< 1 Samweli 28 >

1 Siku zile Wafilisti wakakusanya majeshi yao ili kupigana vita dhidi ya Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Lazima ujue kuwa wewe pamoja na watu wako mtafuatana nami kwenda vitani.”
It happened in those days, that the Philistines gathered their armies together for warfare, to fight with Israel. Achish said to David, "Know assuredly that you are to go out with me to battle, you and your men."
2 Daudi akasema, “Ndipo wewe mwenyewe utakapojionea jambo ambalo mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamjibu Daudi, “Vyema sana, mimi nitakufanya uwe mlinzi wangu daima.”
David said to Achish, "Therefore you shall know what your servant will do." Achish said to David, "therefore I will make you my bodyguard for ever."
3 Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, nao Israeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika kwenye mji wake mwenyewe huko Rama. Sauli alikuwa amewafukuza waaguzi na wachawi.
Now Samuel was dead, and all Israel had lamented him, and buried him in Ramah, even in his own city. Saul had removed the mediums, and spiritists, from the land.
4 Wafilisti wakakusanyika na kupiga kambi yao huko Shunemu, naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao huko Gilboa.
The Philistines gathered themselves together, and came and camped in Shunem: and Saul gathered all Israel together, and they camped in Gilboa.
5 Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, akaogopa; moyo wake ukajawa na hofu kuu.
When Saul saw the army of the Philistines, he was afraid, and his heart trembled greatly.
6 Ndipo Sauli akauliza ushauri kwa Bwana, lakini Bwana hakumjibu kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa njia ya manabii.
When Saul inquired of Jehovah, Jehovah did not answer him, neither by dreams, nor by Urim, nor by prophets.
7 Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwaguzi ili nimwendee, nipate kuuliza kwake.” Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.”
Then Saul said to his servants, "Find for me a woman who is a medium, that I may go to her and inquire of her." His servants said to him, "Look, there is a woman who is a medium at Endor."
8 Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie kwa uaguzi, unipandishie yule nitakayekutajia.”
Saul disguised himself, and put on other clothing, and went, he and two men with him, and they came to the woman by night. And he said, "Divine a spirit for me, please, and bring up for me the one whom I name to you."
9 Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya Mfalme Sauli. Amewakatilia mbali waaguzi, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?”
The woman said to him, "Look, you know what Saul has done, how he has cut off the mediums and spiritists out of the land. Why then do you lay a snare for my life, to cause me to die?"
10 Sauli akamwapia huyo mwanamke kwa Jina la Bwana, akasema, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.”
Saul swore to her by Jehovah, saying, "As Jehovah lives, no punishment shall happen to you for this thing."
11 Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?” Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”
Then the woman said, "Whom shall I bring up to you?" He said, "Bring Samuel up for me."
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”
When the woman saw Samuel, she cried with a loud voice; and the woman spoke to Saul, saying, "Why have you deceived me? For you are Saul."
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?” Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”
The king said to her, "Do not be afraid. For what do you see?" The woman said to Saul, "I see a god coming up out of the earth."
14 Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?” Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.” Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.
He said to her, "What does he look like?" She said, "An old man comes up. He is covered with a robe." Saul perceived that it was Samuel, and he bowed with his face to the ground, and showed respect.
15 Samweli akamuuliza Sauli, “Kwa nini unanitaabisha kwa kunipandisha juu?” Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe la kufanya.”
Samuel said to Saul, "Why have you disturbed me, to bring me up?" Saul answered, "I am very distressed; for the Philistines make war against me, and God has departed from me, and answers me no more, neither by prophets, nor by dreams. Therefore I have called you, that you may make known to me what I shall do."
16 Samweli akamuuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadamu Bwana amekuacha na kuwa adui yako?
Samuel said, "Why then do you ask of me, since Jehovah has departed from you and is with your neighbor?
17 Bwana ametenda lile alilotangulia kusema kupitia kwangu. Bwana ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani Daudi.
Jehovah has done to you as he spoke by me. Jehovah has torn the kingdom out of your hand, and given it to your neighbor, even to David.
18 Kwa sababu wewe hukumtii Bwana, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, Bwana amekutendea mambo haya leo.
Because you did not obey the voice of Jehovah, and did not execute his fierce wrath on Amalek, therefore Jehovah has done this thing to you this day.
19 Zaidi ya hayo, Bwana atawatia Israeli pamoja na wewe mikononi mwa Wafilisti, na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Bwana pia atalitia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”
Moreover Jehovah will deliver Israel also with you into the hand of the Philistines; and tomorrow you and your sons with you will fall. Jehovah will deliver the army of Israel also into the hand of the Philistines."
20 Papo hapo Sauli akaanguka chini, akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala chochote mchana ule wote na usiku.
Then Saul fell immediately his full length on the earth, and was terrified, because of the words of Samuel. There was no strength in him; for he had eaten no bread all the day, nor all the night.
21 Yule mwanamke alipomwendea Sauli na kumwona amepatwa na hofu, akamwambia, “Tazama, mimi mtumishi wako mwanamke nimekutii. Nimeweka maisha yangu hatarini kwa kufanya kile ulichoniagiza nifanye.
The woman came to Saul, and saw that he was very troubled, and said to him, "Look, your handmaid has listened to your voice, and I have put my life in my hand, and have listened to your words which you spoke to me.
22 Sasa tafadhali isikilize sauti ya mtumishi wako, uniruhusu nikupatie chakula kidogo ule ili uwe na nguvu za kurejea ulikotoka.”
Now therefore, please listen also to the voice of your handmaid, and let me set a morsel of bread before you; and eat, that you may have strength, when you go on your way."
23 Akakataa, akisema, “Mimi sitaki kula.” Lakini watumishi wake wakaungana na yule mwanamke wakamsihi ale, naye akakubali. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda.
But he refused, and said, I will not eat. But his servants, together with the woman, pressed him; and he listened to their voice. So he arose from the earth, and sat on the bed.
24 Yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona hapo nyumbani, akamchinja mara moja. Akachukua unga, akaukanda, akatengeneza mkate usio chachu.
The woman had a fattened calf in the house. She hurried and killed it; and she took flour, and kneaded it, and baked unleavened bread of it.
25 Ndipo akamwandalia meza Sauli pamoja na watu wake, nao wakala. Usiku ule ule wakainuka na kwenda zao.
She brought it before Saul, and before his servants; and they ate. Then they rose up, and went away that night.

< 1 Samweli 28 >