< 1 Samweli 9 >

1 Kulikuwako Mbenyamini mmoja, mtu maarufu, ambaye aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Serori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia wa Benyamini.
Torej tam je bil mož iz Benjamina, katerega ime je bilo Kiš, sin Abiéla, sinú Cerórja, sinú Behoráta, sinú Afíaha, Benjaminovec, mogočen človek moči.
2 Alikuwa na mwana aliyeitwa Sauli, kijana anayevutia sana, hakuwepo aliyelingana naye miongoni mwa Waisraeli, alikuwa mrefu kuliko wengine wote.
Imel je sina, čigar ime je bilo Savel, izbranega in čednega mladeniča in med Izraelovimi otroki ni bilo čednejše osebe kakor on. Od njegovih ramen in navzgor je bil višji kakor katerikoli izmed ljudstva.
3 Basi punda wa Kishi baba yake Sauli walipotea, naye Kishi akamwambia mwanawe Sauli, “Mchukue mmoja wa watumishi mwende pamoja naye kuwatafuta punda.”
Oslice Savlovega očeta Kiša so se izgubile. Kiš je rekel svojemu sinu Savlu: »Vzemi torej s seboj enega izmed služabnikov in vstani, pojdi iskat oslice.«
4 Hivyo akapita katika nchi ya vilima ya Efraimu na katika eneo la Shalisha, lakini hawakuwapata. Wakaendelea katika sehemu ya Shaalimu, lakini punda hawakuwepo huko. Kisha wakapita katika nchi ya Benyamini, lakini hawakuwapata.
Prečkal je goro Efrájim in šel skozi deželo Šalíša, toda nista jih našla. Potem sta šla skozi deželo Šaalím in tam jih ni bilo. Šel je skozi deželo Benjaminovcev, toda nista jih našla.
5 Walipofika sehemu ya Sufu, Sauli akamwambia mtumishi aliyekuwa pamoja naye, “Njoo, sisi na turudi, au baba yangu ataacha kufikiria juu ya punda na kuanza kufadhaika kutuhusu sisi.”
In ko sta prišla do dežele Cuf, je Savel rekel svojemu služabniku, ki je bil z njim: »Pridi in se vrniva, da ne bi moj oče prenehal skrbeti za oslice in bi mislil na naju.«
6 Lakini mtumishi akajibu, “Tazama, katika mji huu yupo mtu wa Mungu, anayeheshimiwa sana na kila kitu asemacho hutokea kweli. Sasa na twende huko. Huenda atatuambia twende njia ipi.”
Rekel mu je: »Glej torej, v tem mestu je Božji mož in ta je častitljiv mož. Vse, kar reče, se zagotovo zgodi. Pojdiva sedaj tja, morda nama on lahko pokaže pot, po kateri naj greva.«
7 Sauli akamwambia mtumishi wake, “Kama tukienda, tutampa nini huyo mtu? Chakula kimekwisha kwenye mifuko yetu. Hatuna zawadi ya kumpelekea huyo mtu wa Mungu. Je tuna nini?”
Potem je Savel rekel svojemu služabniku: »Toda glej, če greva, kaj bova prinesla možu? Kajti kruh v najinih posodah je pošel in ni darila, da bi ga prinesla Božjemu možu. Kaj imava?«
8 Mtumishi akamjibu Sauli tena, akasema, “Tazama, nina fedha robo shekeli. Hiyo nitampa huyo mtu wa Mungu ili aweze kutuambia twende kwa njia ipi.”
Služabnik je ponovno odgovoril Savlu in rekel: »Glej, tukaj pri roki imam četrtinko šekla srebra. To bom dal Božjemu možu, da nama pove najino pot.«
9 (Zamani katika Israeli, kama mtu alikwenda kuuliza neno kwa Mungu, angalisema, “Njoo na twende kwa mwonaji,” kwa sababu nabii wa sasa alikuwa akiitwa mwonaji.)
(Poprej je v Izraelu mož, ko je šel, da poizveduje od Boga, govoril tako: »Pridite in pojdimo k vidcu, « kajti kdor je sedaj imenovan prerok, je bil poprej imenovan videc.)
