< 1 Samweli 5 >

1 Baada ya Wafilisti kuteka Sanduku la Mungu, walilichukua kutoka Ebenezeri mpaka Ashdodi.
Now, the Philistines, having taken the ark of God, —brought it in from Eben-ezer, unto Ashdod.
2 Kisha wakaliingiza lile Sanduku ndani ya hekalu la Dagoni na kuliweka kando ya huyo Dagoni.
And, when the Philistines took the ark of God, they brought it into the house of Dagon, —and placed it by the side of Dagon.
3 Watu wa Ashdodi walipoamka asubuhi na mapema kesho yake, kumbe, wakamkuta Dagoni ameanguka chini kifudifudi mbele ya Sanduku la Bwana! Wakamwinua Dagoni na kumrudisha mahali pake.
And, when they of Ashdod rose early on the morrow and entered into the house of Dagon, they looked and lo! Dagon, was lying prostrate on his face to the earth, before the ark of Yahweh, —so they took Dagon and restored him to his place.
4 Lakini asubuhi iliyofuata, walipoamka kumbe, walimkuta huyo Dagoni ameanguka chini kifudifudi mbele ya Sanduku la Bwana! Kichwa chake na mikono vilikuwa vimevunjwa navyo vimelala kizingitini, ni kiwiliwili chake tu kilichokuwa kimebaki.
And, when they rose up early in the morning of the morrow, lo! Dagon, was lying prostrate on his face to the earth, before the ark of Yahweh—and, the head of Dagon, and both the palms of his hands, had been cut off against the threshold, only, Dagon himself, was left to him.
5 Ndiyo sababu mpaka leo makuhani wa Dagoni wala wengine waingiao katika hekalu la Dagoni huko Ashdodi hawakanyagi kizingiti.
For this cause, do not the priests of Dagon, nor any that enter into the house of Dagon, tread upon the threshold of Dagon, in Ashdod, —until this day.
6 Mkono wa Bwana ulikuwa mzito juu ya watu wa Ashdodi na vijiji jirani, akaleta uharibifu juu yao na kuwatesa kwa majipu.
Then was the hand of Yahweh heavy against them of Ashdod, and he astounded them, —and smote with tumours Ashdod and her bounds.
7 Watu wa Ashdodi walipoona kile kilichokuwa kikitokea, wakasema, “Sanduku la Mungu wa Israeli kamwe lisikae hapa pamoja na sisi, kwa sababu mkono wake ni mzito juu yetu na juu ya Dagoni mungu wetu.”
And, when the men of Ashdod saw that, so, it was, then kept they saying, Let not the ark of the God of Israel abide with us, for, hard, is his hand upon us, and upon Dagon our god.
8 Basi wakawaita watawala wote wa Wafilisti pamoja na kuwauliza, “Tutafanya nini na hili Sanduku la Mungu wa Israeli?” Wakajibu, “Sanduku la Mungu wa Israeli na liende Gathi.” Basi wakalihamisha Sanduku la Mungu wa Israeli.
So they sent and gathered together all the lords of the Philistines unto them, and said—What shall we do with the ark of the God of Israel? And they said: To Gath, let the ark of the God of Israel go round. So they took round the ark of the God of Israel.
9 Lakini baada ya kulihamisha, mkono wa Bwana ulikuwa dhidi ya huo mji wa Gathi, akiuweka katika fadhaa kuu. Mungu akawatesa watu wa huo mji, vijana kwa wazee, kwa kuwaletea majipu.
And so it was, after they had taken it round, then was the hand of Yahweh against the city, with an exceeding great consternation, and he smote the men of the city, from the least, even unto the greatest, —and they brake out with tumours.
10 Basi wakapeleka Sanduku la Mungu Ekroni. Wakati Sanduku la Mungu lilipokuwa linaingia Ekroni, watu wa Ekroni walilia wakisema “Wamelileta Sanduku la Mungu wa Israeli kwetu ili kutuua sisi na watu wetu.”
Then sent they the ark of God to Ekron, —and so it was, when the ark of God entered Ekron, that the Ekronites made outcry, saying—They have brought round unto me the ark of the God of Israel, to slay me, and my people!
11 Basi wakawaita watawala wote wa Wafilisti pamoja na kusema, “Liondoeni Sanduku la Mungu wa Israeli na lirudishwe mahali pake, la sivyo litatuua sisi na watu wetu.” Kwa kuwa kifo kilikuwa kimeujaza mji hofu; kwani mkono wa Mungu ulikuwa mzito sana juu yake.
So they sent and gathered together all the lords of the Philistines, and said—Send away the ark of the God of Israel, and restore it to its own place, that it slay not me, and my people. For there had come a deadly consternation, throughout all the city, heavy exceedingly, was the hand of God there.
12 Wale ambao hawakufa walipatwa na majipu, na kilio cha mji kilikwenda juu hadi mbinguni.
And, the men who died not, were smitten with the tumours, —so the cry of the city for help, ascended the heavens.

< 1 Samweli 5 >