< 2 Wakorintho 6 >

1 Kama watendakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msipokee neema ya Mungu bure.
And working together also we call upon [you] that ye receive not in vain the grace of God —
2 Kwa maana asema: “Wakati wangu uliokubalika nilikusikia, siku ya wokovu nilikusaidia.” Tazama, wakati uliokubalika ndio huu, siku ya wokovu ndiyo sasa.
for He saith, 'In an acceptable time I did hear thee, and in a day of salvation I did help thee, lo, now [is] a well-accepted time; lo, now, a day of salvation,' —
3 Hatuweki kitu cha kukwaza katika njia ya mtu yeyote, ili huduma yetu isionekane kuwa na lawama.
in nothing giving any cause of offence, that the ministration may be not blamed,
4 Bali kama watumishi wa Mungu tuonyeshe kwa kila njia: katika saburi nyingi; katika dhiki, katika misiba, na katika shida;
but in everything recommending ourselves as God's ministrants; in much patience, in tribulations, in necessities, in distresses,
5 katika kupigwa, katika kufungwa gerezani na katika ghasia; katika kazi ngumu, katika kukesha na katika kufunga;
in stripes, in imprisonments, in insurrections, in labours, in watchings, in fastings,
6 katika utakatifu, katika ufahamu, katika uvumilivu, na katika utu wema; katika Roho Mtakatifu na upendo wa kweli;
in pureness, in knowledge, in long-suffering, in kindness, in the Holy Spirit, in love unfeigned,
7 katika maneno ya kweli na katika nguvu za Mungu, kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto;
in the word of truth, in the power of God, through the armour of the righteousness, on the right and on the left,
8 katika utukufu na katika kudharauliwa; katika sifa mbaya na katika sifa nzuri; tukiwa kama wadanganyaji, lakini tukiwa wakweli;
through glory and dishonour, through evil report and good report, as leading astray, and true;
9 tukiwa maarufu, lakini tukihesabiwa kama tusiojulikana; tukiwa kama wanaokufa, lakini tunaishi; tukipigwa, lakini hatuuawi;
as unknown, and recognized; as dying, and lo, we live; as chastened, and not put to death;
10 tukiwa kama wenye huzuni, lakini siku zote tukifurahi; tukionekana maskini, lakini tukitajirisha wengi; tukiwa kama wasio na kitu, lakini tuna vitu vyote.
as sorrowful, and always rejoicing; as poor, and making many rich; as having nothing, and possessing all things.
11 Tumesema nanyi wazi, enyi Wakorintho na kuwafungulieni mioyo yetu wazi kabisa.
Our mouth hath been open unto you, O Corinthians, our heart hath been enlarged!
12 Sisi hatujizuii kuwapenda, bali ninyi mmeuzuia upendo wenu kwetu.
ye are not straitened in us, and ye are straitened in your [own] bowels,
13 Sasa nasema, kama na watoto wangu: Ninyi pia ifungueni mioyo yenu kabisa.
and [as] a recompense of the same kind, (as to children I say [it], ) be ye enlarged — also ye!
14 Msifungiwe nira pamoja na watu wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa, kwa maana pana uhusiano gani kati ya haki na uovu? Au kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?
Become not yoked with others — unbelievers, for what partaking [is there] to righteousness and lawlessness?
15 Kuna mapatano gani kati ya Kristo na Beliari? Yeye aaminiye ana sehemu gani na yeye asiyeamini?
and what fellowship to light with darkness? and what concord to Christ with Belial? or what part to a believer with an unbeliever?
16 Kuna mapatano gani kati ya Hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi tu Hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu alivyosema: “Nitakaa pamoja nao na kutembea katikati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
and what agreement to the sanctuary of God with idols? for ye are a sanctuary of the living God, according as God said — 'I will dwell in them, and will walk among [them], and I will be their God, and they shall be My people,
17 “Kwa hiyo tokeni miongoni mwao, mkatengwe nao, asema Bwana. Msiguse kitu chochote kilicho najisi, nami nitawakaribisha.”
wherefore, come ye forth out of the midst of them, and be separated, saith the Lord, and an unclean thing do not touch, and I — I will receive you,
18 “Mimi nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa wanangu na binti zangu, asema Bwana Mwenyezi.”
and I will be to you for a Father, and ye — ye shall be to Me for sons and daughters, saith the Lord Almighty.'

< 2 Wakorintho 6 >