< 2 Wafalme 14 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
The second yeere of Ioash sonne of Iehoahaz King of Israel reigned Amaziah the sonne of Ioash King of Iudah.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
He was fiue and twentie yeere olde when he began to reigne, and reigned nine and twentie yeere in Ierusalem, and his mothers name was Iehoadan of Ierusalem.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
And he did vprightly in the sight of the Lord, yet not like Dauid his father, but did according to all that Ioash his father had done.
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Notwithstanding the hie places were not taken away: for as yet the people did sacrifice and burnt incense in the hie places.
5 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
And when the kingdome was confirmed in his hand, he slewe his seruants which had killed the King his father.
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
But the children of those that did slay him, he slewe not, according vnto that that is written in the booke of the Lawe of Moses, wherein the Lord commanded, saying, The fathers shall not be put to death for the children, nor the children put to death for the fathers: but euery man shall be put to death for his owne sinne.
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
He slew also of Edom in the valley of salt ten thousand, and tooke the citie of Sela by warre, and called the name thereof Ioktheel vnto this day.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
Then Amaziah sent messengers to Iehoash the sonne of Iehoahaz, sonne of Iehu King of Israel, saying, Come, let vs see one another in the face.
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
Then Iehoash the King of Israel sent to Amaziah King of Iudah, saying, The thistle that is in Lebanon, sent to the cedar that is in Lebanon, saying, Giue thy daughter to my sonne to wife: and the wilde beast that was in Lebanon, went and trode downe the thistle.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Because thou hast smitten Edom, thine heart hath made thee proud: bragge of glory, and tary at home. why doest thou prouoke to thine hurt, that thou shouldest fall, and Iudah with thee?
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
But Amaziah would not heare: therefore Iehoash King of Israel went vp: and he and Amaziah King of Iudah sawe one another in the face at Beth-shemesh which is in Iudah.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
And Iudah was put to the worse before Israel, and they fledde euery man to their tents.
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
But Iehoash King of Israel tooke Amaziah King of Iudah, the sonne of Iehoash the sonne of Ahaziah, at Beth-shemesh, and came to Ierusalem, and brake downe the wall of Ierusalem from the gate of Ephraim to the corner gate, foure hundreth cubites.
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
And he tooke all the gold and siluer, and all the vessels that were found in the house of the Lord, and in the treasures of the Kings house, and the children that were in hostage, and returned to Samaria.
15 Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Concerning the rest of the acts of Iehoash which he did and his valiant deedes, and how he fought with Amaziah King of Iudah, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Israel?
16 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Iehoash slept with his fathers, and was buried at Samaria among the Kings of Israel: and Ieroboam his sonne reigned in his stead.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
And Amaziah the sonne of Ioash King of Iudah, liued after the death of Iehoash sonne of Iehoahaz King of Israel fifteene yeere.
18 Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Concerning the rest of the actes of Amaziah, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Iudah?
19 Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
But they wrought treason against him in Ierusalem, and he fled to Lachish, but they sent after him to Lachish, and slewe him there.
20 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
And they brought him on horses, and he was buried at Ierusalem with his fathers in the citie of Dauid.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
Then all the people of Iudah tooke Azariah which was sixteene yeere olde, and made him King for his father Amaziah.
22 Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
He built Elath, and restored it to Iudah, after that the King slept with his fathers.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
In the fifteenth yeere of Amaziah the sonne of Ioash King of Iudah, was Ieroboam the sonne of Ioash made King ouer Israel in Samaria, and reigned one and fourtie yeere.
24 Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
And he did euill in the sight of the Lord: for he departed not from all the sinnes of Ieroboam the sonne of Nebat, which made Israel to sinne.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
He restored the coast of Israel, from the entring of Hamath, vnto the Sea of the wildernesse, according to the worde of the Lord God of Israel, which he spake by his seruant Ionah the sonne of Amittai the Prophet, which was of Gath Hepher.
26 Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
For the Lord saw the exceeding bitter affliction of Israel, so that there was none shutte vp, nor any left, neyther yet any that could helpe Israel.
27 Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
Yet the Lord had not decreed to put out the name of Israel from vnder the heauen: therefore he preserued them by the hand of Ieroboam the sonne of Ioash.
28 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Concerning the rest of the actes of Ieroboam, and all that he did, and his valiant deedes, and how he fought, and how he restored Damascus, and Hamath to Iudah in Israel, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Israel?
29 Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
So Ieroboam slept with his fathers, euen with the Kings of Israel, and Zachariah his sonne reigned in his steade.

< 2 Wafalme 14 >