< 2 Nyakati 24 >

1 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka arobaini. Mama yake aliitwa Sibia aliyekuwa ametoka Beer-Sheba.
Joas was of seuene yeer, whanne he bigan to regne, and he regnyde fourti yeer in Jerusalem; the name of his modir was Sebia of Bersabee.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ya Yehoyada kuhani.
And he dide that, that was good bifor the Lord, in alle the daies of Joiada, the preest.
3 Yehoyada akamwoza wake wawili, akazaa watoto wa kiume na wa kike.
Sotheli and Joas took twei wyues, of whyche he gendride sones and douytris.
4 Baada ya muda, Yoashi akaamua kukarabati Hekalu la Bwana.
After whiche thingis it pleside Joas to reparele the hows of the Lord.
5 Akawaita pamoja makuhani na Walawi akawaambia, “Nendeni katika miji ya Yuda mkakusanye fedha wanazopaswa kulipa kila mwaka kutoka kwa Israeli wote, ili kukarabati Hekalu la Mungu wenu. Fanyeni hivyo sasa.” Lakini Walawi hawakufanya upesi.
And he gaderide togidere preestis and dekenes, and seide to hem, Go ye out to the citees of Juda, and gadere ye of al Israel money, to the reparelyng of the temple of `youre Lord God, bi ech yeer; and do ye this hiyyngli.
6 Kwa hiyo mfalme akamwita Yehoyada kuhani mkuu na kumwambia, “Kwa nini hukuwaambia Walawi walete kutoka Yuda na Yerusalemu kodi iliyowekwa na Mose mtumishi wa Bwana pamoja na kusanyiko la Israeli kwa ajili ya Hema ya Ushuhuda?”
Certis the dekenes diden necgligentli. And the kyng clepide Joiada, the prince, and seide to hym, Whi was it not charge to thee, to constreyne the dekenes to brynge yn money of Juda and of Jerusalem, which money was ordeyned of Moises, the seruaunt of `the Lord, that al the multitude of Israel schulde brynge it in to the tabernacle of witnessyng?
7 Kwa kuwa wana wa yule mwanamke mwovu Athalia, walikuwa wamevunja na kuingia katika Hekalu la Mungu, nao wakawa wamevitumia hata vile vitu vilivyowekwa wakfu kwa Bwana kwa mabaali.
For the worste Athalia, and hir sones, distrieden the hows of God; and of alle thingis, that weren halewid to the temple of the Lord, thei ourneden the temple of Baalym.
8 Kwa amri ya mfalme, likatengenezwa kasha, nalo likawekwa nje kwenye lango la Hekalu la Bwana.
Therfor the kyng comaundide, and thei maden an arke, and settiden it bisidis the yate of the Lord with out forth.
9 Tangazo likatolewa katika Yuda na Yerusalemu kwamba inapasa wamletee Bwana kodi ile ambayo Mose, mtumishi wa Bwana alikuwa amewaagiza Israeli huko jangwani.
And it was prechid in Juda and Jerusalem, that ech man schulde brynge to the Lord the prijs, which Moyses, the seruaunt of God, ordeynede on al Israel, in deseert.
10 Maafisa wote na watu wote wakaleta michango yao kwa furaha, wakaweka kwenye kasha mpaka likajaa.
And alle the princes and al the puple weren glad, and thei entriden, and brouyten, and senten in to the arke of the Lord, so that it was fillid.
11 Ikawa kila wakati kasha lilipoletwa ndani na Walawi kwa maafisa wa mfalme na kuona kwamba kuna kiasi kikubwa cha fedha, mwandishi wa mfalme na afisa wa kuhani mkuu walikuwa wanakuja na kumimina, kisha kulirudisha mahali pake. Walifanya hivi mara kwa mara, nao wakakusanya fedha nyingi sana.
And whanne it was tyme, that thei schulden bere the arke bifor the kyng bi the hondis of dekenes, for thei sien myche money, the clerk of the kyng entride, and he whom the firste preest hadde ordeynede, and thei schedden out the money, that was in the arke; sotheli thei baren ayen the arke to `his place. And so thei diden bi alle daies, and money with out noumbre was gaderid togidere;
12 Mfalme na Yehoyada wakawapa wale watu waliofanya kazi iliyotakiwa katika Hekalu la Bwana. Wakawaajiri waashi na maseremala ili kutengeneza Hekalu la Bwana, pia wafanyakazi za chuma na shaba ili kukarabati Hekalu la Bwana.
which the kyng and Joiada yauen to hem that weren souereyns of the werkis of the hows of the Lord. And thei hiriden therof kitteris of stonys, and crafti men of alle werkis, that thei schulden reparele the hows of the Lord; also thei hiriden smythis of yrun, and of bras, that that thing schulde be vndurset, that bigan to falle.
13 Watu walioshughulika na kazi walikuwa wenye bidii, nayo kazi ya kukarabati ikaendelea vizuri mikononi mwao. Wakalitengeneza upya Hekalu la Bwana likarudi katika hali yake ya awali na kuliimarisha.
Thei that wrouyten diden craftili, and the crasyng of the wallis was stoppid bi the hondis of hem; and thei reisiden the hows of the Lord in to the formere staat, and maden it to stonde stidfastli.
14 Walipokamilisha kazi hiyo ya kukarabati, wakaleta fedha zilizobaki wakampa mfalme na Yehoyada, nao kwa hizo wakatengeneza vyombo kwa ajili ya Hekalu la Bwana: Vyombo kwa ajili ya huduma na kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia mabakuli na vitu vingine vya dhahabu na fedha. Wakati wote Yehoyada alipokuwa hai, sadaka za kuteketezwa zilitolewa wakati wote katika Hekalu la Bwana.
