< 1 Samweli 30 >

1 Daudi na watu wake wakafika Siklagi siku ya tatu. Basi Waamaleki walikuwa wamevamia Negebu na Siklagi. Wakawa wameshambulia mji wa Siklagi na kuuteketeza kwa moto,
Three days later, when David and his men arrived at Ziklag, [they discovered that] men of the Amalek people-group had raided Ziklag and [towns in] the southern part of Judah. They had destroyed Ziklag and burned down all the buildings.
2 nao wakawa wamewachukua mateka wanawake pamoja na wote waliokuwamo humo, vijana na wazee. Hawakuua yeyote, bali waliwachukua wakaenda zao.
They had captured the women [and the children] and everyone else, and had taken them away. But they had not killed anyone.
3 Daudi na watu wake walipofika Siklagi, wakakuta mji umeangamizwa kwa moto na wake zao pamoja na wana wao na binti zao wamechukuliwa mateka.
When David and his men came to Ziklag, they saw that the town had been burned, and that their wives and sons and daughters had been captured and taken away.
4 Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.
David and his men cried loudly, until [they were so weak that] they could not cry [any more].
5 Wake wawili wa Daudi walikuwa wametekwa: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
David’s two wives, Ahinoam and Abigail, had also been taken away.
6 Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe. Kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni kwa sababu ya wanawe na binti zake. Lakini Daudi akajitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
David’s men were threatening to [kill him by] throwing stones at him, because they were very angry because their sons and daughters [had been taken away]. David was very distressed, but Yahweh his God gave him strength.
7 Kisha Daudi akamwambia kuhani Abiathari mwana wa Ahimeleki, “Niletee kisibau.” Abiathari akamletea,
David [did not know what to do, so he] said to Abiathar the priest, “Bring to me the sacred vest.” So Abiathar brought it,
8 naye Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nifuatie kundi hili la wavamizi? Je, nitawapata?” Bwana akajibu, “Wafuatie. Hakika utawapata na utafanikiwa kuwaokoa.”
and David asked Yahweh, “Should I [and my men] pursue the men [who took our families]? Will we [be able to] catch up to them?” Yahweh answered [by means of the stones in Abiathar’s sacred pouch], “Yes, pursue them. You will catch up to them, and you will be able to rescue [your families].”
9 Daudi pamoja na watu wake 600 wakafika kwenye Bonde la Besori, mahali ambapo wengine waliachwa nyuma,
So David and the 600 men who were with him left, and they came to the Besor Ravine. Some of his men stayed there [with some of their supplies].
10 kwa kuwa watu 200 walikuwa wamechoka sana kuweza kuvuka hilo bonde. Lakini Daudi pamoja na watu 400 wakaendelea kufuatia.
David and 400 men continued to pursue [the men who captured their families]. The other 200 men stayed there at the ravine, because they were so exhausted that they could not cross the ravine.
11 Wakamkuta Mmisri katika shamba fulani, nao wakamleta kwa Daudi. Wakampa huyo Mmisri maji ya kunywa na chakula;
[As David and the 400 men were going], they saw a man from Egypt in a field; so they took him to David. They gave the man some water to drink and some food to eat.
12 kipande cha andazi la tini na andazi la zabibu zilizokaushwa. Akala naye akapata nguvu, kwa kuwa hakuwa amekula chakula chochote wala kunywa maji kwa siku tatu usiku na mchana.
They also gave him a piece of fig cake and two clusters/packs of raisins. The man had not had anything to eat or drink for three days and nights, but [after he ate and drank] he felt refreshed.
13 Daudi akamuuliza, “Wewe ni wa nani, na umetoka wapi?” Akajibu, “Mimi ni Mmisri, mtumwa wa Mwamaleki. Bwana wangu alinitelekeza nilipougua siku tatu zilizopita.
David asked him, “Who is your master? And where do you come from?” He replied, “I am from Egypt. I am a slave of a man from the Amalek people-group. Three days ago my master left me here, because I was sick [and I was not able to go with them].
14 Tulivamia Negebu ya Wakerethi, na nchi ya Yuda, na Negebu ya Kalebu. Nasi tulichoma moto Siklagi.”
We had raided the southern part of Judah where the Kereth people-group live, and some other towns in Judah, and the area south [of Hebron city] where the descendants of Caleb live. We also burned Ziklag [town].”
15 Daudi akamuuliza, “Je, unaweza kuniongoza kufikia kundi hili la uvamizi?” Akajibu, “Niapie mbele ya Mungu kwamba hutaniua wala kunikabidhi mikononi mwa bwana wangu, nami nitakupeleka hadi waliko.”
David asked him, “Can you lead us to this group of raiders?” He replied, “Yes, [I will do that] if you ask God to listen while you promise that you will not kill me or give me back to my master. If you promise that, I will take you to them.”
16 Akamwongoza Daudi mpaka mahali walipokuwa, nao walikuwa wametawanyika eneo lote, wakila, wakinywa na wakifanya karamu kwa sababu ya nyara nyingi walizochukua kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka Yuda.
