< 2 Nyakati 9 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
Царица же Савска услыша имя Соломоново и прииде искусити его гаданьми во Иерусалиме с силою тяжкою зело: и велблюды носящии ароматы и злата множество и камения драгаго: и прииде к Соломону и глагола ему вся, елика беша в сердцы ея.
2 Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
И возвести ей Соломон вся словеса ея, и не прейде слово, егоже бы не возвестил ей.
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
И виде царица Савска премудрость Соломоню, и дом егоже созда,
4 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
и яди столов его, и седалища рабов его, и состояние служебников его и ризы их, и виночерпчия его и украшение их, и всесожжения, яже жряше в дому Господни, и вне себе бысть.
5 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
Рече же ко царю: истинно есть слово, еже слышах в земли моей о словесех твоих и о премудрости твоей:
6 Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
и не веровах словесем их, дондеже приидох, и видеста очи мои, и се, не возвестиша мне половины множества премудрости твоея: приложил еси ко слышанию яже слышах:
7 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
блажени мужие твои и блажени раби твои сии, иже предстоят пред тобою на всяко время и слышат премудрость твою:
8 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
да будет Господь Бог твой благословен, иже благоволи в тебе, еже дати тя на престол Свой царя Господу Богу твоему: зане возлюби Господь Бог твой Израиля, еже утвердити его во век, и постави тя над ними царя, да сотвориши суд и правду.
9 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
Даде же царю сто двадесять талант злата и ароматы многи зело и камение драгое, и не быша ароматы таковы яко сия, яже даде царица Савска царю Соломону.
10 (Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
Но и раби Хирамовы с рабы Соломоними приношаху злато Соломону драгое.
11 Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
И сотвори Соломон царь от древ певговых степени в дом Господень и в дом царев, и гусли и псалтири песней, и никогдаже видена быша в земли Иудине прежде такоая.
12 Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
Царь же Соломон даде царице Савстей вся по желанию ея, ихже просила, кроме всех яже принесе царю Соломону, и возвратися в землю свою.
13 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
Бе же вес злата приносимаго к Соломону на всяко лето шесть сот шестьдесят шесть талант злата,
14 mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
кроме мужей подданных и купцов, иже приношаху, и всех царей Аравских и властелей земли, иже вси приношаху злато и сребро царю Соломону.
15 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
Сотвори убо царь Соломон двести щитов златых тягненых, шесть сот златник чистых бяху во единем щите:
16 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
и триста щитов златых тягненых, по триста златник бяше во единем коемждо щите, и положи я царь в дому древа Ливанова.
17 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
Сотвори же царь престол от слоновых зубов велик, и позлати его златом чистым,
18 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
и шесть степений у престола позлащени златом, и мышчицы две туду и сюду над престолом седалища, и два льва стояща близ мышчцей,
19 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
и дванадесять львов стоящих тамо на шести степенех от обоих стран: и не бысть таков престол во всяцем царстве.
20 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
Вси же сосуди царя Соломона бяху златы, и вси сосуди дому дубравы Ливанския златом окружены, сребро бо во днех Соломоних ни во что вменяшеся:
21 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
зане корабль царев хождаше в Фарсис с рабы Хирамовыми, единицею в лета три прихождаше корабль от Фарсиса ко царю, полн злата и сребра и зубов слоновых и обезян.
22 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
И возвеличися Соломон паче всех царей земных богатством и мудростию.
23 Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
Вси же царие земстии желаху видети лице Соломоне и слышати премудрость его, юже даде Бог в сердце его:
24 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
и приношаху ему кийждо дары своя, сосуды сребряны и златы, и одеяния и стакту, и сладости, кони и мски, на всякое лето.
25 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
И бяху царю Соломону четыредесять тысящ кобылиц к колесницы и дванадесять тысящ конник, и постави их во градех колесничных и со царем во Иерусалиме.
26 Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
И быть вождь всех царей от реки (Евфрата) даже до земли иноплеменник и даже до предел Египетских.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
И даде царь злато и сребро во Иерусалиме яко камение, и кедры яко черничие, еже (раждается) в полях множество.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
И приводяху кони Соломону от Египта и от всея земли.
29 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
И прочая словеса Соломоня первая и последняя, се, сия писана суть в словесех Нафана пророка и в словесех Ахии Силониты и в видениих Иоиля видящаго, противу Иеровоама сына Наватова.
30 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
И царствова Соломон во Иерусалиме над всем Израилем четыредесять лет.
31 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
И успе Соломон со отцы своими, и погребоша его во граде Давида отца его. И воцарися Ровоам сын его вместо его.

< 2 Nyakati 9 >