And whanne thei hadden fillid alle werkis, thei brouyten bifor the kyng and Joiada the tother part of the money, of which money vessels weren maad in to the seruyce of the temple, and to brent sacrifices; also viols, and othere vessels of gold and of siluer `weren maad therof. And brent sacrifices weren offrid in the hows of the Lord contynueli, in alle the daies of Joiada.
15 Basi Yehoyada alikuwa mzee aliyeshiba siku wakati alipofariki. Alikufa akiwa na umri wa miaka 130.
Forsothe Joiada ful of daies wexide eld, and he was deed, whanne he was of an hundrid yeer and thritti;
16 Wakamzika pamoja na wafalme katika Mji wa Daudi, kwa sababu ya mema aliyokuwa ametenda katika Israeli kwa ajili ya Mungu na Hekalu lake.
and thei birieden hym in the citee of Dauid with kyngis; for he hadde do good with Israel, and with his hows.
17 Baada ya kifo cha Yehoyada, wakuu wa Yuda walikuja kumpa mfalme heshima, naye akawasikiliza.
But aftir that Joiada diede, the princes of Juda entriden, and worschipiden the kyng, which was flaterid with her seruices, and assentide to hem.
18 Wakaacha Hekalu la Bwana, Mungu wa baba zao, wakaabudu nguzo za maashera na sanamu. Kwa sababu ya hatia yao, hasira ya Mungu ikawajia Yuda na Yerusalemu.
And thei forsoken the temple of the Lord God of her fadris, and seruyden idols in wodis, and grauen ymagis; and the ire of the Lord was maad ayens Juda and Jerusalem for this synne.
19 Ingawa Bwana aliwatuma manabii wawarudishe watu kwake na ingawa waliwaonya, hawakuwasikiliza.
And he sente to hem profetis, that thei schulen turne ayen to the Lord; whiche profetis witnessynge thei nolden here.
20 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya Zekaria mwana wa Yehoyada kuhani. Akasimama mbele ya watu akasema, “Hili ndilo asemalo Mungu, ‘Kwa nini mnakataa kuzitii amri za Bwana? Hamtafanikiwa kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi.’”
Therfor the Spirit of the Lord clothide Zacharie, the preest, the sone of Joiada; and he stood in the siyt of the puple, and seide to hem, The Lord seith these thingis, Whi breken ye the comaundement of the Lord, `which thing schal not profite to you, and ye han forsake the Lord, that he schulde forsake you?
21 Lakini wakafanya shauri baya juu yake na kwa amri ya mfalme wakampiga kwa mawe mpaka akafa katika ukumbi wa Hekalu la Bwana.
Whiche weren gaderide togidere ayens hym, and senten stonys, bi comaundement `of the kyng, in the large place of the hows of the Lord.
22 Mfalme Yoashi hakukumbuka wema aliotendewa na Yehoyada baba yake Zekaria ila alimuua mwanawe, ambaye alisema wakati akiwa amelala akingojea kufa, “Bwana na alione hili na alipize kisasi.”
And kyng Joas hadde not mynde on the merci which Joiada, the fadir of Zacharie, hadde doon with hym; but he killide the sone of Joiada. And whanne Zacharie diede, he seide, The Lord se, and seke.
23 Mwishoni mwa ule mwaka, jeshi la Waaramu likaja dhidi ya Yoashi, likavamia Yuda na Yerusalemu na kuwaua viongozi wote wa watu. Wakapeleka nyara zao zote kwa mfalme wao huko Dameski.
And whanne a yeer was turned aboute, `ether endid, the oost of Sirie stiede ayens Joas, and it cam in to Juda and in to Jerusalem, and it killide alle the princes of the puple; and thei senten al the prey to the kyng, to Damask.
24 Ingawa jeshi la Waaramu lilikuwa limekuja na watu wachache tu, Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa kuliko lao. Kwa sababu Yuda walikuwa wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, hukumu ilitekelezwa juu ya Yoashi.
And certeyn, whanne a ful litle noumbre of men of Sirie was comun, the Lord bitook in her hondis a multitude with out noumbre, for thei hadden forsake the Lord God of her fadris. Also thei vsiden schameful domes in Joas;
25 Waaramu walipoondoka, walimwacha Yoashi akiwa mgonjwa sana. Maafisa wake wakafanya hila dhidi yake kwa sababu alikuwa amemuua mwana wa Kuhani Yehoyada, nao wakamuulia kitandani mwake. Hivyo akafa na wakamzika katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
and thei yeden awei, and leften hym in grete sorewis. Sotheli hise seruauntis risiden ayens hym, in to veniaunce of the blood of the sone of Joiada, preest; and killiden hym in his bed, and he was deed. And thei birieden hym in the citee of Dauid, but not in the sepulcris of kyngis.
26 Wale waliofanya hila mbaya dhidi yake walikuwa Zabadi, mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, Yehozabadi, mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabu.
Forsothe Sabath, the sone of Semath of Amon, and Josabeth, the sone of Semarith of Moab, settiden tresouns to hym.
27 Kwa habari za wanawe, unabii mwingi kumhusu na kumbukumbu za kutengenezwa upya kwa Hekalu la Mungu, zimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme. Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Sotheli hise sones, and the summe of money that was gaderid vndur hym, and the reparelyng of the hows of God, ben writun diligentli in the book of Kyngis.

< 2 Nyakati 24 >