< 2 Nyakati 27 >

1 Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Jotham was twenty-five years old when he began to reign; and he reigned sixteen years in Jerusalem: and his mother's name was Jerushah the daughter of Zadok.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
He did that which was right in the eyes of Jehovah, according to all that his father Uzziah had done: however he did not enter into Jehovah's temple. The people still did corruptly.
3 Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
He built the Upper Gate of the house of Jehovah, and he carried out considerable work on the wall of Ophel.
4 Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
Moreover he built cities in the hill country of Judah, and in the forests he built fortresses and towers.
5 Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
He fought also with the king of the people of Ammon, and prevailed against them. The people of Ammon gave him the same year one hundred talents of silver, and ten thousand measures of wheat, and ten thousand of barley. The people of Ammon gave that much to him in the second year also, and in the third.
6 Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
So Jotham became mighty, because he ordered his ways before Jehovah his God.
7 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
Now the rest of the acts of Jotham, and all his wars, and his ways, look, they are written in the book of the kings of Israel and Judah.
8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
He was five and twenty years old when he began to reign, and reigned sixteen years in Jerusalem.
9 Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jotham slept with his fathers, and they buried him in the City of David: and Ahaz his son reigned in his place.

< 2 Nyakati 27 >