 Naye Bwana alikuwa pamoja naye, akafanikiwa katika kila alichokifanya. Aliasi dhidi ya mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia.
A Pan był z nim; i we wszystkiem, do czego się obrócił, szczęściło mu się. Wybił się też z mocy królowi Assyryjskiemu, i nie służył mu.
8 Kuanzia mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye ngome, aliwashinda Wafilisti, hadi kufikia Gaza na himaya yake yote.
Tenże poraził Filistyny aż do Gazy i granic jego, od wieży strażników aż do miasta obronnego.
9 Mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela kutawala Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru alikwenda kuishambulia Samaria na kuuzunguka kwa majeshi.
Roku czwartego króla Ezechyjasza, (który był rok siódmy Ozeasza, syna Eli, króla Izraelskiego) wyciągnął Salmanaser, król Assyryjski, przeciwko Samaryi, i obległ ją.
10 Baada ya miaka mitatu Waashuru wakautwaa. Kwa hiyo Samaria ulitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mfalme wa Israeli.
A wziął ją przy dokończeniu trzeciego roku; roku szóstego Ezechyjasza, (który był rok dziewiąty Ozeasza, króla Izraelskiego) wzięta jest Samaryja.
11 Mfalme wa Ashuru akawahamishia Waisraeli huko Ashuru na akawaweka Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
Tedy przeniósł król Assyryjski Izraela do Assyryi, i osadził nimi Halach i Habor u rzeki Gazan, i miasta Medskie.
12 Hili lilitokea kwa sababu hawakumtii Bwana Mungu wao, lakini walikuwa wamevunja agano lake, yale yote ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwaamuru. Hawakuzisikiliza amri wala kuzitimiza.
Przeto, iż nie posłuchali głosu Pana Boga swego, ale przestępowali przymierze jego, i tego wszystkiego, co rozkazał Mojżesz, sługa Pański, nie słuchali i nie czynili.
13 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
Potem czternastego roku króla Ezechyjasza ruszył się Sennacheryb, król Assyryjski, przeciw wszystkim miastom Judzkim obronnym, i wziął je.
14 Basi Hezekia mfalme wa Yuda akamtumia ujumbe mfalme wa Ashuru huko Lakishi akisema: “Nimefanya makosa. Ondoka katika nchi yangu, nami nitakulipa chochote unachokitaka kwangu.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia mfalme wa Yuda talanta 300 za fedha, na talanta thelathini za dhahabu.
A tak posłał Ezechyjasz, król Judzki, do króla Assyryjskiego, do Lachys, mówiąc: Zgrzeszyłem; odciągnij odemnie, cokolwiek na mię włożysz, poniosę. Tedy włożył król Assyryjski na Ezechyjasza, króla Judzkiego, dań trzy sta talentów srebra, i trzydzieści talentów złota.
15 Basi Hezekia akampa fedha yote iliyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme.
I dał Ezechyjasz wszystko srebro, które się znalazło w domu Pańskim i w skarbach domu królewskiego.
16 Wakati huu Hezekia mfalme wa Yuda akabandua dhahabu yote iliyokuwa imefunika milango na miimo ya Hekalu la Bwana, akampa mfalme wa Ashuru.
Onegoż czasu obłupił Ezechyjasz drzwi domu Pańskiego, i słupy, które samże Ezechyjasz, król Judzki, był obył, a dał je królowi Assyryjskiemu.
17 Mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wake mkuu, na afisa wake mkuu, na jemadari wa jeshi, pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Wakaja Yerusalemu na kusimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
Wszakże posłał król Assyryjski Tartana, i Rabsarysa, i Rabsacesa z Lachys do króla Ezechyjasza z wielkiem wojskiem do Jeruzalemu. Którzy wyciągnąwszy przyjechali ku Jeruzalemowi, a przyciągnąwszy przyszli i położyli się u rur sadzawki wyższej, która jest podle drogi brukowanej na polu blecharzowem.
18 Wakaagiza mfalme aitwe. Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakawaendea.
A gdy wołali na króla, wyszedł do nich Elijakim, syn Helkijaszowy, przełożony nad domem, i Sobna pisarz, i Joach syn Asafowy, kanclerz.
19 Yule jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia: “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
I rzekł do nich Rabsaces: Proszę powiedzcie Ezechyjaszowi: Tak mówi król wielki, król Assyryjski: Co to za ufność, na której się wspierasz?
