< 2 Wakorintho 6 >

1 Kama watendakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msipokee neema ya Mungu bure.
Помагаючи ж (Йому), благаємо вас, щоб ви марно благодать Божу не приймали.
2 Kwa maana asema: “Wakati wangu uliokubalika nilikusikia, siku ya wokovu nilikusaidia.” Tazama, wakati uliokubalika ndio huu, siku ya wokovu ndiyo sasa.
(Бо глаголе: Приятного часу вислухав я тебе, і в день спасення поміг тобі. Ось тепер пора приятна, ось тепер день спасення.)
3 Hatuweki kitu cha kukwaza katika njia ya mtu yeyote, ili huduma yetu isionekane kuwa na lawama.
Ніякого нї в чому не даємо спотикання, щоб не було ганене служеннє,
4 Bali kama watumishi wa Mungu tuonyeshe kwa kila njia: katika saburi nyingi; katika dhiki, katika misiba, na katika shida;
а у всьому показуючи себе яко слуг Божих: у великому терпінню, в горю, в нуждах, в тіснотах,
5 katika kupigwa, katika kufungwa gerezani na katika ghasia; katika kazi ngumu, katika kukesha na katika kufunga;
в ранах, в темницях, в бучах, у працях, у недосипаннях, у постах,
6 katika utakatifu, katika ufahamu, katika uvumilivu, na katika utu wema; katika Roho Mtakatifu na upendo wa kweli;
в чистоті, в знанню, в довготерпінню, в добрості, в сьвятому Дусї, в любові нелицемірній,
7 katika maneno ya kweli na katika nguvu za Mungu, kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto;
в словах правди, в силї Божій, із зброєю праведности в правій і лївій,
8 katika utukufu na katika kudharauliwa; katika sifa mbaya na katika sifa nzuri; tukiwa kama wadanganyaji, lakini tukiwa wakweli;
славою і безчестєм, ганьбою і хвалою; яко дуросьвіти, та правдиві;
9 tukiwa maarufu, lakini tukihesabiwa kama tusiojulikana; tukiwa kama wanaokufa, lakini tunaishi; tukipigwa, lakini hatuuawi;
яко незнані, та познані; яко вмираючі, і ось ми живі; яко карані, та не повбивані;
10 tukiwa kama wenye huzuni, lakini siku zote tukifurahi; tukionekana maskini, lakini tukitajirisha wengi; tukiwa kama wasio na kitu, lakini tuna vitu vyote.
яко сумні, а завсїди веселі, яко вбогі, многих же збогачуючі; яко нічого немаючі, а все держучи.
11 Tumesema nanyi wazi, enyi Wakorintho na kuwafungulieni mioyo yetu wazi kabisa.
Уста наші відкрились до вас, Коринтяне, - серця, наші розпросторились.
12 Sisi hatujizuii kuwapenda, bali ninyi mmeuzuia upendo wenu kwetu.
Не стіснені ви в нас, а тїснитесь в утробах ваших.
13 Sasa nasema, kama na watoto wangu: Ninyi pia ifungueni mioyo yenu kabisa.
Такою ж нагородою (кажу вам, як дїтям) розпросторітесь і ви.
14 Msifungiwe nira pamoja na watu wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa, kwa maana pana uhusiano gani kati ya haki na uovu? Au kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?
Не ходіть у жадному ярмі з невірними, яке бо товаришуваннє праведности і беззаконня, і яка спільність сьвітла з темрявою?
15 Kuna mapatano gani kati ya Kristo na Beliari? Yeye aaminiye ana sehemu gani na yeye asiyeamini?
Яка ж згода в Христа з Велиялом? або яка часть вірному з невірним?
16 Kuna mapatano gani kati ya Hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi tu Hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu alivyosema: “Nitakaa pamoja nao na kutembea katikati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
І яка згода церкви Божої з ідолською? бо ви церква Бога живого, яко ж рече Бог: вселю ся в них, і ходити му; і буду їм Бог, а вони будуть менї люде.
17 “Kwa hiyo tokeni miongoni mwao, mkatengwe nao, asema Bwana. Msiguse kitu chochote kilicho najisi, nami nitawakaribisha.”
Тимже вийдіть із між них, і відлучіть ся, глаголе Господь, і до нечистого не приторкайтесь; і я прийму вас,
18 “Mimi nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa wanangu na binti zangu, asema Bwana Mwenyezi.”
і буду вам за отця, а ви будете менї за синів і дочок, глаголе Господь Вседержитель.

< 2 Wakorintho 6 >