10 Sauli akamwambia mtumishi wake, “Vyema, njoo na twende.” Basi wakaenda mjini alipokuwepo huyo mtu wa Mungu.
Potem je Savel rekel svojemu služabniku: »Dobro rečeno. Pridi, pojdiva.« Tako sta šla v mesto, kjer je bil Božji mož.
11 Walipokuwa wakipanda mlima kwenda mjini, wakakutana na baadhi ya wasichana wanakuja kuchota maji, nao wakawauliza, “Je, mwonaji yuko?”
In ko sta šla gor, po hribu do mesta, sta našla mladenke, ki so prihajale ven, da zajamejo vodo in rekla sta jim: »Je tukaj videc?«
12 Wakajibu, “Yuko, yu mbele yenu amewatangulia, sasa fanyeni haraka, ndiyo tu amekuja mjini kwetu leo, kwa kuwa watu wana dhabihu huko mahali pa juu.
Odgovorile so jima in rekle: »Je, glejta, pred vama je. Sedaj pohitita, kajti danes je prišel v mesto, kajti danes je klavna daritev ljudstva na visokem kraju.
13 Mara tu mwingiapo mjini, mtamkuta kabla hajapanda kwenda mahali pa juu kula. Watu hawataanza kula mpaka atakapofika kwa sababu ni lazima kwanza yeye abariki dhabihu, ndipo wale walioalikwa watakapokula. Pandeni sasa, mtamkuta kwa wakati huu.”
Takoj ko prideta v mesto, ga bosta nemudoma našla, preden gre gor na visok kraj, da jé, kajti ljudstvo ne bo jedlo, dokler on ne pride, ker on blagoslovi klavno daritev in potem tisti, ki so povabljeni, jedo. Sedaj torej pojdita gor, kajti približno ta čas ga bosta našla.«
14 Wakapanda mjini, nao walipokuwa wakiingia mjini, tazama, Samweli alikuwa akija kuelekea walikokwenda mahali pa juu.
Šla sta gor v mesto in ko sta prišla v mesto, glej, je Samuel prihajal ven proti njima, da bi šel gor na visok kraj.
15 Basi siku moja kabla Sauli hajaja, Bwana alikuwa amemfunulia Samweli jambo hili:
Torej Gospod je Samuelu na uho povedal, dan poprej, preden je Savel prišel, rekoč:
16 “Kesho wakati kama huu nitakupelekea mtu kutoka nchi ya Benyamini. Umtie mafuta awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli, ndiye atakayewakomboa watu wangu na mkono wa Wafilisti. Nimewaangalia watu wangu, kwa kuwa kilio chao kimenifikia.”
»Jutri okrog tega časa ti bom poslal moža iz Benjaminove dežele in ti ga boš mazilil, da bo poveljnik nad mojim ljudstvom Izraelom, da bo lahko rešil moje ljudstvo iz roke Filistejcev, kajti jaz sem pogledal na svoje ljudstvo, ker je njihov krik prišel k meni.«
17 Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekuambia habari zake, kwamba yeye atawatawala watu wangu.”
Ko je Samuel zagledal Savla, mu je Gospod rekel: »Glej mož, o katerem sem ti govoril! Ta isti bo kraljeval nad mojim ljudstvom.«
18 Sauli akamkaribia Samweli langoni na kumuuliza, “Tafadhali, je, waweza kuniambia mahali nyumba ya mwonaji ilipo?”
Potem se je Savel približal k Samuelu v velikih vratih in rekel: »Povej mi, prosim te, kje je vidčeva hiša.«
19 Samweli akamjibu Sauli, “Mimi ndiye mwonaji, panda utangulie mbele yangu mpaka mahali pa juu, kwa kuwa leo itakupasa kula pamoja nami na asubuhi nitakuruhusu uende na nitakuambia yale yote yaliyo moyoni mwako.