20 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
Mówiłeś: (aleć to słowa daremne) Rady i mocy mam dosyć do wojny. A teraz w kimże ufasz, żeś mi się sprzeciwił?
21 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
Oto teraz spolegasz na Egipcie, jako na lasce trzcinnej, i to nałamanej, którą jeźliby się kto podpierał, tedy wnijdzie w rękę jego i przekole ją. Takić jest Farao, król Egipski, wszystkim, co w nim ufają.
22 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya katika Yerusalemu”?
A jeźli mi rzeczecie: W Panu Bogu naszym ufność mamy: azaż nie ten jest, którego zniósł Ezechyjasz wyżyny i ołtarze? i rozkazał Judzie i Jeruzalemowi, mówiąc: Przed tym ołtarzem kłaniać się będziecie w Jeruzalemie.
23 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
Przetoż teraz zaręcz się królowi Assyryjskiemu, panu memu, a dam ci dwa tysiące koni; będzieszli mógł mieć jezdnych tak wiele do dnich?
24 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
I jakoż się ty możesz oprzeć hetmanowi jednemu najmniejszemu z sług pana mego? choć pokładasz nadzieję w Egipcie dla wozów i jezdnych.
25 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza mahali hapa pasipo neno kutoka kwa Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
Nadto, czy bez woli Pańskiej przyciągnąłem przeciw temu miejscu, abym je zburzył? Pan mówi do mnie: Idź do tej ziemi, a spustosz ją.
26 Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
Tedy rzekł Elijakim, syn Helkijaszowy, i Sobna, i Joach do Rabsacesa: Proszę mów do sług twoich po syryjsku, boć rozumiemy; a nie mów z nami po żydowsku, gdzie słyszy lud, który jest na murze.
27 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
Którym odpowiedział Rabsaces: Azaż mię do pana twego, albo do ciebie przysłał Pan mój, abym te słowa mówił? Azaż nie do tych mężów, którzy siedzą na murze, aby jedli łajna swoje, i pili mocz swój z wami.
28 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
A tak stanąwszy Rabsaces wołał głosem wielkim po żydowsku, a mówiąc rzekł: Słuchajcie słów króla wielkiego, króla Assyryjskiego.
29 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa mkononi mwangu.
Tak mówi król: Niech was nie zwodzi Ezechyjasz; bo was nie będzie mógł wyrwać z ręki mojej.
30 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
A niech wam nie rozkazuje ufać Ezechyjasz w Panu, mówiąc: Pewnie nas wyrwie Pan, a nie będzie podane to miasto w ręce króla Assyryjskiego.
31 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
Nie słuchajcie Ezechyjasza. Albowiem tak mówi król Assyryjski: Uczyńcie ze mną przymierze, a wynijdźcie do mnie, a jedzcie każdy z winnicy swojej i każdy z figi swojej, i pijcie każdy wodę z studnicy swojej,
32 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya mizeituni na asali. Chagueni uzima, sio mauti! “Msimsikilize Hezekia, kwa kuwa anawapotosha asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’
Aż przyjdę a pobiorę was do ziemi podobnej ziemi waszej, do ziemi żyznej i obfitującej winem, do ziemi chleba i winnic, do ziemi drzew oliwnych, i oliwy, i miodu; i będziecie żyli, a nie pomrzecie. Nie słuchajcież Ezechyjasza; bo was zwodzi, mó wiąc: Pan was wybawi.
33 Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
Izaż mogli bogowie narodów wybawić każdy ziemię swoję, z ręki króla Assyryjskiego?
34 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
Gdzież jest bóg Emat i Arfad? gdzież jest bóg Sefarwaim, Ana i Awa? izali wyrwali Samaryję z rąk moich?
35 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
Któryż jest między wszystkimi bogi tych ziem, któryby wyrwał ziemię swoję z ręki mojej? A miałby Pan wyrwać Jeruzalem z ręki mojej?
36 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
Ale milczał lud, i nie odpowiedzieli mu słowa; bo takie było rozkazanie królewskie, mówiąc: Nie odpowiadajcie mu.
37 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
Przyszedł tedy Elijakim, syn Helkijaszowy, przełożony domu, i Sobna pisarz, i Joach, syn Asafowy, kanclerz, do Ezechyjasza, rozdarłszy szaty swe, i oznajmili mu słowa Rabsacesowe.

< 2 Wafalme 18 >