< 1 Samweli 8 >

1 Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli.
Et Samuel devint vieux, et il institua ses fils juges d'Israël.
2 Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba.
Voici les noms de ces fils: le premier-né s'appelait Joël, le second Abia; ils jugeaient en Bersabée.
3 Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.
Mais ses fils ne marchèrent pas en ses voies; ils en furent détournés par l'intérêt; ils acceptèrent des présents et ils firent dévier la justice.
4 Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama.
En conséquence, les fils d'Israël se rassemblèrent; ils allèrent trouver Samuel en Armathem,
5 Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”
Et ils lui dirent: Écoute, tu es devenu vieux, et tes fils ne marchent pas en tes voies; donne-nous donc un roi comme en ont les autres nations, afin qu'il nous juge.
6 Lakini wao waliposema, “Tupe mfalme wa kutuongoza,” hili lilimchukiza Samweli, hivyo akamwomba Bwana.
Cette parole parut mauvaise à Samuel, lorsqu'ils dirent: Donne-nous un roi, afin qu'il nous juge; et Samuel pria le Seigneur.
7 Naye Bwana akamwambia: “Sikiliza yale yote watu wanakuambia. Si wewe ambaye wamekukataa, bali wamenikataa mimi kuwa mfalme wao.
Or, le Seigneur dit à Samuel: Écoute la voix du peuple, fais comme ils te diront; ce n'est point toi, c'est moi qu'ils ont méprisé et dont ils ne veulent pas pour régner sur eux.
8 Kama vile walivyofanya tangu siku nilipowapandisha kutoka Misri mpaka siku hii ya leo; wakiniacha mimi na kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokufanyia wewe.
C'est ce qu'ils ont toujours fait à mon égard depuis le jour où je les ai tirés de l'Égypte jusqu'à ce moment: ils m'ont abandonné, et ils ont servi d'autres dieux; ils te traitent de même maintenant.
9 Sasa wasikilize, lakini waonye kwa makini na uwafahamishe yale watakayotendewa na mfalme atakayewatawala.”
Obéis donc à leur voix; seulement prends-les à témoin, et prends-les à témoin pour leur faire connaître les droits du roi qui règnera sur eux.
10 Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakiomba wapewe mfalme maneno yote ya Bwana.
Et Samuel répéta toutes les paroles du Seigneur au peuple qui lui demandait un roi.
11 Akasema, “Hivi ndivyo atakavyowatendea mfalme atakayewatawala. Atawachukua wana wenu na kuwafanya watumike kwa magari yake ya vita na farasi, nao watakimbia mbele ya magari yake.
Il leur dit: Voici quels seront les droits du roi qui régnera sur vous: Il prendra vos fils, et il les placera sur ses chars de guerre ou parmi ses cavaliers; il les fera courir devant ses chars.
12 Baadhi yao atawaweka kuwa majemadari wa jeshi wa maelfu na majemadari wa jeshi wa hamsini, wengine kulima mashamba yake na kuvuna mavuno yake, pia na wengine kutengeneza silaha za vita na vifaa kwa ajili ya magari yake.
Il s'en fera des centeniers et des chefs de mille hommes; il leur fera faire sa moisson et sa vendange; il leur fera fabriquer des armes de guerre, et les pièces diverses de ses chariots.
13 Atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi na waokaji.
Il prendra vos filles pour préparer ses parfums, cuire son pain, et faire sa cuisine.
14 Atayachukua mashamba yenu yaliyo mazuri, mashamba ya mizabibu na mashamba yenu ya mizeituni na kuwapa watumishi wake.
Il prendra vos champs, vos vignes, vos meilleurs oliviers, pour les donner à ses serviteurs.
15 Ataichukua sehemu ya kumi ya nafaka yenu na ya zabibu zenu na kuwapa maafisa wake na watumishi wake.
Il prendra la dîme de vos grains et de votre vendange, pour la donner à ses eunuques et à ses esclaves.
16 Atawachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, na ngʼombe wenu walio wazuri sana na punda kwa matumizi yake mwenyewe.
Il prendra vos serviteurs, vos servantes, vos bœufs et vos ânes; il prendra la dîme de tous les fruits de vos travaux.
17 Atachukua sehemu ya kumi ya makundi yenu ya kondoo na mbuzi, na ninyi wenyewe mtakuwa watumwa wake.
Il prendra la dîme de votre bétail, et vous serez ses esclaves.
18 Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye Bwana hatawajibu.”
Et, ce jour-là, vous crierez à cause du roi que vous vous serez choisi; et, ce jour-là, le Seigneur ne vous écoutera point, parce que c'est vous-mêmes qui aurez voulu ce roi pour vous.
19 Lakini watu wakakataa kumsikiliza Samweli wakasema, “Hapana! Tunataka mfalme wa kututawala.
Mais le peuple ne voulut pas écouter Samuel, et il dit: Nullement, mais nous aurons un roi,
20 Kisha tutakuwa kama mataifa mengine yote, tukiwa na mfalme wa kutuongoza na kwenda mbele yetu na kutupigania vita vyetu.”
Nous serons comme toutes les nations; notre roi nous jugera, il marchera à notre tête et il dirigera nos guerres.
21 Samweli aliposikia yote watu waliyosema, akarudia kuyasema mbele za Bwana.
Et Samuel écouta tous les discours du peuple, et il les transmit au Seigneur.
22 Bwana akamjibu, “Wasikilize na uwape mfalme.” Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, “Kila mmoja arudi mjini kwake.”
Et le Seigneur dit à Samuel: Obéis-leur, et donne-leur un roi. Alors, Samuel dit aux fils d'Israël: Que chacun s'en retourne en sa ville.

< 1 Samweli 8 >