Samuel je odgovoril Savlu in rekel: »Jaz sem videc. Pojdi gor pred menoj na visok kraj, kajti danes boš jedel z menoj, jutri pa te bom pustil oditi in povedal ti bom vse, kar je v tvojem srcu.
20 Kuhusu wale punda uliowapoteza siku tatu zilizopita, usifadhaike kwa habari yao; wamepatikana. Ni kwa nani ambaye shauku yote ya Israeli imeelekea, kama si kwako na jamaa yote ya baba yako?”
Glede oslic, ki so bile izgubljene pred tremi dnevi, ne naravnaj svojih misli nanje, kajti najdene so. Na kom je vse hrepenenje Izraela? Ali ni na tebi in na vsej hiši tvojega očeta?«
21 Sauli akajibu, “Je, mimi si Mbenyamini, kutoka kabila dogo kuliko yote ya Israeli, nao ukoo wangu si ndio mdogo kuliko koo zote za kabila la Benyamini? Kwa nini uniambie jambo la namna hiyo?”
Savel je odgovoril in rekel: » Ali nisem Benjaminovec, od najmanjšega izmed Izraelovih rodov? In moja družina najmanjša izmed vseh družin Benjaminovega rodu? Zakaj mi potem tako govoriš?«
22 Kisha Samweli akamleta Sauli na mtumishi wake ndani ukumbini na kuwaketisha mahali pa heshima zaidi miongoni mwa wale waliokuwa wamealikwa; jumla yao walikuwa kama watu thelathini.
Samuel je vzel Savla in njegovega služabnika ter ju privedel v dvorano in ju primoral sesti na najvišje mesto med tistimi, ki so bili povabljeni, katerih je bilo približno trideset oseb.
23 Samweli akamwambia mpishi, “Leta ile sehemu ya nyama niliyokupa, ile niliyokuambia iweke kando.”
Samuel je rekel kuharju: »Prinesi delež, ki sem ti ga dal, od katerega sem ti rekel: ›Postavi to poleg sebe.‹«
24 Hivyo mpishi akachukua mguu pamoja na kile kilichokuwa juu yake akaiweka mbele ya Sauli. Samweli akasema, “Hiki ndicho ambacho kimewekwa kwa ajili yako. Ule, kwa sababu kilitengwa kwa ajili yako kwa tukio hili, tangu niliposema, ‘Nimewaalika wageni.’” Naye Sauli akala pamoja na Samweli siku ile.
Kuhar je vzel pleče in tisto, kar je bilo na njem in to postavil pred Savla. Samuel je rekel: »Glej to, kar je preostalo! Postavi to predse in jej, kajti za ta čas je bilo prihranjeno zate, odkar sem rekel: ›Povabil sem ljudstvo.‹« Tako je Savel tisti dan jedel s Samuelom.
25 Baada ya kushuka kutoka mahali pa juu na kufika mjini, Samweli alizungumza na Sauli juu ya dari ya nyumba yake.
Ko sta prišla dol iz visokega kraja v mesto, se je Samuel s Savlom posvetoval na vrhu hiše.
26 Walipoamka mapema alfajiri, Samweli akamwita Sauli darini, akamwambia, “Jiandae, nami nitakuaga uende zako.” Sauli alipokuwa tayari yeye na Samweli wakatoka nje pamoja.
Zgodaj so vstali in pripetilo se je ob svitanju dneva, da je Samuel poklical Savla na vrhu hiše, rekoč: »Vstani, da te lahko odpošljem.« Savel je vstal in odšla sta ven, oba izmed njiju, on in Samuel.
27 Hata walipokuwa wakiteremka kuelekea mwisho wa mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi atangulie mbele yetu.” Naye mtumishi akafanya hivyo. “Lakini subiri hapa kwa kitambo kidogo, ili nipate kukupa ujumbe kutoka kwa Mungu.”
In ko sta se spuščala dol, do konca mesta, je Samuel rekel Savlu: »Zapovej služabniku, da gre naprej pred nama (in ta je šel naprej), toda ti malce postoj, da ti lahko pokažem besedo od Boga.«

< 1 Samweli 9 >