< 2 Nyakati 17 >

1 Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
Jehoshaphat his son reigned in his place, and strengthened himself against Israel.
2 Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
He placed forces in all the fortified cities of Judah, and set garrisons in the land of Judah, and in the cities of Ephraim, which Asa his father had taken.
3 Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
Jehovah was with Jehoshaphat, because he walked in the first ways of his father, and did not seek the Baals,
4 bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
but sought to the God of his father, and walked in his commandments, and not after the doings of Israel.
5 Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
Therefore Jehovah established the kingdom in his hand; and all Judah brought to Jehoshaphat tribute; and he had riches and honor in abundance.
6 Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
His heart was lifted up in the ways of Jehovah: and furthermore he took away the high places and the Asherim out of Judah.
7 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
Also in the third year of his reign he sent his officials, even Ben Hail, and Obadiah, and Zechariah, and Nethanel, and Micaiah, to teach in the cities of Judah;
8 Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
and with them the Levites, even Shemaiah, and Nethaniah, and Zebadiah, and Asahel, and Shemiramoth, and Jehonathan, and Adonijah, and Tobijah, and Tobadonijah, the Levites; and with them Elishama and Jehoram, the priests.
9 Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
They taught in Judah, having the scroll of the law of Jehovah with them; and they went about throughout all the cities of Judah, and taught among the people.
10 Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
The fear of Jehovah fell on all the kingdoms of the lands that were around Judah, so that they made no war against Jehoshaphat.
11 Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
Some of the Philistines brought Jehoshaphat presents, and silver for tribute; the Arabians also brought him flocks, seven thousand and seven hundred rams, and seven thousand and seven hundred male goats.
12 Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
Jehoshaphat grew great exceedingly; and he built in Judah fortresses and cities of store.
13 na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
He had many works in the cities of Judah; and men of war, mighty men of valor, in Jerusalem.
14 Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
This was the numbering of them according to their fathers' houses: Of Judah, the captains of thousands: Adnah the captain, and with him mighty men of valor three hundred thousand;
15 aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
and next to him Jehohanan the captain, and with him two hundred eighty thousand;
16 aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
and next to him Amasiah the son of Zikri, who willingly offered himself to Jehovah; and with him two hundred thousand mighty men of valor.
17 Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
Of Benjamin: Eliada a mighty man of valor, and with him two hundred thousand armed with bow and shield;
18 aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
and next to him Jehozabad and with him one hundred eighty thousand ready prepared for war.
19 Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.
These were those who waited on the king, besides those whom the king put in the fortified cities throughout all Judah.

< 2 Nyakati 17 >