[David agreed to do that, ] so the man from Egypt led David [and his men] to where the men from the Amalek people-group were. Those men were lying on the ground, eating and drinking and celebrating because of having captured many things from the Philistia and Judah areas.
17 Daudi akapigana nao kuanzia machweo ya jua hadi kesho yake jioni, na hakuna yeyote miongoni mwao aliyetoroka, isipokuwa vijana wanaume 400 waliopanda ngamia na kutoroka.
David [and his men] fought against them from sunset that day until the evening of the following day. Four hundred of them escaped and rode away on camels, but none of the others escaped.
18 Daudi akarudisha kila kitu Waamaleki walikuwa wamechukua, pamoja na wake zake wawili.
David rescued his two wives, and he and his men got back everything else that the men of the Amalek people-group had taken.
19 Hakuna chochote kilichopotea: kijana au mzee, mvulana au msichana, nyara au kitu kingine chochote walichokuwa wamechukua. Daudi akarudisha kila kitu.
Nothing was missing. They took all their people back [to Ziklag]—young people and old people, [their wives], their sons and their daughters. They also recovered all the other things that the men of the Amalek people-group had taken from Ziklag.
20 Akachukua makundi yote ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, nao watu wake wakawaswaga wanyama hao mbele ya wanyama wengine wa kufugwa, wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
They took with them the sheep and cattle that had been captured, and his men caused those animals to go in front of them, saying, “These are animals that we captured in the battle; they belong to David!”
21 Kisha Daudi akafika kwa wale watu 200 waliokuwa wamechoka sana kumfuata na ambao waliachwa nyuma kwenye Bonde la Besori. Wakatoka kwenda kumlaki Daudi na wale watu aliokuwa nao. Daudi na watu wake walipowakaribia, akawasalimu.
David and his men got back to where the other 200 men were waiting, the men who did not go with David because they were very exhausted. They had stayed at Besor Ravine. [When they saw David and his men coming], they went out to greet them. And David [greeted them and] said to them, “I hope that things are going well with you!”
22 Lakini watu wote waovu na wakorofi miongoni mwa wafuasi wa Daudi wakasema, “Kwa sababu hawakwenda pamoja nasi, hatutagawana nao nyara tulizorudisha. Lakini, kila mtu aweza kuchukua mkewe na watoto wake na kuondoka.”
But some of the men who had gone with David, men who were evil and troublemakers, said, “These 200 men did not go with us. So we should not give to them any of the things that we recovered/captured. Each of them should take only his wife and children and go [back to their homes].”
23 Daudi akajibu, “La hasha, ndugu zangu, kamwe hamwezi kufanya hivyo kwa kile ambacho Bwana ametupatia. Yeye ametulinda na kuweka mikononi mwetu majeshi yale yaliyokuja kupigana dhidi yetu.
David replied, “No, my fellow Israelis, it would not be right to divide up like that the things that Yahweh has allowed us to capture. Yahweh has protected us and enabled us to defeat the enemies who attacked our town.
24 Ni nani atasikiliza yale mnayosema? Fungu la mtu aliyekaa na vyombo litakuwa sawa na la yule aliyekwenda vitani. Wote watashiriki sawa.”
(Who will pay attention to you if you say things like that?/No one will pay attention to you if you say things like that.) [RHQ] The men who stayed here with our supplies will get the same amount that the men who went into the battle will get. They will all receive the same amount.”
25 Daudi akafanya hili liwe amri na agizo kwa Israeli kutoka siku ile hata leo.
David made that to be a law [DOU] for the Israeli people, and that is still a law in Israel.
26 Daudi alipofika Siklagi, akatuma baadhi ya nyara kwa wazee wa Yuda, waliokuwa rafiki zake, akasema, “Tazama, hapa kuna zawadi kwa ajili yenu kutoka nyara za adui za Bwana.”
When David [and all the others] arrived in Ziklag, David sent to his friends who were leaders in Judah some of the things that they had captured from the Amalek people-group. He said to them, “Here is a present for you. These are things that we took from Yahweh’s enemies.”
27 Akazituma kwa wale waliokuwa Betheli, Ramoth-Negebu na Yatiri;
[Here is a list of the cities and towns to whose leaders David sent gifts: ] Bethel, Ramoth in the southern part of Judah, Jattir,
28 kwa wale walioko Aroeri, Sifmothi, Eshtemoa
Aroer, Siphmoth, Eshtemoa,
29 na Rakali; kwa wale waliokuwa katika miji ya Wayerameeli na ya Wakeni;
Racal, the cities where the descendants of Jehrameel lived and the cities where the Ken people-group lived,
30 na kwa wale walioko Horma, Bori-Ashani, Athaki,
Hormah, Bor-Ashan, Athach,
31 na kwa wakazi wa Hebroni; na kwa wale waliokuwa mahali pengine pote ambako Daudi na watu wake walitembelea.
Hebron, and all the other places where David and his men had gone [when they were hiding from Saul].

< 1 Samweli 30 >