< 2 Nyakati 24 >

1 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka arobaini. Mama yake aliitwa Sibia aliyekuwa ametoka Beer-Sheba.
Joash was seven years old when he began to reign; and he reigned forty years in Jerusalem: and his mother's name was Zibiah, of Beersheba.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ya Yehoyada kuhani.
Joash did that which was right in the eyes of Jehovah all the days of Jehoiada the priest.
3 Yehoyada akamwoza wake wawili, akazaa watoto wa kiume na wa kike.
Jehoiada took for him two wives; and he became the father of sons and daughters.
4 Baada ya muda, Yoashi akaamua kukarabati Hekalu la Bwana.
It happened after this, that Joash intended to restore the house of Jehovah.
5 Akawaita pamoja makuhani na Walawi akawaambia, “Nendeni katika miji ya Yuda mkakusanye fedha wanazopaswa kulipa kila mwaka kutoka kwa Israeli wote, ili kukarabati Hekalu la Mungu wenu. Fanyeni hivyo sasa.” Lakini Walawi hawakufanya upesi.
He gathered together the priests and the Levites, and said to them, "Go out to the cities of Judah, and gather money to repair the house of your God from all Israel from year to year. See that you expedite this matter." However the Levites did not do it right away.
6 Kwa hiyo mfalme akamwita Yehoyada kuhani mkuu na kumwambia, “Kwa nini hukuwaambia Walawi walete kutoka Yuda na Yerusalemu kodi iliyowekwa na Mose mtumishi wa Bwana pamoja na kusanyiko la Israeli kwa ajili ya Hema ya Ushuhuda?”
The king called for Jehoiada the chief, and said to him, "Why haven't you required of the Levites to bring in the tax of Moses the servant of Jehovah, and of the assembly of Israel, out of Judah and out of Jerusalem, for the tent of the testimony?"
7 Kwa kuwa wana wa yule mwanamke mwovu Athalia, walikuwa wamevunja na kuingia katika Hekalu la Mungu, nao wakawa wamevitumia hata vile vitu vilivyowekwa wakfu kwa Bwana kwa mabaali.
For the sons of Athaliah, that wicked woman, had broken up God's house; and they also gave all the dedicated things of the house of Jehovah to the Baals.
8 Kwa amri ya mfalme, likatengenezwa kasha, nalo likawekwa nje kwenye lango la Hekalu la Bwana.
So the king commanded, and they made a chest, and set it outside at the gate of the house of Jehovah.
9 Tangazo likatolewa katika Yuda na Yerusalemu kwamba inapasa wamletee Bwana kodi ile ambayo Mose, mtumishi wa Bwana alikuwa amewaagiza Israeli huko jangwani.
They made a proclamation through Judah and Jerusalem, to bring in for Jehovah the tax that Moses the servant of God laid on Israel in the wilderness.
10 Maafisa wote na watu wote wakaleta michango yao kwa furaha, wakaweka kwenye kasha mpaka likajaa.
And all the leaders and all the people rejoiced, and brought in, and threw it into the chest, until it was full.
11 Ikawa kila wakati kasha lilipoletwa ndani na Walawi kwa maafisa wa mfalme na kuona kwamba kuna kiasi kikubwa cha fedha, mwandishi wa mfalme na afisa wa kuhani mkuu walikuwa wanakuja na kumimina, kisha kulirudisha mahali pake. Walifanya hivi mara kwa mara, nao wakakusanya fedha nyingi sana.
It was so, that whenever the chest was brought to the king's officers by the hand of the Levites, and when they saw that there was much money, the king's scribe and the chief priest's officer came and emptied the chest, and took it, and carried it to its place again. Thus they did day by day, and gathered money in abundance.
12 Mfalme na Yehoyada wakawapa wale watu waliofanya kazi iliyotakiwa katika Hekalu la Bwana. Wakawaajiri waashi na maseremala ili kutengeneza Hekalu la Bwana, pia wafanyakazi za chuma na shaba ili kukarabati Hekalu la Bwana.
The king and Jehoiada gave it to such as did the work of the service of the house of Jehovah; and they hired masons and carpenters to restore the house of Jehovah, and also such as worked iron and bronze to repair the house of Jehovah.
13 Watu walioshughulika na kazi walikuwa wenye bidii, nayo kazi ya kukarabati ikaendelea vizuri mikononi mwao. Wakalitengeneza upya Hekalu la Bwana likarudi katika hali yake ya awali na kuliimarisha.
So the workmen worked, and the work of repairing went forward in their hands, and they set up God's house in its state, and strengthened it.
14 Walipokamilisha kazi hiyo ya kukarabati, wakaleta fedha zilizobaki wakampa mfalme na Yehoyada, nao kwa hizo wakatengeneza vyombo kwa ajili ya Hekalu la Bwana: Vyombo kwa ajili ya huduma na kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia mabakuli na vitu vingine vya dhahabu na fedha. Wakati wote Yehoyada alipokuwa hai, sadaka za kuteketezwa zilitolewa wakati wote katika Hekalu la Bwana.
