< 2 Nyakati 32 >

1 Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake.
Après ces événements et ces preuves de zèle, Sennachérib, roi d’Assyrie, vint envahir Juda, assiégea les villes fortes et prétendit les forcer pour s’en emparer.
2 Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu,
Ezéchias, voyant que Sennachérib était venu avec l’intention d’attaquer Jérusalem,
3 akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia.
consulta ses chefs et ses héros sur l’idée de boucher les sources d’eau qui se trouvaient en dehors de la ville, et ils l’appuyèrent.
4 Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?”
Alors ils se rassemblèrent en grand nombre et bouchèrent toutes les sources, ainsi que le torrent qui coulait dans le pays, en disant: "Pourquoi les rois d’Assyrie trouveraient-ils à leur arrivée quantité d’eau?"
5 Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.
Il s’enhardit et rebâtit toutes les brèches de la muraille; il suréleva les tours et l’autre muraille extérieure; il fortifia le Millo dans la cité de David et fabriqua un grand nombre d’armes de trait et des boucliers.
6 Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya:
Il établit des chefs militaires à la tête du peuple, les assembla autour de lui sur la place à la porte de la ville et les encouragea en ces termes:
7 “Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye.
"Soyez forts et courageux, n’ayez crainte et ne vous laissez point effrayer par le roi d’Assyrie et toute la foule qui raccompagne, car il y a avec nous quelqu’un de plus grand qu’avec lui.
8 Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.
Avec lui est un bras de chair; avec nous est l’Eternel, notre Dieu, pour nous assister et combattre nos combats", et le peuple s’en rapporta aux paroles d’Ezéchias, roi de Juda.
9 Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:
Après cela Sennachérib, roi d’Assyrie, envoya ses serviteurs à Jérusalem, tandis qu’il était lui-même devant Lakhich avec toutes ses forces, vers Ezéchias, roi de Juda, et vers tous ceux de Juda qui se trouvaient à Jérusalem pour leur dire:
10 “Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi?
"Ainsi parle Sennachérib, roi d’Assyrie: En quoi mettez-vous votre confiance pour rester ainsi bloqués dans Jérusalem?
11 Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu.
Ne voyez-vous pas qu’Ezéchias vous abuse pour vous livrer à la mort par la famine et par la soif, quand il vous dit: L’Eternel, notre Dieu, nous sauvera de la main du roi d’Assyrie?
12 Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?
N’Est-ce pas lui, Ezéchias, qui a fait disparaître ses hauts lieux et ses autels et qui a parlé en ces termes à Juda et à Jérusalem: Devant un seul autel vous vous prosternerez et ferez fumer l’encens?
13 “Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu?
Ne savez-vous pas ce que j’ai fait, moi et mes pères, à tous les peuples des diverses contrées? Est-ce que les dieux des nations de ces contrées ont jamais pu soustraire leur pays à mon pouvoir?
14 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu?
De tous les dieux de ces nations qu’ont anéanties mes pères, quel est celui qui a pu soustraire son peuple à mon pouvoir? Et votre Dieu pourrait vous arracher à ma domination!
15 Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”
Et maintenant, ne vous laissez pas abuser par Ezéchias ni séduire ainsi, ne croyez pas en lui, car aucun dieu d’aucune nation et royaume ne pourra soustraire son peuple à ma domination et à celle de mes pères, à plus forte raison votre Dieu ne pourra-t-il vous soustraire à mon pouvoir."
16 Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia.
Ses serviteurs continuèrent à déblatérer contre le Seigneur Dieu et contre Ezéchias, son serviteur.
17 Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.”
Il avait écrit aussi des libelles injurieux pour l’Eternel, Dieu d’Israël, et s’exprimait sur lui en ces termes: "Tels les dieux des contrées qui n’ont pu soustraire leur peuple à mon pouvoir, ainsi le Dieu d’Ezéchias ne soustraira point son peuple à mon pouvoir."
18 Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji.
Ils s’adressaient à haute voix en judéen au peuple de Jérusalem qui était sur le rempart pour les effrayer et les troubler afin de s’emparer de la ville.
19 Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.
Ils parlaient du Dieu de Jérusalem comme des dieux des nations de la terre, œuvre des mains de l’homme.
20 Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili.
Alors le roi Ezéchias et le prophète Isaïe, fils d’Amoç, se mirent à prier à ce sujet et ils implorèrent le Ciel.
21 Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.
L’Eternel envoya un ange, qui extermina tous les guerriers, princes et chefs, dans le camp du roi d’Assyrie, lequel s’en revint, plein de confusion, dans son pays. Il entra dans le temple de son dieu et là, il tomba sous le glaive de sa propre progéniture.
22 Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande.
C’Est ainsi que l’Eternel sauva Ezéchias et les habitants de Jérusalem de la main de Sennachérib, roi d’Assyrie, et de la main de tous leurs ennemis et les protégea tout alentour.
23 Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.
Puis, beaucoup apportèrent une offrande à l’Eternel à Jérusalem et des présents à Ezéchias, roi de Juda; et il fut élevé après cela aux yeux de tous les peuples.
24 Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara.
En ce temps-là Ezéchias fut atteint d’une maladie mortelle. Il implora le Seigneur, qui lui parla et lui accorda un prodige.
25 Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu.
Mais Ezéchias n’agit pas comme il aurait dû en retour de cette faveur, car son cœur s’enorgueillit, et la colère divine fut excitée contre lui et contre Juda et Jérusalem.
26 Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.
Mais Ezéchias s’humilia dans son cœur orgueilleux, lui et les habitants de Jérusalem, et la colère de l’Eternel ne les atteignit pas du temps d’Ezéchias.
27 Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani.
Ezéchias eut des richesses et des honneurs en grande abondance; il se fit des trésors pour l’argent, l’or et les pierres précieuses, pour les aromates, les boucliers et tous les objets de prix,
28 Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi.
des magasins pour les récoltes de blé, pour le moût et l’huile, des étables pour tous les animaux domestiques et des troupeaux pour les étables.
29 Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.
Il se bâtit des villes, s’acquit du menu et du gros bétail en quantité, car Dieu lui avait donné des richesses très considérables.
30 Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya.
Ce fut Ezéchias qui boucha l’issue supérieure des eaux du Ghihôn et les dirigea par en bas du côté occidental vers la cité de David, et Ezéchias réussit dans toutes ses entreprises.
31 Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.
Pourtant, dans l’affaire des conseillers des princes de Babylone qui lui avaient envoyé une ambassade pour s’informer du prodige qui avait eu lieu dans le pays, Dieu l’abandonna afin de le mettre à l’épreuve et connaître tous les sentiments de son cœur.
32 Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
Pour les autres faits concernant Ezéchias et ses mérites, tout cela est consigné dans les prophéties d’Isaïe, fils d’Amoç et dans le livre des rois de Juda et d’Israël.
33 Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.
Ezéchias s’endormit avec ses pères; on l’ensevelit sur la montée des tombeaux de la famille de David, et des honneurs lui furent rendus à sa mort par tout Juda et par les habitants de Jérusalem. Il eut pour successeur son fils Manassé.

< 2 Nyakati 32 >