< 1 Samweli 8 >

1 Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli.
It happened, when Samuel was old, that he made his sons judges over Israel.
2 Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba.
Now the name of his firstborn was Joel; and the name of his second, Abijah: they were judges in Beersheba.
3 Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.
His sons did not walk in his ways, but turned aside toward dishonest gain, and took bribes, and perverted justice.
4 Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama.
Then all the elders of Israel gathered themselves together, and came to Samuel to Ramah;
5 Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”
and they said to him, "Look, you are old, and your sons do not walk in your ways: now make us a king to judge us like all the nations."
6 Lakini wao waliposema, “Tupe mfalme wa kutuongoza,” hili lilimchukiza Samweli, hivyo akamwomba Bwana.
But the thing displeased Samuel, when they said, "Give us a king to judge us." Samuel prayed to Jehovah.
7 Naye Bwana akamwambia: “Sikiliza yale yote watu wanakuambia. Si wewe ambaye wamekukataa, bali wamenikataa mimi kuwa mfalme wao.
Jehovah said to Samuel, "Listen to the voice of the people in all that they tell you; for they have not rejected you, but they have rejected me, that I should not be king over them.
8 Kama vile walivyofanya tangu siku nilipowapandisha kutoka Misri mpaka siku hii ya leo; wakiniacha mimi na kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokufanyia wewe.
According to all the works which they have done to me since the day that I brought them up out of Egypt even to this day, in that they have forsaken me, and served other gods, so do they also to you.
9 Sasa wasikilize, lakini waonye kwa makini na uwafahamishe yale watakayotendewa na mfalme atakayewatawala.”
Now therefore listen to their voice: however you shall protest solemnly to them, and shall show them the way of the king who shall reign over them."
10 Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakiomba wapewe mfalme maneno yote ya Bwana.
Samuel told all the words of Jehovah to the people who asked of him a king.
11 Akasema, “Hivi ndivyo atakavyowatendea mfalme atakayewatawala. Atawachukua wana wenu na kuwafanya watumike kwa magari yake ya vita na farasi, nao watakimbia mbele ya magari yake.
He said, "This will be the way of the king who shall reign over you: he will take your sons, and appoint them to him, for his chariots, and to be his horsemen; and they shall run before his chariots.
12 Baadhi yao atawaweka kuwa majemadari wa jeshi wa maelfu na majemadari wa jeshi wa hamsini, wengine kulima mashamba yake na kuvuna mavuno yake, pia na wengine kutengeneza silaha za vita na vifaa kwa ajili ya magari yake.
And he will appoint for himself commanders of thousands, and commanders of fifties; and he will assign some to plow his ground, and to reap his harvest, and gather his vintage, and to make his implements of war, and the equipment of his chariots.
13 Atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi na waokaji.
He will take your daughters to be perfumers, and to be cooks, and to be bakers.
14 Atayachukua mashamba yenu yaliyo mazuri, mashamba ya mizabibu na mashamba yenu ya mizeituni na kuwapa watumishi wake.
He will take your fields, and your vineyards, and your olive groves, even their best, and give them to his servants.
15 Ataichukua sehemu ya kumi ya nafaka yenu na ya zabibu zenu na kuwapa maafisa wake na watumishi wake.
He will take the tenth of your seed, and of your vineyards, and give to his officers, and to his servants.
16 Atawachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, na ngʼombe wenu walio wazuri sana na punda kwa matumizi yake mwenyewe.
He will take your male servants, and your female servants, and your best cattle, and your donkeys, and put them to his work.
17 Atachukua sehemu ya kumi ya makundi yenu ya kondoo na mbuzi, na ninyi wenyewe mtakuwa watumwa wake.
He will take the tenth of your flocks: and you shall be his servants.
18 Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye Bwana hatawajibu.”
You shall cry out in that day because of your king whom you shall have chosen for yourselves, and Jehovah will not answer you in that day."
19 Lakini watu wakakataa kumsikiliza Samweli wakasema, “Hapana! Tunataka mfalme wa kututawala.
But the people refused to listen to the voice of Samuel; and they said, "No; but we will have a king over us,
20 Kisha tutakuwa kama mataifa mengine yote, tukiwa na mfalme wa kutuongoza na kwenda mbele yetu na kutupigania vita vyetu.”
that we also may be like all the nations, and that our king may judge us, and go out before us, and fight our battles."
21 Samweli aliposikia yote watu waliyosema, akarudia kuyasema mbele za Bwana.
Samuel heard all the words of the people, and he repeated them in the hearing of Jehovah.
22 Bwana akamjibu, “Wasikilize na uwape mfalme.” Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, “Kila mmoja arudi mjini kwake.”
Jehovah said to Samuel, "Listen to their voice, and make them a king." Samuel said to the men of Israel, "Every man go to his city."

< 1 Samweli 8 >