When they had made an end, they brought the rest of the money before the king and Jehoiada, of which were made vessels for the house of Jehovah, even vessels with which to minister and to offer, and spoons, and vessels of gold and silver. They offered burnt offerings in the house of Jehovah continually all the days of Jehoiada.
15 Basi Yehoyada alikuwa mzee aliyeshiba siku wakati alipofariki. Alikufa akiwa na umri wa miaka 130.
But Jehoiada grew old and was full of days, and he died; one hundred thirty years old was he when he died.
16 Wakamzika pamoja na wafalme katika Mji wa Daudi, kwa sababu ya mema aliyokuwa ametenda katika Israeli kwa ajili ya Mungu na Hekalu lake.
They buried him in the City of David among the kings, because he had done good in Israel, and toward God and his house.
17 Baada ya kifo cha Yehoyada, wakuu wa Yuda walikuja kumpa mfalme heshima, naye akawasikiliza.
Now after the death of Jehoiada the leaders of Judah came and paid homage to the king. And the king listened to them.
18 Wakaacha Hekalu la Bwana, Mungu wa baba zao, wakaabudu nguzo za maashera na sanamu. Kwa sababu ya hatia yao, hasira ya Mungu ikawajia Yuda na Yerusalemu.
They forsook the house of Jehovah, the God of their fathers, and served the Asherim and the idols: and wrath came on Judah and Jerusalem for this their guiltiness.
19 Ingawa Bwana aliwatuma manabii wawarudishe watu kwake na ingawa waliwaonya, hawakuwasikiliza.
Yet he sent prophets to them, to bring them again to Jehovah; and they testified against them: but they would not give ear.
20 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya Zekaria mwana wa Yehoyada kuhani. Akasimama mbele ya watu akasema, “Hili ndilo asemalo Mungu, ‘Kwa nini mnakataa kuzitii amri za Bwana? Hamtafanikiwa kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi.’”
The Spirit of God came on Zechariah the son of Jehoiada the priest; and he stood above the people, and said to them, "Thus says God, 'Why do you disobey the commandments of Jehovah, so that you can't prosper? Because you have forsaken Jehovah, he has also forsaken you.'"
21 Lakini wakafanya shauri baya juu yake na kwa amri ya mfalme wakampiga kwa mawe mpaka akafa katika ukumbi wa Hekalu la Bwana.
They conspired against him, and stoned him with stones at the commandment of the king in the court of the house of Jehovah.
22 Mfalme Yoashi hakukumbuka wema aliotendewa na Yehoyada baba yake Zekaria ila alimuua mwanawe, ambaye alisema wakati akiwa amelala akingojea kufa, “Bwana na alione hili na alipize kisasi.”
Thus Joash the king did not remember the kindness which Jehoiada his father had done to him, but killed his son. When he died, he said, "May Jehovah look at it, and repay it."
23 Mwishoni mwa ule mwaka, jeshi la Waaramu likaja dhidi ya Yoashi, likavamia Yuda na Yerusalemu na kuwaua viongozi wote wa watu. Wakapeleka nyara zao zote kwa mfalme wao huko Dameski.
It happened at the end of the year, that the army of the Arameans came up against him. And they came to Judah and Jerusalem, and destroyed all the leaders of the people from among the people, and sent all their spoil to the king in Damascus.
24 Ingawa jeshi la Waaramu lilikuwa limekuja na watu wachache tu, Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa kuliko lao. Kwa sababu Yuda walikuwa wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, hukumu ilitekelezwa juu ya Yoashi.
For the army of the Arameans came with a small company of men; and Jehovah delivered a very great army into their hand, because they had forsaken Jehovah, the God of their fathers. So they executed judgment on Joash.
25 Waaramu walipoondoka, walimwacha Yoashi akiwa mgonjwa sana. Maafisa wake wakafanya hila dhidi yake kwa sababu alikuwa amemuua mwana wa Kuhani Yehoyada, nao wakamuulia kitandani mwake. Hivyo akafa na wakamzika katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
When they were departed for him (for they left him very sick), his own servants conspired against him for the blood of the son of Jehoiada the priest, and killed him on his bed, and he died; and they buried him in the City of David, but they did not bury him in the tombs of the kings.
26 Wale waliofanya hila mbaya dhidi yake walikuwa Zabadi, mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, Yehozabadi, mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabu.
These are those who conspired against him: Zabad the son of Shimeath the Ammonitess, and Jehozabad the son of Shimrith the Moabitess.
27 Kwa habari za wanawe, unabii mwingi kumhusu na kumbukumbu za kutengenezwa upya kwa Hekalu la Mungu, zimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme. Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Now concerning his sons, and the many oracles against him, and the rebuilding of God's house, look, they are written in the commentary of the book of the kings. Amaziah his son reigned in his place.

< 2 Nyakati 24 >