< 2 Nyakati 35 >

1 Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Bwana katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
Et Josias célébra à Jérusalem la Pâque à l’Éternel; et on égorgea la pâque, le quatorzième jour du premier mois.
2 Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Bwana.
Et il établit les sacrificateurs dans leurs charges, et les encouragea pour le service de la maison de l’Éternel.
3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Bwana, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa huku na huko mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Bwana Mungu wenu na watu wake Israeli.
Et il dit aux lévites qui enseignaient tout Israël, [et] qui étaient saints, [consacrés] à l’Éternel: Mettez l’arche sainte dans la maison que Salomon, fils de David, roi d’Israël, a bâtie: vous n’avez pas à la porter sur l’épaule; servez maintenant l’Éternel, votre Dieu, et son peuple Israël;
4 Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Solomoni.
et préparez-vous, selon vos maisons de pères, selon vos divisions, suivant l’écrit de David, roi d’Israël, et suivant l’écrit de Salomon, son fils;
5 “Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu.
et placez-vous dans le lieu saint pour les sections des maisons de pères de vos frères, les fils du peuple, et selon les divisions des maisons de pères des lévites;
6 Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Mose.”
et égorgez la pâque, et sanctifiez-vous, et préparez [la pâque] pour vos frères, afin d’agir conformément à la parole de l’Éternel par Moïse.
7 Ndipo Yosia akawapa watu wote wana-mbuzi waliokuwepo jumla ya kondoo wapatao 30,000 kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ngʼombe 10,000, vyote hivi kutoka mali binafsi ya mfalme.
Et Josias donna aux fils du peuple du menu bétail, des agneaux et des chevreaux, au nombre de 30 000, le tout pour les pâques, pour tous ceux qui se trouvaient là, et 3 000 bœufs; cela fut [pris] sur les biens du roi.
8 Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi 2,600 na mafahali 300.
Et ses chefs donnèrent volontairement pour le peuple, pour les sacrificateurs et pour les lévites. Hilkija, et Zacharie, et Jekhiel, les princes de la maison de Dieu, donnèrent aux sacrificateurs, pour les pâques, 2 600 [têtes de menu bétail] et 300 de gros bétail.
9 Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi 5,000 na mafahali 500, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
Et Conania, et Shemahia et Nethaneël, ses frères, et Hashabia, et Jehiel, et Jozabad, chefs des lévites, donnèrent pour les lévites 5 000 [têtes de menu bétail] pour les pâques, et 500 de gros bétail.
10 Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru.
Et le service fut réglé, et les sacrificateurs se tinrent à leurs places, et les lévites dans leurs divisions, selon le commandement du roi.
11 Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi.
Et ils égorgèrent la pâque; et les sacrificateurs firent aspersion [du sang qu’ils recevaient] de leurs mains, et les lévites écorchaient [les victimes].
12 Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Bwana kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali.
Et ils mirent à part les holocaustes pour les donner aux sections des maisons de pères des fils du peuple, pour les présenter à l’Éternel, selon qu’il est écrit dans le livre de Moïse; et [ils firent] de même pour le gros bétail.
13 Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi.
Et ils firent cuire la pâque au feu, selon l’ordonnance; et les choses saintes, ils les firent cuire dans des chaudières, et des chaudrons, et des poêles, et les distribuèrent à la hâte à tous les fils du peuple.
14 Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani, wazao wa Aroni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona mpaka usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Aroni.
Et ensuite, ils préparèrent [ce qui était] pour eux et pour les sacrificateurs; car les sacrificateurs, fils d’Aaron, [furent occupés] jusqu’à la nuit à offrir les holocaustes et les graisses; et les lévites préparèrent [ce qui était] pour eux-mêmes, et pour les sacrificateurs, fils d’Aaron.
15 Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.
Et les chantres, fils d’Asaph, étaient à leur place, selon le commandement de David, et d’Asaph, et d’Héman, et de Jeduthun, le voyant du roi; et les portiers étaient à chaque porte: ils n’eurent pas à se retirer de leur service, car leurs frères, les lévites, préparaient [ce qui était] pour eux.
16 Kwa hiyo wakati ule huduma yote ya Bwana ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana kama alivyoamuru Mfalme Yosia.
Et tout le service de l’Éternel fut réglé, en ce jour-là, pour faire la Pâque, et pour offrir des holocaustes sur l’autel de l’Éternel, selon le commandement du roi Josias.
17 Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba.
Et les fils d’Israël présents, firent la Pâque en ce temps-là, et la fête des pains sans levain pendant sept jours.
18 Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi na watu wote wa Yuda na watu wa Israeli waliokuwepo huko, pamoja na watu wa Yerusalemu.
Et on n’avait point célébré en Israël de Pâque semblable depuis les jours de Samuel, le prophète; et aucun des rois d’Israël n’avait célébré une Pâque comme celle que firent Josias, et les sacrificateurs et les lévites, et tout Juda et Israël, qui s’y trouvèrent, et les habitants de Jérusalem.
19 Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.
Cette Pâque fut célébrée la dix-huitième année du règne de Josias.
20 Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye.
Après tout cela, quand Josias eut mis en état la maison, Neco, roi d’Égypte, monta pour faire la guerre à Carkemish sur l’Euphrate; et Josias sortit à sa rencontre.
21 Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”
Et [Neco] lui envoya des messagers, disant: Qu’y a-t-il entre moi et toi, roi de Juda? Ce n’est pas contre toi que je viens aujourd’hui, mais contre la maison avec laquelle je suis en guerre, et Dieu m’a dit de me hâter. Désiste-toi de [t’opposer à] Dieu, qui est avec moi, afin qu’il ne te détruise pas.
22 Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.
Et Josias ne se détourna pas de lui, mais il se déguisa pour combattre contre lui; et il n’écouta pas les paroles de Neco, [qui venaient] de la bouche de Dieu. Et il vint pour combattre dans la vallée de Meguiddo.
23 Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.”
Et les archers tirèrent sur le roi Josias; et le roi dit à ses serviteurs: Ôtez-moi d’ici, car je suis grièvement blessé.
24 Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.
Et ses serviteurs l’ôtèrent du char, et le mirent sur un second char qu’il avait, et le conduisirent à Jérusalem. Et il mourut; et on l’enterra dans les sépulcres de ses pères; et tout Juda et Jérusalem menèrent deuil sur Josias.
25 Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.
Et Jérémie fit des lamentations sur Josias; et tous les chanteurs et toutes les chanteuses ont parlé de Josias dans leurs lamentations jusqu’à aujourd’hui; et on l’a établi comme ordonnance pour Israël. Et, voici, cela est écrit dans les Lamentations.
26 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana:
Et le reste des actes de Josias, et ses actions pieuses, conformément à ce qui est écrit dans la loi de l’Éternel,
27 matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
et ses actes, les premiers et les derniers, voici, ils sont écrits dans le livre des rois d’Israël et de Juda.

< 2 Nyakati 35 >